Dr. Magufuli amechafuka, hachaguliki

Dr. Magufuli amechafuka, hachaguliki

Umesoma na kuelewa Mkuu? Acha kuropoka kabla ya kuelewa.

Mzee Tupatupa

Sasa ni nani hajavunja utaratibu? Kingunge ambaye alianza kampeni kwa mgombea aliyemtaka kabla ya wakati au kamati ya nidhamu iliyokuwa imevurugwa na mwenendo wa mzee wa busara kingunge? Mimi siyoshabiki wa chama chochote ila nimsomaji wa alama za nyakati na muumini mzuri wa nidhamu. Kwa kuwa yaliyotokea kwenye chama cha kingunge ni yao basi angeyasema kwenye chama na siyo kwenye vuombo vya habari. Hivi aliyekuwa chaguo lake kingunge angepita kwa mizengwe ya aina yoyote angelalamika? Badala ya kuanza kulaumiana na kulalamika tusubiri vyama vingine vilete wagombea watanzania wapime nani zaidi kiutendaji na siyo kimchakato.
 
Vuta Nikuvute-Mzee wa Ifipa muda huu jielekezeni kuinusuru ndoa yenu ya UKAWA ili walau mlete msisimko wa kumsindikiza Magufuli kwenye kukamilisha ratiba ya uchaguzi.

Hayo ya kuhangaika na Magufuli ni mazito kwenu,hamyawezi.Jielekezeni kuokoa ndoa yenu inayopumulia mashine.
 
sawa mzee Tupatupa kwa mantiki hiyo unawashauri nini wanaCCM? Au wachague Ukawa mchezo uishe?
 
Ndiyo matatizo yenu hayo huwa hampendi kuambiwa ukweli. Hata Baba wa Taifa aliposema CCM si mama yangu vikaragosi vya mafisadi kama wewe na wenzio mngemuita, Baba wa Taifa la Ufipa Dar es Salaam.

Mzee Tupa Tupa wa Ufipa Dar es Salaam.
 
Ama Kweli mchakato batili huzaa batili na mtu mchafu, huenda naye akawa hasafishiki hata kwa dodoki!
 
VUTA-NKUVUTE

Da!
Ubaguzi,ukabila,uchochezi,uzushi na uroho wa madaraka. muda wake umeisha.
Na mkiyaendeleza hayo NAWATOA KATIKA WANAOILITAKIA MEMA TAIFA.Hongereni kwa jitihada zenu..
Lakini nawashangaa sana viongozi wao wa chama.
Miaka yote minne walikuwa wanapiga majungu.sawa ndio kazi yao kama wapinzani kuikosoa serikali.

Lakin pia nawashangaa watu ambao muda wa kuuza na kunadi sera zao kuwa watawafanyia nini wananchi..
Wao bado wanakalia tu fulani hivi fulani vile...

Muda wa majungu umeisha sasa tunataka sera.Maana watu mitaani wamelewa.wakienda kwenye mikutano wanashangilia tu.ukiangalia wanashangilia nini? "Kasema fulani fisadi"
Sasa hilo ni jambo la kushangilia au lakusikitika?
Muda wa kuuza Sera huu..
Majungu si mtaji bai zhe wei
LABDA KAMA MAJUNGU NDIO SERA YA CHAMA TUAMBIANE KABISAA!!!!
 
Last edited by a moderator:
Nikuulize swali, Nyerere mnayemsifia kila siku aliongoza kupitia chama gani?
aliishia kusema Bila CCM Madhubuti Nchi itayumba,hatimaye tingatinga linaingia kurekebisha paliposinyaa.

Endelea kumzoea Magufuli kama Rais wako wa awamu ya tano,hauna namna nyingine.


Nyerere huyo huyo pia alisema CCM sio mama yangu. Na tena akasema Watanzania wanataka mabadiliko, wasipoyapata wasipoyaona ndani ya CCM, watayatafuta nje ya CCM. CCM aliyosema Nyerere ni ile CCM madhubuti sio hii ya leo ambayo imejaa wezi, wahuni, matapeli na walaghai kama nyinyi
 
Mkuu,
Ni wapi sijaelewa, nieleweshe!
Nimekuuliza kama wewe unadhani Magafuli hachaguliki, nani anachagulika?
Mkuu Achana naye VUTA-NKUVUTE na BAVICHA wamechanganyikiwa
Mizinga ya Maguu-full hakuna wa kuizuia
UKAWA wote wamepoteana
Mgombea wao mtarajiwa sasa ni Lowassa
tusubirie matamko yake huko Monduli
Kapokelewa kwa shangwe na CHADEMA Patamu hapo?
attachment.php
 
huyu mzee anashawishika na vijisenti alivyopewa ili kuchafua wasafi na kusafisha wachafu.
kamwe ukweli utabaki kuwa ukweli.

magufuli anakubalika sannaaaaa....

#tukutane_oktoba
Huyo sio mzee ni Bavicha wanajaribu kumtetea Lowasa maana walikuwa wana mshawishi aende kwao ili wapambane na CCM ...Teh Teh
 
Huyo sio mzee ni Bavicha wanajaribu kumtetea Lowasa maana walikuwa wana mshawishi aende kwao ili wapambane na CCM ...Teh Teh


BAVICHA hawamtetei Lowassa. Nyinyi wahuni, matapeli na walaghai wa CCM ndio mnaoeneza propaganda ili kudanganya Watanzania. Acheni kutapeli Wananchi
 
kubali kilichopangwa na ccm huwez linganisha na ukawa ambao hadi leo hawana mgombea urais
 
Huyo ni mmoja wa Bavicha walio changanyikiwa..amesahau kuwa hata UKAWA hadi sasa hawana mgombea kutokana na mziki wa Magufuli..

Bavicha siku hizi wanapatikana Lumumba. Mbona bado mapema huyu mwizi wenu hajaanza kuchambwa hhadhdarani? Na wewe jikongoje hadi baada ya October kama bk 7 zitaendelea
 
vuta nikuvute-mzee wa ifipa muda huu jielekezeni kuinusuru ndoa yenu ya ukawa ili walau mlete msisimko wa kumsindikiza magufuli kwenye kukamilisha ratiba ya uchaguzi.

Hayo ya kuhangaika na magufuli ni mazito kwenu,hamyawezi.jielekezeni kuokoa ndoa yenu inayopumulia mashine.
ifipa ndiyo wapi mkuu au umetumwa?
 
Back
Top Bottom