Dr. Slaa alikuwa CCM kabla ya kujiunga na CDM, kilitokea nini pale karatu?

Ilikuwa uchaguzi mkuu wa mwaka 1995, ambapo katika kura za maoni za ccm, dr. Slaa alimshinda mpinzani wake Patrick Qoro ambaye kwa wakati huo alikuwa mbunge anayelitetea nafasi yake ya ubunge, na dr. slaa alikuwa diwani kupitia ccm pia kwa wakati huo.

Kama kawaida ya ccm huwa wanautaratibu wa kupeleka majina ya wagombea kuanzia mshindi wa kwanza mpaka wa tatu kwenye kamati kuu, ambayo ndiyo itakayoamua nani awe mbunge.

Majina yalipopelekwa dodoma, kamati kuu ya ccm waliamua kulirejesha jina la Patrick Qoro kutetea nafasi yake ya ubunge kwenye uchaguzi mkuu, kwa kigezo kwamba Dr. Slaa alikuwa hauziki kwa wananchi wa karatu.

Matokeo hayo yaliwakasirisha sana wananchi wa karatu, mpaka wakaamua kuandamana mpaka nyumbani kwa Dr. Slaa, wakamwambia chagua chama chochote cha siasa tutakuchagua. Kabla Dr. Slaa hajaamua nini cha kufanya, wazee wakawa wamemletea fomu ya kugombea ubunge kupitia chadema, wakamwambia saini hapa na usipige kampeni kaa nyumbani sisi tutamaliza kazi. Dr. Slaa hakuwa na lakufanya, ilibidi akubali sauti ya wengi, ambayo ni sauti ya mungu.

Mkuu hapo kwenye red uhakika ukoje, maana ndio mara yangu ya kwanza kusikia.
 
Siasa bana ni mchezo wa ajabu sana. Najaribu kufikiri...JK alikuwa anasubiriwa na CDM mwaka 2005 awe mgombea wake wa urais. Na sababu ni kwamba Big Ben hakumtaka katakata huyu mtu wa Msoga. Na kina EL walijua, na ndio maana CDM ilikuwa ya mwisho kabisa kumtaja mgombea wake wa Urais baada ya kupikwa zengwe kuwa Baregu(PhD) eti alikuwa mgonjwa asingeweza kugombea urais. Na ndipo ilipobidi Mbowe aache jimbo lake na kugombea.
Kama Big Ben angepuuza ushauri wa TISS kuwa nguvu ya JK wakati huo hata angehamia UDP(Mkumbuke kuwa Mangula alichimba Mkwara kupitia BBC Swahili kuwa wana taarifa Mgombea wao mmoja mwenye nguvu anataka kuhamia upinzani lakini atashughulikiwa kama Mrema) angeshinda basi huu upuuzi wote wa JK kwa sasa ungekuwa wa CDM. Sasa ninapooanisha na namna Slaa(PhD) alivyohama CCM na jinsi CDM ilivyokuwa inamdondoshea udenda JK naona siasa kama jukwaa la dhihaka tu
 
Nadhani katika mambo ambayo CCM haitakaa kusahau na itaendelea kujuta mpaka siku kitakapokuwa chama cha upinzani ni pamoja na kuleta mizengwe pale karatu wakati wa kura za maoni kati ya Dr Slaa na aliyekuwa mbunge wa karatu enzi hizo aliyekuwa anaitwa Qoro kupitia CCM. kulikuwa na mizengwe ambayo ilimpelekea Dr. Slaa kuhamia CDM.

Ilikuaje, ni kilitokea, hebu tukumbushane hii historia nzuri kwa CDM na upinzani kwa ujumla, kama kuna mtu anaelewa vizuri nini kilitokea.
mimi nilikuwa hata sikujua kama ndivyo alivyoingia upinzania, lakini nadhani issue si majuto ya alikotoka bali tujiulize mimi, wewe na wanzania kwa ujumla tunajifunza nini kuhusu mtu kujiengua huku na kwenda kule hasa baada ya kukosa kitu fulani!
 
Wala usishangae, Huyo Slaa mwenyewe akibahatika akaingia ikulu atafanya mambo ya ajabu sasa sijui utazimia au la! kama aliweza kujiengua CCM eti kisa hakupitishwa kura za maoni mimi binafsi I dont think if he is a good person. Nadhani goals ni zile zile walizo nazo wote waliojiengua chama hiki na kuingia kile km vile Mpendazoe, Shitambala, Shibuda, Prof Safari, Wilfred Lwakatare na wengine wengi. If I was me wote hao lengo lao ni keki siyo maslahi ya Watanzania
 
Mkuu hapo kwenye red uhakika ukoje, maana ndio mara yangu ya kwanza kusikia.

Sahihisho: Dr. Slaa mwaka 1995 kwenye harakati za kugombea ubunge wa karatu, pia alichukua fomu ya kugombea udiwani wa kata ya Endarofta kwa tiketi ya ccm, alikuja kuitema baadaye kutokana na kuhamia chadema.
 
Ilikuwa hivi;
Wananchi wa Karatu walichoshwa na mbunge wao wa wakati huo ambaye alikuwa anaitwa Matheo Quaresh kama sijakosea jina. Wakatuma ujumbe kumfuata Dr. Slaa ambaye alikuwa anaishi Dar kumwomba akagombee ubunge Karatu. Alikubali na akaenda kuchukua form kwenye chama chake cha CCM kuomba ateuliwe kuwa mgombea ubunge jimbo la Karatu kwa tiketi ya CCM.

Katika kura za awali ambazo ni kura za maoni Dr. Slaa aliibuka kidedea mshindi dhidi ya Matheo Quoresh. Mizengwe kama kawaida ya CCM iliibuka kwenye kupitia kura za maoni kitaifa ambako jila la Dr. Slaa lilitupwa nje ya uringo kwa hoja iliyozoeleka kwamba si mwenzao, na wakapitisha jina la mbunge wa zamani kuendelea kutetea kiti hicho na Dr. kutupwa nje bila ridhaa ya wananchi bali na kikundi kidogo cha vigogo wa CCM wenye hulka ya kulinda.

Wananchi wa Karatu waliporudishiwa jina la mgombea ambaye wao hawakumtaka, walilikiataa katakata na kumwomba Dr. Slaa agombee kupitia chama kingine cha siasa na kumwahidi kumpigia kura si kwa mlengo wa kichama ila uwezo wake. Na tukumbuke kabla yake Dr. alishafanya huduma nyingi za kijamii wakati yupo katika kofia nyingine. Dr. Akakubali na kuwa na mtihani wa chama gani agombee ubunge maana ni mambo ya papo kwa papo.

Sera za Chadema zilimvutia na hivyo kuamua kuwasikiliza wananchi Karatu kilio chao na kugombea ubunge. Na kwa mshangao mkubwa katika uchaguzi huo alimtupa mbali sana mpinzani wake kutoka CCM na hivyo kuanza kuliongoza jimbo la uchaguzi la Karatu na kugeuka kuwa ngome ya upinzani wakati ilikuwa bustani ya uhakika ya CCM kwenda chuma matunda mazuri wayapendayo.

Nyerere alitoa kauli yake kwa yaliyojilia kwa kusema, watu hawa nawafahamu, na kwamba siku za nyuma jambo kama hili lilishatokea kwa kutoa mfano ambao kwa sasa siukumbuki. Alisema watu hawa wakishaamua juu ya mtu wao wanayemtaka, waachieni vinginevyo ni kuumbuka kama ilivyotokea.

Ukweli ni kwamba CCM hawapendi kuongelea jambo hilo, kinachofanyika ni kufunikafunika ukweli, lakini kwa sasa kinachoendelea ni kile tunachoweza kujifunza toka Biblia kwamba "Jiwe la pembeni lililokataliwa na waashi limekuwa jiwe kuu la msingi.



"Jiwe lililokataliwa na waashi limekuwa jiwe kuu la msingi!"

Inasemekana 2015 Mbowe mwenyewe anagombea sasa SLAA atahama chama tena kwa vile wananchi wanampenda? Hapa sasa mtihani, Jamani mimi bado nakataa hii dhana ya kuhama kwa visingizio kuwa wananchi wanampenda. Huyu bwana alikuwa Dar es Salaam siku zote , maneno wananchi walikuwa wanampenda walimjulia wapi? Tutafute Interest za aina hii ya watu wa kutoka chama hiki kwenda kule ni nini? Nini kimejificha nyuma ya pazia hili? Sisemi kwamba SLAA hafai ila naongelea ujumla wa watu wa aina hii
 
Always kama plan A imebuma lazima uangalie plan B. nakwa taarifa yako plan B must prove to be better tha plan A. ok
 
Ijapokuwa nilikuwa std 1 nilichokisikia toka kwa wazee waliokuwa wanampigania dr. Slaa ni kuwa walikuwa hawamtaki patrick Qoro ambaye alikuwa mbunge wetu kabla, wazee wakatumwa kwa dr. Slaa ili aweze kugombea ubunge na wakamsisitizia kuwa wao hawataangalia ni chama gani kimemsimamisha(kwa utamaduni wa wairaqw ukiletewa majani kukuomba hauwezi kukataa) naye akaamua kukubali lakini yeye akawaambia kuwa atagombea kwa tiketi ya ccm, basi muda ukafika akachukua form kupitia magamba ktk kura za maoni akamshinda patric Qoro lakini cc ikapitisha jina la PQ. Akakaa chini akitafakari maneno ya wazee waliotumwa kwake kuwa ss hatutaangalia chama kitakachokusimamisha naye akaona chadema ni chama chenye sera zuri na malengo yanayoweza kuwatoa ccm madarakani siku za usoni, hatimaye akachukua form kwa tiketi ya chadema kampeni zikaanza hatimaye uchaguzi naye akatangazwa mshindi, PQ akakata rufaa na akashindwa vby tena na akatakiwa kulipa fidia kwa dr. Slaa naye akaamua kumsamehe. Matamshi ya Nyerere yalikuja kutokana na kumbukumbu aliyonayo baada ya uhuru ya chief DODO NA CHIEF SARWATT cc ya wakati huo ilimpitisha chief dodo kaka mwakilishi wa jimbo la mbulu(ikumbukwe by that time karatu,mbulu,babati na hanang zilikuwa jimbo moja la mbulu), sarwat akasimama independently na na akashinda mpaka chama kikabadilisha mfumo wa kuwapata wagombea wake so till this time tuna historia nzuri kuhusu kukua kwa demokrasia. Addition zinaruhusiwa na kuchallenge nilichokiandika. Thanks.
 
Ijapokuwa nilikuwa std 1 nilichokisikia toka kwa wazee waliokuwa wanampigania dr. Slaa ni kuwa walikuwa hawamtaki patrick Qoro ambaye alikuwa mbunge wetu kabla, wazee wakatumwa kwa dr. Slaa ili aweze kugombea ubunge na wakamsisitizia kuwa wao hawataangalia ni chama gani kimemsimamisha(kwa utamaduni wa wairaqw ukiletewa majani kukuomba hauwezi kukataa) naye akaamua kukubali lakini yeye akawaambia kuwa atagombea kwa tiketi ya ccm, basi muda ukafika akachukua form kupitia magamba ktk kura za maoni akamshinda patric Qoro lakini cc ikapitisha jina la PQ. Akakaa chini akitafakari maneno ya wazee waliotumwa kwake kuwa ss hatutaangalia chama kitakachokusimamisha naye akaona chadema ni chama chenye sera zuri na malengo yanayoweza kuwatoa ccm madarakani siku za usoni, hatimaye akachukua form kwa tiketi ya chadema kampeni zikaanza hatimaye uchaguzi naye akatangazwa mshindi, PQ akakata rufaa na akashindwa vby tena na akatakiwa kulipa fidia kwa dr. Slaa naye akaamua kumsamehe. Matamshi ya Nyerere yalikuja kutokana na kumbukumbu aliyonayo baada ya uhuru ya chief DODO NA CHIEF SARWATT cc ya wakati huo ilimpitisha chief dodo kaka mwakilishi wa jimbo la mbulu(ikumbukwe by that time karatu,mbulu,babati na hanang zilikuwa jimbo moja la mbulu), sarwat akasimama independently na na akashinda mpaka chama kikabadilisha mfumo wa kuwapata wagombea wake so till this time tuna historia nzuri kuhusu kukua kwa demokrasia. Addition zinaruhusiwa na kuchallenge nilichokiandika. Thanks.

uko sahihi kabisa atakayepinga uliyoyaeleza atakuwa haijui hii 'issue' vizuri,mimi natokea karatu hata sasa(currently) niko krt,mi sifungamani na chama chochote cha siasa niko 'politically non-aligned to any party' ila Dr. slaa ni kiongozi mwenye sifa nyingi(siyo zote) za kiuongozi ila amekosa sifa kuu moja (1)alipokuwa mbunge kwenye awamu yake ya mwisho(2005-2010) alishindwa kabisa kupambana na mafisadi wa ndani ya chama chake ambao ni mafisadi tu kama hawa wa ccm!,m/keti wa halmashauri ya krt ambaye pia ni diwani wa kata ya Ganako(Lazaro Titus Massay) ni fisadi tu kama mafisadi wa ccm wala hana tofauti nao maana amekomaa kuuza viwanja/mashamba na maeneo ya wazi ya vijiji vya Tloma na Ayalabe tangu slaa akiwa mbunge amemtetea sana huyu jamaa ili kuepusha mgawanyiko ndani ya chama hapa krt,huyu jamaa aliuza mpk eneo la shule ya secondary ya Welwel iliyoko kata ya krt mjini(kwa m/keti wa bodi ya maji ya KAVIWASU na diwani wa krt mjini ambaye ni hasimu wake ktk kugombania uenyekiti wa halmashauri!,huyu m/keti wa bodi ya maji/diwani wa krt mjini(Jublete Gerson Mnyenye naye ni fisadi tu wa kuchanganya maslahi yake binafsi na bodi 'conflict of interests' kwa kuchelewesha 'pipe installation' kweye visima vilivyochimbwa ili visima vyake viendelee kupiga 'deal',manager wa bodi ya maji(Ticha) huyu ndiyo fisadi kuliko hata m/keti mwenyewe,infact bodi ya maji imegeuzwa kuwa mradi wa watu binafsi,simu yangu imeisha chaji nitawaeleza mengi kuliko haya maana mimi napenda sana mabadiliko na pia nakubali harakati za slaa kuikomboa nchi kutoka kwa mafisadi na wadhalimu(ccm) ila nahoji uwezo wake wa kupambana na mafisadi watakao ibukia ndani ya chama chake ngazi ya taifa atakapochukua dola maana atawezaje kupambana nao ikiwa madiwani wake(walio chini yake) walimshinda akiwa mbunge!?
 
Mkuu mateo Qaresi alikuwa mbunge wa babati siyo karatu.

Asante, majina haya ya kiiraq yanatuchanganya wengine sijui quoro or quoresh, nadhani maudhui yameeleweka, asante sana kwa kusahihisha, ndo maana nilisema sina hakina na jina hilo.
 
Chadema ni kiusiwa cha makapi? Waliotoswa na CCM wote wanapokelewa CDM

u must have a problem... we hujui nchi hii ilikua na mfumo wa single party hivyo by default every citizen alikua member wa ccm!!! au umesau mitaala ya shule ya msingi ilivyokua imeandaliwa ??
think critically acha kutumia masaburi kufikiri..over
 
Inasemekana 2015 Mbowe mwenyewe anagombea sasa SLAA atahama chama tena kwa vile wananchi wanampenda? Hapa sasa mtihani, Jamani mimi bado nakataa hii dhana ya kuhama kwa visingizio kuwa wananchi wanampenda. Huyu bwana alikuwa Dar es Salaam siku zote , maneno wananchi walikuwa wanampenda walimjulia wapi? Tutafute Interest za aina hii ya watu wa kutoka chama hiki kwenda kule ni nini? Nini kimejificha nyuma ya pazia hili? Sisemi kwamba SLAA hafai ila naongelea ujumla wa watu wa aina hii

Mbona rahisi hiyo mbona walimchagua kuwa mbunge wao kwa miaka 15 mfululizo mpaka alipoacha mwenyewe? Halafu suala jingine ambalo unapaswa kujua ni kwamba yeye aliwahi kuwahudumia kama padre tangu mwaka 1977 mpaka alipoacha upadre 1990 kwa hiyo walimfahamu pamoja na kwamba alikuwa Dar. Pia suala jingine la kuangalia ni kitu gani amefanyia jimbo lake na taifa baada ya kuhama, kwa jambo hilo naomba tuwe specific zaidi na sio general.
 
Sahihisho: Dr. Slaa mwaka 1995 kwenye harakati za kugombea ubunge wa karatu, pia alichukua fomu ya kugombea udiwani wa kata ya Endarofta kwa tiketi ya ccm, alikuja kuitema baadaye kutokana na kuhamia chadema.

Mungi
Ni vizuri kuwa na facts kabla ya kuchangia jambo. Ni vizuri zaidi kuyochangia kama huna uhakika. Karatu hakuna kata ya Endarafta kati ya Kata 13 zilizokuwepo 1995. Dr Slaa pia hakuchukua fomu ya udiwani. Baada ya kushinda ubunge alikuwa diwani kwa mujibu wa sheria kama walivyo wabunge wote,
 
Mungi
Ni vizuri kuwa na facts kabla ya kuchangia jambo. Ni vizuri zaidi kuyochangia kama huna uhakika. Karatu hakuna kata ya Endarafta kati ya Kata 13 zilizokuwepo 1995. Dr Slaa pia hakuchukua fomu ya udiwani. Baada ya kushinda ubunge alikuwa diwani kwa mujibu wa sheria kama walivyo wabunge wote,

Hata mimi nilikuwa nashangaa kauli ya Slaa kuchukua form ya kugombea udiwani na wala kwenye kumbukumbu hakuna alipokuwa diwani zaidi ya kuhudhuria vikao vya madiwani kwa tiketi ya ubunge. Asante Dr. kwa ufafanuzi.
 
Back
Top Bottom