Dr. Slaa amteua Mnyika kuwa Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA

Status
Not open for further replies.
Hongera John Mnyika.. Sasa ni mapambano na mafisadi kwa kwenda mbele.. Anza na hiki kifisadi mtoto cha siri siri kinaitwa Nape Nauye..
 
Mukandara acha ubishi Kijana,Wewe ni mtoto wa yule mzee wa udsm nini?Mbona mbishi sana.Maana yule mzee kashindwa kazi sasa ni kufukuza tu watoto wa masikini,eti wanaendekeza siasa wanapodai haki!!!
Mada sasa:Unafahamu Marketing "strategic plan",especially katika Siasa?Hawa watu wa hapa JF nani anawajua zaidi yako?Bavicha hapa Kijijini anajulikana Heche Peke yake maana kila siku wanamuona Star TV.Sasa kazi ya Uenezi unaona kama nyepesi ya kupewa tu mtu sio?Poor marketing plan hiyo.PSG wanapotaka kumsajili Beckham sio kwamba sasa anamzidi Ronaldo au Rooney,au Ile timu ya Uchina sio inamtaka Drogba na imemchukua Anelka kwa sababu wataibebesha ubingwa la hasha,Anzhi Makachakala ilipomchukua Etoo ilikuwa na ajenda nyuma sio ubingwa.Ni kweli Mnyika majukumu mengi sana,lakini kwa faida ya chama,ni lazima awe yeye TU for the time being.Hivi huyo tumbo zaidi ya Igunga,huku kwetu swekeni unafikiri nani anamjua?Hata mijini kwenyewe nani anamjua?Hapa Chadema imelenga kuwashika masikio Wananchi wengi,lakini hizo kazi si anaweza kuwa na wasaidizi lukuki ili kumrahisishia majukumu,kama alivyokuwa na yeye anakaimu nafasi ya Dr.wakati wa kampeni.Hapana,kwa hili una lako jambo,Dr.Slaa hajawahi kukosea uteuzi baba,Mnyika ni sahihi kabisa kwa sasa,otherwise Hueleweki Bro.Nafasi nyingine huhitaji zaidi "Celebrities" ili ku-capture MARKET hasa Vijijini,maana ndiko Mnyika anajulikana kuliko sisi wa mjini tunaoshinda hapa JF,you know kuna watu hapahapa mjini tena wanafunzi wa vyuo vikuu hawajui JF ambako unawataja Kina Lunyungu et al.
Hawa kina Lunyungu Kama uteuzi wa Uenezi hapa JF,kama wasipoteuliwa wao hapo tutaandamana na kusema kweli kuna upendeleo.Nakumbuka Lema alipokuwa anazindua Tawi la Chadema Pale Chuo Cha Uhasibu Njiro,alituambia kwamba,Sisi tunaojiita wasomi kazi yetu kubwa ni kueneza chama kupitia Mitandao,kazi nzuri sana inafanywa na hao uliowataja Mukandara.Na ndio sehemu yetu sahihi kabisa.
 
Hao uliowataja wamekuambia wanaiweza hiyo nafasi? Je wamekumbia hawana majukumu kiasi hawatatingwa kama wangeteuliwa kwenye hiyo nafasi?


Hujamuelewa Mkandara,
Anachohoji yeye ni kwanini Mnyika ambaye tayari ana majukumu mengi alundikiwe majukumu mengine as if hakuna vijana wengine wakati kuna watu wako kwenye mitandao kwa muda mrefu?

Kuna mdau akamuuliza walau majina matano tu ya vijana anaowafahamu na kudhani kwamba wanaiweza kazi hiyo, ndipo akawataja hao unaomuuliza kama wako tayari kufanya kazi hiyo. Na sidhani kama chama kinaweza kukosa watu nje ya wabunge, wapo wanachama wengi sana wenye uwezo na nia ya kukitumikia ni suala la kuaminiwa na kupewa nafasi!
 
Hatimaye katibu mkuu wa chadema dr slaa amemteua rasmi mbunge wa jimbo la ubungo JOHN MNYIKA kuwa mkurugenzi wa habari na uenezi wa CHADEMA taifa na kumshusha ndg ERASTO TUMBO KUWA afisa ndani ya kurugenzi source TBC TAARIFA

Hongera yako hata kwa kuwa unaangaliaga TBC bado!

Thankx Best!
 
Wee waulize hawa hawa kama wananjua Robert Gibbs ktk siasa za Marekani..wachache sana wanamjua, wengine utaona wanakimbilia Google kwa sababu tumezoea siasa za kujuana...

I'm Sorry Dr.Slaa nadhani ktk hili kachemsha maana uwezo pekee hauwezi kuwa kigezo bali nafasi muda na kuelewa vyanzo vipi unatakiwa wakati muafaka na sii kusubiri vitu vimekwisha tokea kama zilivyo siasa za Bongo. Unaanda mikakati mbele ya safari na inahitaji muda mkubwa sana na ujuzi wa kazi hiyo jambo ambalo vyama vyetu vina mapungufu sehemu zote hizi.
Kumbe ulikuwa unakuja huku, mwanzo umepongeza uteuzi wa Mnyika sasa unaponda aliyemteua can you declare your interest.
 
Kweli, kama ni jembe basi limepata mlimaji, na kama ni mashua, imepata nahodha wa ukweli kabisa. Sina kipingamizi wala shaka yoyote juu ya uteuzi na mtu aliyeteuliwa. Naamini kichwa cha Dr. Slaa siyo kama cha Dr. Bana au Dr. Dr. Kikwete ambacho kinafanya kazi kupitia mawazo ya watu kama akina Tyson na Mzee Kingunge.
Swali, Mnyika ataweza kutimiza majukumu yake kama mbuge, kama mkurugenzi wa mambo ya nje ya chama, kawa waziri kivuli nimesahawa sijui wa nini... na kama mkurugenzi wa habari na uenezi wa chama?
Hivi hakuna uwezekano wa kumpunguzia majukumu ili yale machache atakayobaki nayo ayafanye kwa ufasaha na kwa matunda ya chama ili ukombozi 2015 uwe wa uhakika? Ni mawazo na mtazamo tu....!!!
 
Japokuwa watu wengi wanaweza wasielewe unachokisema Mkandara kwa ajili ya mapenzi waliyonayo juu ya Mnyika lakini ni jambo muhimu sana ambalo lilitakiwa kutafakariwa kwa undani na Chadema kabla ya kufanya uteuzi.
Mnyika mara kadhaa anasema kwamba yuko busy anashindwa kuwa available, kwa maana hiyo kumuongezea majukumu mimi naona ni kumpunguzia ufanisi.
Kila la kheri Mnyika kwenye majukumu yako mapya
Anashindwa kuwa available wapi.
 
Mukandara acha ubishi Kijana,Wewe ni mtoto wa yule mzee wa udsm nini?Mbona mbishi sana.Maana yule mzee kashindwa kazi sasa ni kufukuza tu watoto wa masikini,eti wanaendekeza siasa wanapodai haki!!!
Mada sasa:Unafahamu Marketing "strategic plan",especially katika Siasa?Hawa watu wa hapa JF nani anawajua zaidi yako?Bavicha hapa Kijijini anajulikana Heche Peke yake maana kila siku wanamuona Star TV.Sasa kazi ya Uenezi unaona kama nyepesi ya kupewa tu mtu sio?Poor marketing plan hiyo.PSG wanapotaka kumsajili Beckham sio kwamba sasa anamzidi Ronaldo au Rooney,au Ile timu ya Uchina sio inamtaka Drogba na imemchukua Anelka kwa sababu wataibebesha ubingwa la hasha,Anzhi Makachakala ilipomchukua Etoo ilikuwa na ajenda nyuma sio ubingwa.Ni kweli Mnyika majukumu mengi sana,lakini kwa faida ya chama,ni lazima awe yeye TU for the time being.Hivi huyo tumbo zaidi ya Igunga,huku kwetu swekeni unafikiri nani anamjua?Hata mijini kwenyewe nani anamjua?Hapa Chadema imelenga kuwashika masikio Wananchi wengi,lakini hizo kazi si anaweza kuwa na wasaidizi lukuki ili kumrahisishia majukumu,kama alivyokuwa na yeye anakaimu nafasi ya Dr.wakati wa kampeni.Hapana,kwa hili una lako jambo,Dr.Slaa hajawahi kukosea uteuzi baba,Mnyika ni sahihi kabisa kwa sasa,otherwise Hueleweki Bro.Nafasi nyingine huhitaji zaidi "Celebrities" ili ku-capture MARKET hasa Vijijini,maana ndiko Mnyika anajulikana kuliko sisi wa mjini tunaoshinda hapa JF,you know kuna watu hapahapa mjini tena wanafunzi wa vyuo vikuu hawajui JF ambako unawataja Kina Lunyungu et al.
Hawa kina Lunyungu Kama uteuzi wa Uenezi hapa JF,kama wasipoteuliwa wao hapo tutaandamana na kusema kweli kuna upendeleo.Nakumbuka Lema alipokuwa anazindua Tawi la Chadema Pale Chuo Cha Uhasibu Njiro,alituambia kwamba,Sisi tunaojiita wasomi kazi yetu kubwa ni kueneza chama kupitia Mitandao,kazi nzuri sana inafanywa na hao uliowataja Mukandara.Na ndio sehemu yetu sahihi kabisa.
Kwa nini naitwa mimi mbishi ikiwa nilichokiona nyie hamkukiona?.. hatuzungumzii kitu kimoja hapa. Mbishi ni yule anayekataa kwamba Mnyika hana uwezo na ha qualify bali nachosema Vyeo hivi vinawabana viongozi ktk utendaji kazi wao kiasi kwamba watakuja shindwa jambo muwaone wao wabovu kumbe sisi wenyewe ndio tumekosea...Nini hizi kofia 10 maana mbili pekee mmeona hazitoshi? hawa ni miungu watu wana nguvu za ajabu?

Sina mahusiano na Mukandara hivyo sijui mbishi nani kati yangu na wewe maana ndivyo mnavyofikiria kila siku kumtazama mtu sura, kundi gani na nafasi yake kisha mnatoa hukumu..hao kina Dragba, Beckham na Etoo wana vyeo gani vya uongozi wa team zao management apart from being Captain uwanjani?..
 
Kumbe ulikuwa unakuja huku, mwanzo umepongeza uteuzi wa Mnyika sasa unaponda aliyemteua can you declare your interest.
Kwa kuzingatia majukumu mengine alokuwa nayo Mnyika na sii vinginevyo!...Nilijua tu mawazo yenu yameganda sana ktk mitandao. Nina hakika kabisa ndivyo wengi hapa wanafikiria hivyo lakini amini maneno yangu nampenda sana Mnyika japokuwa sikufurahia sana kutokuwepo hapa JF baada ya kuwa mbunge na yeye akanambia ametingwa sana na majukumu.

Niliheshimu mawazo na maamuzi yake ingawa nina kisongo na wabunge karibu wote wa Chadema ambao waliitumia sana JF kujijenga leo wametukimbia.. Hiyo nitasema kweli wala sintoficha.

Sehemu ambazo mtazamo wangu kiongozi yeyote akivurunda wala simwachi iwe yeye Zitto, Mbowe au Dr.Slaa kwa sababu nadhani ninawajibika kwa chama na sio Mbowe, Zitto wala Mnyika..Na nimekwenda hadi Kitaifa kwa JK sii kwa sababu ni mwana CCM bali nikiona makosa nayasema bila kujali chama wala yeye nani isipokuwa heshima yake kama rais wangu nitampa - Unafiki kwangu haramu ya kwanza!
 
Hapana mkuu wangu wewe nadhani ndio unapotoka maana hata Rais anapotoa hotuba huandikwa na watu ambao hawapo ktk siasa. Press Scretary wa Obama au Romney, Ron Paul na wengineo hawa sii wanasiasa kwa jinsi unavyowafikiria bali hawa ni watu wanajua mbinu za kupanga vitu kisomi na utaalam maana kiongozi wake tayari anazo nyenzo za kisiasa..

Mnyika ni mwanaSiasa, mbunge mwenyekiti sijui waziri kivuli hivyo ni vigumu sana yeye kuweza kuwa na muda wa kuyafanya yote haya. Mathlan, Hivi Salva ni mwanasiasa kwa mtazamo wako au mapungufu yake yanatokana na kutokuwa mwanasiasa?...Sio lazima Mnyika ndiye awe anajibu kama alivyosema Soby bali kuandaa shughuli za chama iwe mahojiano, makutano na kadhalika. Na kwa mfano unapo chat na Obama Tweet au JK haina maana huyo ni Obama au JK mwenyewe bali ni imetokana na maadalizi yamefanya ktk idara yake ya mawasiliano..

Sina uhakika Mnyika atakuwa na muda huo wa kushinda makao makuu akiweka mikakati ya chama wakati ana majukumu Ubungo, bungeni sijui uwaziri kivuli wakati wapo watu Chadema wamesoma na hata kama hawaelewi somo hili, wataiweka kazi kama wataelekezwa vizuri kwani huyo Mnyika katokea wapi jamani?

Mkuu huku majuu maadam una elimu tosha, ari na uwezo unao kinachotakiwa ni maelekezo ambayo msomi anaweza chukua nyaraka akazisoma nyumbani kujua kazi zake. Wewe unaweza na wengine wote nilowataja wanaweza hata huyo Tumbo anayedharauliwa naweza ndio maana kachaguliwa nafasi nyingine.

Again why tunakazania hili? Mnyika kisha chaguliwa haina neno lakini nasema hivi mna mzeesha dogo mapema kwa kumpa majukumu makubwa wakati muda wenyewe hana.....Ni ushauri tu.
Tatizo lako unafananisha cheo cha katibu mwenezi na press secretary au mkurugenzi wa mawasiliano ikulu kama Soby anavyodhani, katibu mwenezi si mtu wa kumjibia Mbowe emails zake au tweets za Katibu mkuu is a political position, is a lobbying post ni zaidi ya press secretary, Salva haandiki speech na kuipeleka jukwaani anampa mwanasiasa akaisome aisome vipi ni juu ya mwanasiasa si juu ya Salva au secretary wa Obama. Tofauti yake na post ya Mnyika, Mnyika anatakiwa aandae speech yake halafu akaiuze mwenyewe kwenye majukwaa uenezi ni zaidi ya kutweet ndugu yangu.

Anyway kama ulivyosema Mnyika ameshachaguliwa binafsi nina imani naye tena sana, ila jaribu kuwa gentleman uwe na positive thinking kwa vijana badala ya kusema wana mzeesha dogo sema wana mkomaza.
 
Simply wewe huzijui siasa za bongo mwisho utasema anaweza akatuma hata mkanda wa video hata tape recoder kwenye mikutano na yeye asiende.
Mkuu siasa za bongo ndiyo zinatumaliza...
Siyo kwa sababu CCM wanagawa pilau, basi na vyama vingine vidai pilau.

Hivi wewe unaweza kumuita Karl Rove mwanasiasa?.... Ila hao ndiyo maengineer wa siasa.
Campaign managers kama kina Abdulrahman Kinana huwa wanakalishwa mbali na everyday politics ..... ni watu ambao huwasikii ila ndio matechnocrats wenyewe wa CCM.
Sasa kwanini Dr. Slaa hapangiwi lectures?, hawamschedule kwenye internet radios..., local radios

Kwanini CDM wanashindwa kutafuta watu 1000 ambao watakuwa tayari kuanza kufundishwa udiwani? i.e Sheria, majukumu na jinsi ya kukampeni kwa ajili ya 2014?... hii yote ni kwa sababu hakuna PR....

Ila kama mtaendelea kuwaweka wanasiasa kwenye mambo ya kitaalam, ndivyo hivyohivyo mtawaweka kina Mnyika au Heche kuwa wakurugenzi wa Tanesco mkipata nchi (I doubt if that will happen).
 
Tatizo lako unafananisha cheo cha katibu mwenezi na press secretary au mkurugenzi wa mawasiliano ikulu kama Soby anavyodhani, katibu mwenezi si mtu wa kumjibia Mbowe emails zake au tweets za Katibu mkuu is a political position, is a lobbying post ni zaidi ya press secretary, Salva haandiki speech na kuipeleka jukwaani anampa mwanasiasa akaisome aisome vipi ni juu ya mwanasiasa si juu ya Salva au secretary wa Obama. Tofauti yake na post ya Mnyika, Mnyika anatakiwa aandae speech yake halafu akaiuze mwenyewe kwenye majukwaa uenezi ni zaidi ya kutweet ndugu yangu.

Anyway kama ulivyosema Mnyika ameshachaguliwa binafsi nina imani naye tena sana, ila jaribu kuwa gentleman uwe na positive thinking kwa vijana badala ya kusema wana mzeesha dogo sema wana mkomaza.
No sir,
Najua katibu mwenezi maana yake...
Publicity Secretay.. a.k.a Public relations secretary.
Kazi yake kuu ni ku-publicize, especially wanasiasa wa CDM....
Siyo position ya kisiasa hata kidogo, ila vyama vyetu ni vyama vya kimjinimjini kwa hiyo it's okay.
Hiyo position ni ya kitaaluma..... Negative ads, websites, TV, that is public relations. It's PR usipende kubisha vitu usivyoelewa.
Ila mwisho wa siku ni maamuzi ya Chama, na wewe kama mwanachama umefanya vizuri kupongeza uamuzi huo, tusigombane.
 
By considering the mathematics of time allocation per specified jobs per Mnyika, we come out with this logic

1. Chadema doesn't have enough funds to allocate a share for a Katibu Mwenezi, so is asking Mnyika who has pretty good salary to do it for free

2. Apart from Mnyika's job at Ubungo, the rest are not important, so he can allocate his free time for the rest of them (*take out minimum of 8hours for Ubungo per day sans the weekends)

3. Chadema is asking Mnyika knowingly to slack on all his jobs, so he can do a somewhat okay job in all of them

4. Chadema doesn't have enough people to do its job, so it has to apply 'The three R" process for the few it has

5. Mnyika is a robot
 
sasa napendekeza cdm ianze mchakato wa kumtafuta mrithi wa mnyika ubungo kwani kazi za ubunge zinamshinda. Anafaa za kitaifa zaidi
 
sasa napendekeza cdm ianze mchakato wa kumtafuta mrithi wa mnyika ubungo kwani kazi za ubunge zinamshinda. Anafaa za kitaifa zaidi
Nakubaliana na Mkandara,tumepigia sana kelele mambo ya kurundikiana vyeo alafu tunafanya yale yale! Mnyika ni Mbunge,ni waziri kivuli sasa mwenezi! Kweli kuna ufanisi hapa! Uwezo anao ndio lakini mbona CDM ina vichwa kibao? Tukubali kujikosoa!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom