apolycaripto
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 644
- 225
Katika kipindi cha mahojiano mnamo tarehe 24/03/2011,Dr Hans Kitine mbali na mambo mengine alidiriki kuangazia ndani ya serikali hii kwa sasa na kusema moja kati vitu vinavyochangia ukosefu wa maadili ni pamoja na kuwapa watu vyeo bila kuwafanyia vetting kupitia vyombo vya usalama. Alidai kuna Katibu Mkuu mmoja ni mchafu kwa maana ya fisadi na watu wanamlalamikia japo hakumtaja jina lakini bado amepewa Wizara tena nyeti zenye fedha nyingi na anaendelea kufisadi kama kawaida.
Tutambue maneno haya ya Dr. Kitine si ya kupuuzwa kwani ni Mzee na Bosi Mstaafu wa Usalama wa Taifa. Nimefanya uchunguzi kupitia kwa baadhi ya watu waliotizama na kumsikia katika mahojiano yale, wengi wamedai Katibu Mkuu anayezungumziwa ni Eng.Omary Chambo. Sina uthibitisho kwa maana ya ushahidi lakini ndiye anayetajwa.
Nashauri suala la kujivua gamba kama inavyosemekana,kuelekee pia kwa hawa Makatibu Wakuu (ambao ndio technical figure na watendaji wakubwa ndani ya Serikali). Haiwezekani Mawaziri wao wachafuke kisha wao wakabaki salama hata kidogo. Kuyumba kwa Serikali kunachangiwa na hawa kwa kiasi kikubwa na si kuishia kwa Wanasiasa pekee. Kikwete hawa watu wanakutafuna hawa!
Tutambue maneno haya ya Dr. Kitine si ya kupuuzwa kwani ni Mzee na Bosi Mstaafu wa Usalama wa Taifa. Nimefanya uchunguzi kupitia kwa baadhi ya watu waliotizama na kumsikia katika mahojiano yale, wengi wamedai Katibu Mkuu anayezungumziwa ni Eng.Omary Chambo. Sina uthibitisho kwa maana ya ushahidi lakini ndiye anayetajwa.
Nashauri suala la kujivua gamba kama inavyosemekana,kuelekee pia kwa hawa Makatibu Wakuu (ambao ndio technical figure na watendaji wakubwa ndani ya Serikali). Haiwezekani Mawaziri wao wachafuke kisha wao wakabaki salama hata kidogo. Kuyumba kwa Serikali kunachangiwa na hawa kwa kiasi kikubwa na si kuishia kwa Wanasiasa pekee. Kikwete hawa watu wanakutafuna hawa!