Hivi nyinyi mnafikiri Magufuri ni mtu ona tu chama chake kushindwa kukiongoza anasaidiwa na maafisa vipenyo tu , Chama chake chenyewe hawamtski Ila hawawezi kuonyesha hadharani pamoja na kuwa wanasimamia na kupiga kampeni wanaogopa tu asiwakolimbe .
Sasa wewe hueeweki. Shida yako ni nini hasa?
Unataka kiongozi mkuu asisaidiwe na mifumo ya taasisi? Unatafuta uongozi upi wewe?
Unasema ccm hawamtaki Magufuli. Kwa mantiki yako na uelewa wako juu ya ccm. Ni kwa nini hawamtaki Magufuli?
Unapoona kwamba ccm imegawanyika vipande viwili kwa maana ya Magufuli na wanaccm. Wewe inaonekana unaona ccm ndio wako sahihi kuliko Magufuli. Unapoungana na ccm ambayo tayari ilishapitisha ufisadi, rushwa, wizi, kutokuwajibika, ulaghai, madawa na kila aina ya uovu kuwa sera zake, ukamkataa Magufuli ambaye anajitahidi kutekeleza sera za UPINZANI katika kurekebisha hali japo kwa sehemu, wewe unaonekana huna uchungu na taifa hili.
Tukuweke wapi?
Naomba uache hila, na uwe mkweli ili ueleweke wewe uko upande wa Tanzania ama upande wa ccm fisadi.