Jerry Slaa: Serikali isikubali kuyumbishwa na Watu wenye nia ya Kuona Tanzania haiendelei kiuchumi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 53 leo Juni 22, 2023



Mbunge wa Ukonga Mhe. Jerry Slaa amesema Serikali ipokee mawazo mazuri ya wananchi lakini isikubali kuyumbishwa na watu wasioitakia mema nchi yetu.

"Niiombe Serikali ikubali ushauri, isikilize wananchi lakini wakati mwingine isikubali kuyumbishwa na watu wenye nia zao za kuitaka nchi yetu isiendelee kiuchumi, ikubaliane na hoja za msingi za kuendeleza taifa letu, tuwe na uwekezaji na kushirikisha sekta Binafsi kwenye yale maeneo ambayo wenzetu wamebobea, tupate uwekezaji mzuri wa Bandari" amesema Jerry Slaa.

Jerry Slaa1 ed1.jpg

Jerry Slaa, Mbunge wa Ukonga (CCM)
Mhe. Slaa ametamka maneno haya wakati akisisitiza umuhimu wa Serikali kushirikiana na Sekta binafsi katika kukuza maendeleo ya taifa huku akitolea mfano wa Hayati Benjamin Mkapa alivyokumbana na upinzani mkubwa wakati wa ubinafsishaji wa benki ya NMB, benki ambayo kwa sasa inajiendesha kwa faida kubwa.

Pia, amesisitiza hadi sasa Serikali haijasaini mikataba ya Utekelezaji uwekezaji wa Bandari Nchini, bali imeingia makubaliano ya awali (IGA), na mikataba ya utekelezaji itasainiwa baadae.

Stahiki za Jeshi la Magereza zitazamwe upya
Mbunge wa viti maalumu Esther Matiko amesema askari wa jeshi la Magereza wanafanya kazi wakiwa kwenye mazingira magumu.

Amedai kuwa kuna Askari Magereza wametumikia nchi kwa zaidi ya miaka 26 bila kupandishwa vyeo huku utaratibu ukidai kila baada ya miaka 3 wapandishwe vyeo.

Esther Matiko.jpg

Esther Matiko, Mbunge wa viti Maalum
Askari hawa kwa muda mrefu wamekuwa pia wanadai madeni mengi bila kulipwa na mishahara yao ni tofauti na majeshi mengine. Ameiomba serikali kuwazama upya ili kuboresha maisha yao.

Kupanda kwa Gharama ya Vifaa vya Ujenzi
Mbunge wa viti Maalum, Mhe. Salome Makamba ameshangaa mapendekezo ya Serikali ya kuongeza kodi kwenye vifaa vya ujenzi na Simenti.

makamba.jpg

Salome Makamba, Mbunge wa viti Maalum
Amesema suala hili kitapunguza kasi ya wananchi kujipatia makazi mazuri na inawaumiza watanzania.

Ni muhimu kwa Serikali kutafuta vyanzo vingine vya mapato ili wananchi wawe na uwezo wa kujenga na kuboresha makazi yao.

Unyanyasaji wa Kijinsia, Serikali ichukue hatua
Suala la ukeketaji na ndoa za utotoni limeibuka tena Bungeni ambapo Mbunge Dr. Thea Medard Ntara ameshangaa kwa nini Serikali imeshindwa kukomesha kabisa vitendo hivi na wakati mwingine inawaacha wahusika waendelee kutekeleza unyanyasaji huu.

Amehoji, kama Serikali ilikomesha masuala ya mauaji ya Albino inashindwa vipi kukomesha ukeketaji na ndoa za mabinti wadogo? Dr. Thea ameenda mbali zaidi kwa kubainisha kuwa pengine masuala haya hayapati nguvu kubwa ya serikali kwa kuwa yanahusu sana wanawake na sio wanaume.

Amemuomba Waziri wa fedha kutenga fedha kwa ajili ya ulinzi wa watoto ambao bado upo nyuma ili dawa kwa wanaume walawiti na wabakaji ipatikane, ikiwezekana kuwahasi.

Amehoji, "Mtoto wa miaka 12 anaolewa anakwenda kufanya nini huko? Mbona hakuna uchungu na mabinti... Wangekuwa wanakeketwa wanaume ukeketaji ungeisha..."
 
Hili Bunge lililopora chaguzi ni Bunge la mchongo🐒🐒🐒




 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 53 leo Juni 22, 2023


Hivi umesikia majibu ya mawziri kwa wabunge. Majibu mengine yanasikitisha sana, sijui kwanini Spika wa Bunge hakemei hilo?
Mbunge anauliza swali hili waziri anajibu mbali kabisa; mfano barabara fulani sehemu; majibu mbali kabisa; lakini kwa wengine wanataja muda na wakati
 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 53 leo Juni 22, 2023



Mbunge wa Ukonga Mhe. Jerry Slaa amesema Serikali ipokee mawazo mazuri ya wananchi lakini isikubali kuyumbishwa na watu wasioitakia mema nchi yetu.

"Niiombe Serikali ikubali ushauri, isikilize wananchi lakini wakati mwingine isikubali kuyumbishwa na watu wenye nia zao za kuitaka nchi yetu isiendelee kiuchumi, ikubaliane na hoja za msingi za kuendeleza taifa letu, tuwe na uwekezaji na kushirikisha sekta Binafsi kwenye yale maeneo ambayo wenzetu wamebobea, tupate uwekezaji mzuri wa Bandari" amesema Jerry Slaa.

View attachment 2665184
Jerry Slaa, Mbunge wa Ukonga (CCM)
Mhe. Slaa ametamka maneno haya wakati akisisitiza umuhimu wa Serikali kushirikiana na Sekta binafsi katika kukuza maendeleo ya taifa huku akitolea mfano wa Hayati Benjamin Mkapa alivyokumbana na upinzani mkubwa wakati wa ubinafsishaji wa benki ya NMB, benki ambayo kwa sasa inajiendesha kwa faida kubwa.

Pia, amesisitiza hadi sasa Serikali haijasaini mikataba ya Utekelezaji uwekezaji wa Bandari Nchini, bali imeingia makubaliano ya awali (IGA), na mikataba ya utekelezaji itasainiwa baadae.

Haka kamjamaa hakajui kuwa tulitaka uhuru ili tuijenge nchi yetu sisi wenyewe, namshauri atafute wawekezaji wa kuiendesha familia yake.
 
tushindwe kuendelea na mikataba lukuki tuliyoingia kuanzia kwenye madini, gas nk tuje kuendelea kwa kubinafsisha bandari?
 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 53 leo Juni 22, 2023



Mbunge wa Ukonga Mhe. Jerry Slaa amesema Serikali ipokee mawazo mazuri ya wananchi lakini isikubali kuyumbishwa na watu wasioitakia mema nchi yetu.

"Niiombe Serikali ikubali ushauri, isikilize wananchi lakini wakati mwingine isikubali kuyumbishwa na watu wenye nia zao za kuitaka nchi yetu isiendelee kiuchumi, ikubaliane na hoja za msingi za kuendeleza taifa letu, tuwe na uwekezaji na kushirikisha sekta Binafsi kwenye yale maeneo ambayo wenzetu wamebobea, tupate uwekezaji mzuri wa Bandari" amesema Jerry Slaa.

View attachment 2665184
Jerry Slaa, Mbunge wa Ukonga (CCM)
Mhe. Slaa ametamka maneno haya wakati akisisitiza umuhimu wa Serikali kushirikiana na Sekta binafsi katika kukuza maendeleo ya taifa huku akitolea mfano wa Hayati Benjamin Mkapa alivyokumbana na upinzani mkubwa wakati wa ubinafsishaji wa benki ya NMB, benki ambayo kwa sasa inajiendesha kwa faida kubwa.

Pia, amesisitiza hadi sasa Serikali haijasaini mikataba ya Utekelezaji uwekezaji wa Bandari Nchini, bali imeingia makubaliano ya awali (IGA), na mikataba ya utekelezaji itasainiwa baadae.

Naunga mkono hoja,Wala Rushwa bandarini,wavisha mizigo Bure na wanaonufaika na ukiritimba ndio wamekuwa mstari wa mbele kupinga maendelea..

Washughulikiwe
 
Kumbe huyu dogo sometimes ana akili....
Nilijua na yeye ataenda Kwa Karamagi kupokea fungu lake aanze kubwabwaja kama Tibaijuka
 
Kwenye madini tulibinafisisha, hatukupata maendeleo

Gas nako vile vile

Mbuga za wanyama huko lolyondo nako hakuna

Tumebinafisisha mabenk napo hakuna

Ndo tuje kuwa dona kantiri kwenye Bandari?

Jamaa wanaumwa ama?
 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 53 leo Juni 22, 2023



Mbunge wa Ukonga Mhe. Jerry Slaa amesema Serikali ipokee mawazo mazuri ya wananchi lakini isikubali kuyumbishwa na watu wasioitakia mema nchi yetu.

"Niiombe Serikali ikubali ushauri, isikilize wananchi lakini wakati mwingine isikubali kuyumbishwa na watu wenye nia zao za kuitaka nchi yetu isiendelee kiuchumi, ikubaliane na hoja za msingi za kuendeleza taifa letu, tuwe na uwekezaji na kushirikisha sekta Binafsi kwenye yale maeneo ambayo wenzetu wamebobea, tupate uwekezaji mzuri wa Bandari" amesema Jerry Slaa.

View attachment 2665184
Jerry Slaa, Mbunge wa Ukonga (CCM)
Mhe. Slaa ametamka maneno haya wakati akisisitiza umuhimu wa Serikali kushirikiana na Sekta binafsi katika kukuza maendeleo ya taifa huku akitolea mfano wa Hayati Benjamin Mkapa alivyokumbana na upinzani mkubwa wakati wa ubinafsishaji wa benki ya NMB, benki ambayo kwa sasa inajiendesha kwa faida kubwa.

Pia, amesisitiza hadi sasa Serikali haijasaini mikataba ya Utekelezaji uwekezaji wa Bandari Nchini, bali imeingia makubaliano ya awali (IGA), na mikataba ya utekelezaji itasainiwa baadae.

wananchi nawawomba tuyapuuze madalali na makuwadi ya warabu yaliyohongwa.
 
Back
Top Bottom