Dr Peter Dalaly Kafumu apata ajali

Dr Peter Dalaly Kafumu apata ajali

Kati ya majimbo ambayo wananchi wake wanatakiwa kujutia mzaha mbaya walioufanya, katika sanduku la kura, mwaka 2010, ni Iramba Magharibi,Singida.
Naelewa utetezi wa yule jamaa wa Mtera waweza kuwa hakubahatika kupata elimu rasmi kuweza kustaarabika katika kauli na matendo.
Sasa huyu wa Iramba Magharibi ana kisingizio gani?
Huyu ndugu angeishia Elimu ya Darasa la Saba tu hali ingekuwaje huko kwao Makanda?
Nadhani angejikita katika uuzaji wa ugoro,mtukuru,mataputapu,wizi,uuzaji wa bangi.Hapo sijagusia masuala ya kukamatwa ugoni mara kwa mara.
 
Aliyekuwa mbunge wa Igunga kwa tiketi ya CCM, Dr. Dalali Peter Kafumu alipata ajali huko kwao Igunga akiwa na gari yake aina ya Toyota Prado. Gari hiyo ilikuwa ikiendeshwa na mtoto wake na walikuwa wakielekea kwenye mazinshi ya mama wa ubatizo. Alipata majeraha madogo kichwani na alitibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani. Mtoto wake hakupata majeraha yaliyohitaji kwenda hosipitali. Chanzo cha ajali ni gari kuhama njia na kupinduka. Hali zao ni nzuri kwa sasa.Source: ITV, habari za saa.
 
Aliyekuwa mbunge wa Igunga kwa tiketi ya CCM, Dr. Dalali Peter Kafumu alipata ajali huko kwao Igunga akiwa na gari yake aina ya Toyota Prado. Gari hiyo ilikuwa ikiendeshwa na mtoto wake na walikuwa wakielekea kwenye mazinshi ya mama wa ubatizo. Alipata majeraha madogo kichwani na alitibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani. Mtoto wake hakupata majeraha yaliyohitaji kwenda hosipitali. Chanzo cha ajali ni gari kuhama njia na kupinduka. Hali zao ni nzuri kwa sasa.Source: ITV, habari za saa.
saa ngapi?? tulia uandike kwa makini, unakimbilia wapi??
 
saa ngapi?? tulia uandike kwa makini, unakimbilia wapi??

wewe ndiye unatakiwa utulie wakati unaposoma hii thread. Kama hujui si vibaya kuuliza.
Kuna kasegment ka habari itv kanaitwa habari za saa......
 
daaah nchemba naona sasa ameanza rasmi kuvaa viatu vya sheikh yahya,prof MAJI MAFUPI
 
Nahisi hii ajali ni feki iliyo pangwa na mwigulu ili kutafuta umaruufu na kuwachafua wapinzani wake
 
Habari za uhakika na zimethibitishwa na Mwigulu Nchemba mbele ya mkutano wa hadhara Nkinga leo jioni.

Kuwa Dr Dalaly Kafumu amepata ajali mbaya maeneo ya kijiji cha Mwisi, amelazwa hapa Nkinga hospital ameumia kichwani.

Nchemba amehusisha ajali hiyo na imani za kishirikina kuwa ni uchawi wa Cdm uliosababisha ajali hiyo.

-------

Watu kama Nchemba ndio tegemeo kubwa la CCM !!! Kazi kweli kweli ...
 
Kweli CCM wamekwisha!

Yaani kila upuuzi unaotokea ni CDM kweli? Kafumu apate ajali ni CDM,mtu auawe na Polisi kwa bomu la machozi ni CDM,ajali za meli baharini ni CDM, magamba wakichukua pesa za Kifisadi ni CDM,Serikali imeshindwa kuleta Maisha bora kwa kila Mtanzania wanalaumiwa CDM!

Kweli wahenga walisema mfa maji haachi kutapatapa hata akiona unyasi ataudaka ili kujaribu kujiokoa. But it's too late to survive! CCM yaangalieni wenyewe. Nchi imewashinda msianze kutafuta mchawi. Wachawi ni ninyi wenyewe!!!!!!!
 
Habari za uhakika na zimethibitishwa na Mwigulu Nchemba mbele ya mkutano wa hadhara Nkinga leo jioni.

Kuwa Dr Dalaly Kafumu amepata ajali mbaya maeneo ya kijiji cha Mwisi, amelazwa hapa Nkinga hospital ameumia kichwani.

Nchemba amehusisha ajali hiyo na imani za kishirikina kuwa ni uchawi wa Cdm uliosababisha ajali hiyo.

-------
Kutoka kwa Kigwangalla:

Dr. Dalaly Kafumu amepata ajali ya kupinduka na gari akielekea kwenye kijiji kimoja kilichopo kata ya Mwisi ambako alikuwa anaelekea kushiriki mazishi ya Mama mmoja maarufu. Ajali hiyo ilitokea jana ambapo gari ilipoteza uelekeo kutokana na hitilafu ya barabara na hivyo kuvutwa, kugonga gema na kupinduka mara moja na gari kukaa matairi juu.

Gari iko nyang'anyang'a huwezi amini kama kuna mtu ametoka salama, lakini tunavyoongea hapa Dr. Kafumu na kijana wake ambaye alikuwa akiendesha walitoka salama. Dk. Alibanwa na Airbags na walilazimika ili kumtoa kuvunja mavyuma kwa shooka na kumkuta amezimia na alizinduka baada ya muda kidogo, pia alikuwa na bruises zilizokuwa zinavuja damu sana kichwani na alilazwa hospitali ya Nkinga na asbh hii atapewa ruhusa arudi nyumbani.

Amekuwa jimboni humo toka Jumatatu akifanya ziara ya kukamilisha miradi ya maendeleo aliyoianzisha, pia kuwaondoa mashaka wananchi kuwa hatowatelekeza kwa kuwa ametolewa Ubunge, na kwamba bado yuko nao pamoja tu.



Hapo kwenye bold ni kweli mkuu au unanogesha story tu ili ipate wachangiaji wengi?
 
PoLE DR KAFUMU ni ajali kama ajali zingine sidhani kama kuna kuhusishwa na uchawi hapa
kama kweli Mwinguluuuu kasema hivo ana matatizo kichwani mwake
Mungu akuponye uendelee kutekeleza ahadi zako kwa wananchi na ushuhudie mbunge halali akiapishwa
 
Hii Inaonyesha Ishara ya Hii Nchi inayofanya Kila Kitu Kwa Majaribio!! Mimi Ninavyolinganisha Umri wa Kafumu Mimi Naona Umri wa Huyo Mtoto wake Haukuwa na weledi wowote wa Kuweza kuendesha na Kumudu Barabara!! Hivyo ni Bora basi Ikajulikana ajali hii imesababishwa na Uendeshaji Usiozingatia weledi!!
 
Back
Top Bottom