Dr Slaa amuumbua John Tendwa

Dr Slaa amuumbua John Tendwa

Huyo rage ipo siku atampiga mtu risasi raia bila kosa,kila mara anavunja sheria hatua hazifuatwi,sidhani kama ana nguvu zaidi ya uma,sheria ifuate mkondo wake

maharage ana nguvu zaidi ya umma?! ila siku akikiasi chama cha kijani (ccm) ndipo utajua jamaa si mtanzania! ila kwa sasa aaaahh..ni mtanzania!
 
Watu wamepigwa na wengine kufa kwa siasa chafu za ccm overtime Tendwa hajawahi kusema cdm wapeleke maoni, polisi wameua watu Tendwa yupo kimya, Rais anashauriwa aunde tume ya kijaji kuchunguza vifo hajawahi kujibu hata barua. Mkutano mkuu wa ccm Rais anakiri kwa kauli yake kuwa ni mwafaka sasa ccm kuacha kulitumia Jeshi. Tendwa yupo kimya. Je kinachomuwasha ni nini kwa sasa? He iz useless
 
Sharobaro Tendwa, upara si busara! Mwanya uko hadi ubongoni!
 
Hili zee jinga sana....hebu litueleze basi kama lilimwandikia Mukama barua ya kumtaka atoe maoni yake juu ya kukatwa mapanga wabunge wa cdm kule Mwanza ukizingatia gari la mbunge wa viti maalumu (ccm)Maria hewa...lilihusika kwenye operation hiyo chafu...halafu leo anamtaka Slaa atoe maoni..shenzi zake aakafilie mbali na unafiki wake..Suala si liko mahakamani au yeye ni nani?Kwanza ni nini maoni yake kuhusu maneno yake ya uongo kuhusu washiri kule Arumeru?
 
Soon utasikia wagogo hawataki CHADEMA, hili zee bana.
 
Wakati mwingine ukimfikiria sana Tendwa na kauli zake na matendo yake unaishia kujisemea moyoni kuwa Tanzania ina hadithi za kuumiza sana mioyo! Hadithi za kuuwawa kwa Albino (ndugu zangu wa Kwembago) vikongwe na kauli za Tendwa haviachani mbali sana.

Eee Mungu niepushe na uzee wa aina hii.
 
wangetoa tu maoni yao, yanini malumbano yasiyo na tija?

Hebu wewe toa maoni yako hapa tuyaone.

uploadfromtaptalk1360327414385.jpg
uploadfromtaptalk1360327455048.jpg
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimemwandikia barua kali Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, kikisema kuwa hakiko tayari kutoa maoni kuhusu vurugu zilizotokea hivi karibuni mjini Dodoma.
Sababu kubwa iliyotajwa na chama hicho ni kwamba suala hilo ni la kijinai na msajili hana mamlaka ya kushughulikia makosa ya namna hiyo.

Msimamo huo wa CHADEMA unakuja siku chache baada ya Tendwa kupitia barua yake ya 05/02/2013, yenye Kumb. Na. AB.115/123/01A/45 kumtaka Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, atoe maoni yake juu ya vurugu zilizotokea mwishoni mwa juma lililopita.

Katika vurugu hizo wanachama wa CCM, wakiwemo viongozi, wabunge na makada waandamizi, waliwavamia na kuwashushia kipigo wanachama na viongozi wa CHADEMA.

Vurugu hizo zilitokea eneo la Mwanga Bar baada ya wafuasi wa CCM wakiongozwa na mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Rage, kung’oa mlingoti na kushusha bendera ya CHADEMA kisha kufanya mkutano wa maadhimisho ya miaka 36 ya kuzaliwa chama hicho.
CHADEMA katika barua hiyo ambayo imesainiwa na Idara ya Sheria ya chama hicho kwa niaba ya katibu mkuu wake, yenye Kumb. Na. C/ADMMSJ/04/04 ya 06/02/2013, wanasema chama hakiwezi kutoa maoni yake, kwa sababu suala hilo ni la kijinai.
Viongozi wake mkoani Dodoma, wameshafungua mashtaka, hivyo kumtaka Tendwa awasiliane na mamlaka zinazohusika na makosa ya jinai.

“Nimeagizwa na katibu mkuu nikujulishe kuwa hatatoa maoni kuhusu tukio lililotokea Dodoma siku ya tarehe Februari 3, 2013 kwa kuwa suala hilo ni la jinai na viongozi wa CHADEMA Mkoa wa Dodoma, wameshafungua mashtaka polisi,” ilisomeka sehemu ya barua hiyo.

Batua hiyo inaongeza kuwa kutokana na suala hilo kuwa la jinai, Msajili wa Vyama vya Siasa hana mamlaka ya kulishughulikia.

Source:Tanzania Daima/Nipashe

Ubongo ukiwa kibogoyo watu wazima wanatia aibu kweli!! Tendwa sasa ni kituko!
 
Tendwa zero kabisa, yaani hawezi kuficha mapenzi yake kwa chama cha CCM.
 
Huyo rage ipo siku atampiga mtu risasi raia bila kosa,kila mara anavunja sheria hatua hazifuatwi,sidhani kama ana nguvu zaidi ya uma,sheria ifuate mkondo wake

Nyie si mmewapa Al Shabab Ubunge ndani ya Bongo kana kwamba hakuna wa Tz....... Sasa endeleeni kushuhudia yanayojiri kwa huyu Al shabab......
 
Inabidi apewe mipaka ya kazi yake! Tofauti na hapo atakuwa anaumbuka kila uchao!!
 
Back
Top Bottom