Dr. Slaa akimbia Mdahalo wa Kesho

Dr. Slaa akimbia Mdahalo wa Kesho

Nikuulize Dr Slaa ni aspirant wa Urais? Kwa sababu mdahalo unaitwa 2nd Presidential Aspirants debate.
Dr.slaa bado hajatoa sababu za msingi za kutoshiriki.mdahalo kuitwa 2nd presidential aspirant siyo sababu ya kutoshiriki.hata waandaaji wa debate wanajuwa bado chadema hawajatangaza mgombea.lakini si lazima watatangaza? Dr.slaa angekuwepo kuelezea mambo mengi tu yanayohusu urais kwa mwaka huu si lazima kwamba yeye binafsi ndie awe mgombea yeye ni Katibu mkuu ana mengi ya kuwaambia wananchi.
 

mkuu, mtu kama Mufuruki ambaye ndiye kinara wa CEOs wote hapa Tanzania kukosa umakini kwa jinsi hii ni aibu.

uhovyohovyo wa kiutendaji kwenye serikali hii ya CCM unachangiwa pia kwa kiasi kikubwa na kukosekana kwa changamoto za msukumo kutoka kwenye private sector ambayo CEOs wake ndio hawa wakurupukaji!
Wewe ndo hujielewi kabisa.Mufuruki ndio atakuwa anawashangaa watanzania na hao wagombea wenu wanaokimbia mijadala. Bado miezi mitatu tupate rais bado watu hamtaki kuwasikia wanaoutaka urais wana uwezo gani? Linchi lina watu wa ajabu sana hili.
 
Dr.slaa bado hajatoa sababu za msingi za kutoshiriki.mdahalo kuitwa 2nd presidential aspirant siyo sababu ya kutoshiriki.hata waandaaji wa debate wanajuwa bado chadema hawajatangaza mgombea.lakini si lazima watatangaza? Dr.slaa angekuwepo kuelezea mambo mengi tu yanayohusu urais kwa mwaka huu si lazima kwamba yeye binafsi ndie awe mgombea yeye ni Katibu mkuu ana mengi ya kuwaambia wananchi.

Hujajibu swali......Mdahalo ni kuwapima watia nia wa Urais? kuna haja gani ya kuharakisha wakati Vyama havijamaliza internal process zake?

Unajua tofauti ya Mdahalo na Kongamano?

Dr slaa ataongeleaje mambo yanayohusu Urais wakati yeye hagombei? Na kama angeongea kwa niaba ya chama ,atayatoaje mambo yake binafsi wakati ilani ya chama ambayo ndiyo leading document bado haijapitishwa na vikao vya chama?

Na kama ilikuwa ni kuwakilisha CHADEMA kwa nini waandaaji wa mdahalo wasingekialika CHAMA na badala yake Dr slaa...Point is Chama kingemtuma hata Mnyika.

Na je kwa nini NCCR hawajaalikwa wakati kuna mtia nia George Kahangwa?

Mkuu.....CHADEMA wako systematic...hawana mvurugano kama CCM
 

mkuu, mtu kama Mufuruki ambaye ndiye kinara wa CEOs wote hapa Tanzania kukosa umakini kwa jinsi hii ni aibu.

uhovyohovyo wa kiutendaji kwenye serikali hii ya CCM unachangiwa pia kwa kiasi kikubwa na kukosekana kwa changamoto za msukumo kutoka kwenye private sector ambayo CEOs wake ndio hawa wakurupukaji!

Nadhani anataka kujenga CV yake...kwa hio anakurupuka ili kuwa wa kwanza ku organize midahalo

Anatakiwa awe patient vyama vimalize internal Processes

Hili suala ITV watalifanyia kazi wakati mwafaka...na hawakurupuki...Rose Mwakitwanga
 
Nani aliyetangaza hilo?

Kudumu kivipi?

Dr Amegombea mara moja tu.

Na CHADEMA haijatangaza mgombea wake?

We haya maneno umeyatoa wapi?

Umekula maharage ya wapi Mohddd?
Mimi uwa naongea na data siyo porojo za kwenye mbegu. Soma hapa chini.

Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu kwamba Katibu mkuu wa chama hicho kikuu cha upinzani, Dk Willibrod Slaa ndiye atakayekuwa mgombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).Akiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Chadema mjini Moshi, hivi karibuni, Lissu alikaririwa akieleza kuwa Dk Slaa, ndiye atakayepitishwa na Ukawa kugombea nafasi hiyo.Lakini Mkuu wa Idara ya Kampeni na Uchaguzi wa NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura aliliambia gazeti hili mwishoni mwa juma kuwa ni makosa kudhani kwamba Chadema ndicho chenye nafasi ya kusimamisha mgombea urais kupitia Ukawa, wakati bado mchakato wa kumpata mgombea haujafanyika.


Sasa wewe Chadema-Kata na Tundu Lissu tumuamini nani?
 
Mimi uwa naongea na data siyo porojo za kwenye mbegu. Soma hapa chini.

Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu kwamba Katibu mkuu wa chama hicho kikuu cha upinzani, Dk Willibrod Slaa ndiye atakayekuwa mgombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).Akiwa kwenye mkutano wa hadhara wa Chadema mjini Moshi, hivi karibuni, Lissu alikaririwa akieleza kuwa Dk Slaa, ndiye atakayepitishwa na Ukawa kugombea nafasi hiyo.Lakini Mkuu wa Idara ya Kampeni na Uchaguzi wa NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura aliliambia gazeti hili mwishoni mwa juma kuwa ni makosa kudhani kwamba Chadema ndicho chenye nafasi ya kusimamisha mgombea urais kupitia Ukawa, wakati bado mchakato wa kumpata mgombea haujafanyika.


Sasa wewe Chadema-Kata na Tundu Lissu tumuamini nani?

Hhaahahhaahah.....mkuu kweli unapotea...CHADEMA kata tena? Anyway sio topic at hand.

Mkuu hayo ni maoni ya Lissu...kama ilivyo hata wewe mkuu moh kwamba kuna watu wanaona unafaa kuwa Rais....Lakini wewe hujatangaza kuwa una nia ya Kuutaka Urais.

Mkuu....nadhani una uelewa mpana.

Unaposema mtu ana nia....ni mtu mwenyewe muhusika ameonesha nia .....Dr Slaa ameonesha nia?

Kama unaongelea maoni...kuwa Dr Slaa ndiye anayefaa...wamesema wengi tu...Kina Kafulila...kina Mbowe na wengine....

Muhusika ana nia hiyo?

Kama tukienda kwa mtindo huo unaoutaka basi na wewe uende kwenye mdahalo mkuu......

Maharage ya wapi unakula ndugu yangu? ila nakupongeza kwa kuleta maoni ya Lissu kuwa Dr anafaa
 
mdahalo utakaorushwa kesho kuanzia saa 1 hadi saa 4 na azam tv unaoandaliwa na ceort chini ya kiongozi wao ally mufuruki, dr slaa amesema wao hawatashiriki mijadala mpaka watakapomaliza kura za maoni ndani ya chama.



Washiriki ni prof lipumba cuf, zitto kabwe act, dr. Slaa chadema na dr. Emanuel makaidi nld.



dr slaa anawapa wakati mgumu magamba na washirika wake. Tamko lilitolewa na chadema liko sahihi na limejitosheleza. Dr slaa atashiriki vipi mdahalo wa wagombea wa urais wakati bado hajapitishwa wala kutangaza nia ya kugombea? Dr slaa hatafuti sifa za kijinga kama mtu mwingine ambae sio mgombea na wala hajatangaza nia kugombea urais. Dr slaa ni kiongozi makini na hafanyi vitu kupata sifa za hovyohovyo. Amefanya maamuzi sahihi. Tusubiri apitishwe na chadema ndio mtaona moto wake
 
Well said Denyo na Freeland. Ritz naomba nikufahamishe kuwa Chadema hawajamuidhisha (Endorsement) Dr Slaa kugombea uraisi vile vile Mufuruki aandae mdahalo wa Ukawa kama Ukawa kama alivyoandaa wa wanaCCM peke yako kisha vyama vyote vilivyobaki ACT; DP: UDP nk wa kwao. Mufuruki ana hila au anatumiwa na CCM. Tuwasubiri akina Rose Mwakitwange na Hamza Kassongo na Jenerali Ulimwengu waitishe wa wagombea uraisi vyama vyote
 
Baada ya Dr. Slaa kutokuhudhuria Mdahalo hapo kempisti leo je, Mdahalo nao umesitishwa ,au Hao waalikwa wengine wameudhuria? Na kama umesitishwa nini maana yake? Au mdahalo hauwezi fanyika mpaka Dr. Slaa awepo?

Naomba munisidie majibu ........
 
Jamani munaofuatilia haya mambo tupeni majibu, Mdahalo umefanyika leo hapo kempisti?
 
Inawezekana mdaharo ukawa umesitishwa,bcoz mdaharo ungependeza tu iwapo Dr. Slaa chague la wengi angekuwepo
 
Kwanini huyu jamaa anarusha kwenye Tv ambayo wengi hawana access nayo au ndio yale yale hawezi kurusha kwenye TV za makafiri!?
 
Ndugu zangu watanzania,
Nikupongezeni kwa kutumia vizuri uhuru wa kutoa maoni na kujadiliana. Tafadhali naomba nikutaarifuni kwamba, ingawa lengo la awali la CEOrt lilikuwa kufanya mdahalo wa wagombea urais, kilichopangwa kufanyika leo si mdahalo huo bali ni mjadala unaowakutanisha viongozi wakuu wa vyama, kwa ajili ya kudokeza sera za vyama vyao.

Nimekuwa na mawasiliano na wahusika katika CEOrt, nikihoji kwanini watia-nia hatukualikwa. Wamenihakikishia kwamba walichopanga leo si cha watia-nia, bali ni hicho mtakachokiona leo.
Nakutakieni ufatiliaji mwema na makini wa kinachojiri sasa hata tutakapofika siku ya kupiga kura.
Shime kila mmoja wetu, mwenye umri stahiki, ahakikishe anajiandikisha katika daftari la kudumu la wapigakura.
 
Chama cha chadema Leo kimejitoa kwenye mdahalo unaoshirikisha vyama vya upinzani ambapo Muda huu tayari baadhi ya wapinzani washaingia ukumbini akiwemo ZITO ,LIPUMBA ....
Akiongea na BBC muandaaji wa mdahalo amesema bwana katibu wa chama cha CDm Silaa amesema Sera za chama zinamzuia kushiriki katika mdahalo ingawa mwanzo alishiriki katika kupanga tare he ya mdahalo na tarehe ya Leo ilipangwa ili naye aweze kushiriki
 
hawa wapinzani kuna siku watakujadundana wenyewe kwa wenyewe,,
 
Slaa apumzike alee familia sasa umri umeshamtupa!
 
Back
Top Bottom