Dr Slaa amuumbua John Tendwa

Dr Slaa amuumbua John Tendwa

tendwa kawa dpp siku hizi? Tatizo la kukosa vyama vya kusajili baada ya kuwa amesajili vyama fake mwaka jana sasa anakosa kazi za kufanya.
 
“Nimeagizwa na katibu mkuu nikujulishe kuwa hatatoa maoni kuhusu tukio lililotokea Dodoma siku ya tarehe Februari 3, 2013 kwa kuwa suala hilo ni la jinai na viongozi wa CHADEMA Mkoa wa Dodoma, wameshafungua mashtaka polisi,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo.

Batua hiyo inaongeza kuwa kutokana na suala hilo kuwa la jinai, Msajili wa Vyama vya Siasa hana mamlaka ya kulishughulikia.
 
wangetoa tu maoni yao, yanini malumbano yasiyo na tija?
Hayo ni mawazo ya kishabiki zaidi. Kumwambia ukweli Tendwa kwa kumfundisha mipaka ya mamlaka na uwezo wake ambao bahati mbaya hayajui kwa vile kila wakati anatetea unga kwa kuwakingia kifua waliomweka madarakani, kuna malubano gani? Au niulize hivi, aliyeanza malumbano kati ya Tendwa na Chadema ni nani? Majambazi wamenivamia kivulini ninapopumzika, wakang'ao utamulisho wangu na kunishushia mkong'oto, mimi nikapeleka kesi polisi, wewe unakuja kuniuliza nitoe maoni? Maoni gani umeambiwa natoka damu? Wewe ndo utoe maoni maana aliyenishushia mkong'oto na mimi wote tunalelewa na wewe. Kama wewe sio mbaguzi unapaswa kuwa mkali na kusema ukweli ukimkaripia mkorofi hata kama kakuhonga ugali. Alichemsha Tendwa. Ina maana yeye yuko nchi gani haoni ccm na vibaraka wake wanavyoutenda upinzani?
 
Washauri wa John Tendwa naona wako ktk mgomo baridi, hawawezi kuingia kwenye kesi ya jinai ambayo hawana mamlaka nayo.
 
tendwa nape ndungai makinda nchemba ...........................................wanafanana hawa waweza kuwa wa baba mmoja
 
wangetoa tu maoni yao, yanini malumbano yasiyo na tija?

maoni ni kwamba, tukio ni la jinai, hivyo basi Tendwa akae mbali na hii issue.
Tuna akili zaidi ya Tendwa anavyofikiri. yeye anataka slaa atoe tamko la kisiasa ili mwisho wa siku hii issue tuimalizie kwenye meza ya kisiasa.

 
Washauri wa John Tendwa naona wako ktk mgomo baridi, hawawezi kuingia kwenye kesi ya jinai ambayo hawana mamlaka nayo.

mkuu, Tendwa anataka dr.slaa atoe tamko la kisiasa ili mwisho wa siku tukio hili litengenezewe sura ya kisiasa per se na ofisi yake ivalie njuga kuwa ccm na chadema wamalize hii issue kwenye meza ya kisiasa.
slaa amegundua hii janja ya nyani, msimamo wetu ni kwamba hili ni tukio la jinai, hatutaki siasa hapa.
 
kumbe maoni tu, mi nilidhani ni kutoa ushaidi. ..
ishu ndogo inazua hoja na kuwa kubwa a a....
kutoa maoni ni hiari sio lazima.
 
Halafu nasikia hata Tendwa naye ni mwanansheria, hivi ukiisha kua kada wa magamba hata akili hua zinaruka? Mbona hili ni rahisi sana tu kulijua, issue tayari ipo mahakamani, sasa yeye anataka maelezo ya nini!?
 
Naona atakuwa ameamini sasa kuwa jamaa hawatanii.
 
hilo ni tatizo la kuwa kilaza na kutumia masaburi kufikiria...sasa maoni yangesaidia nin?kwani yeye Tendwa keshakua polisi au jaji?jamaa kilaza kweli.
 
Back
Top Bottom