Inasikitisha JF imekuwa sehemu ya wapiga majungu, kilichotokea Ipinda ni tofauti kabisa na alichoandika huyu jamaa, pengine kafanya makusudi kufurahisha waajiri wake ili mwisho wa siku ajipatie posho.
Mkutano wa Ipinda uliweka record na kamanda Makongoro alikuwepo pia. Inasikitisha sana kuona Kyela imeendekeza majungu na ndiyo wilaya inaongoza kwa kuwa na wakurugenzi wengi wanaokaimu kitu kinachoirudisha nyuma sana kimaendeleo. Na hata hao wanaojifanya kuipenda Kyela wameshindwa hata kubadilisha makazi ya wazazi wao wamebaki na nyumba za nyasi kama siyo majani ya migomba. Wanakyela majungu hayajengi badala yake unganisheni nguvu kuibadili wilaya yenu, mbona Rungwe wameweza.
Mtu anasema Mwakyembe hajafanya kitu! Ajabu kwelikweli, lakini ni mbunge aliyeweza kuishawishi serikali kuwajengea barabara inayounganisha tarafa kwa kiwango cha lami (Njia panda ya Ipinda kwenda Matema) wakati kuna mikoa haijaunganishwa kwa barabara za lami. Vilevile ni mbunge huyohuyo ameweza ishawishi serikali kujenga daraja la mabilioni kwenye track (sijui hata kama mnajua maana yake) wakati kuna trunk road kibao zinakosa madaraja. Mbunge huyo huyo alipata wakati mgumu sana bungeni kutoka kwa marehemu Komba kuelezea sababu zilizofanya kujenga chelezo Kyela badala ya Mbambay lakini kwa sababu wanakyela wanajua kupiga majungu tu hawajui hata umuhimu wake! Lakini pia sasa hivi umeme unasambazwa vijijini ila kwa vile wanasema umeme si rafiki ya wachawi yawezekana ndiyo maana hili nalo hawalioni. Miradi yote hiyo ni level za kitaifa na inahitaji mbunge strong kuweza kujenga hoja na kuipata, sasa mnataka mfanyiwe nini hasa? Ninyi endelei tu kakaa juwa kali mkisubiria mabadiliko wakati wenzenu wanaendelea kuchapa kazi. Halmashauri inashindwa kujenga hata km moja ya lami kwa mwaka, matokeo yake wameishia kupiga majungu tu! UKAWA msijidanganye hamuwezi kumshinda Mwakyembe Kyela.