Dr Kitila Mkumbo aing'arisha CHADEMA vyuo vikuu

Dr Kitila Mkumbo aing'arisha CHADEMA vyuo vikuu

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Dk Kitila Mkumbo, jana alikabidhi kadi kwa wanachama wapya 56 kutoka Chuo cha Mtakatifu John, akiwamo Mhadhiri wa chuo hicho, Martine Tetti.

Dk Mkumbo alisema unahitajika ujasiri katika kutekeleza dhana ya mabadiliko nchini, kwa kuwa CCM imekuwa ikitumia mbinu mbalimbali za kutaka wasomi wasihusike kwenye siasa ili kuendeleza siasa chafu za ufisadi na rushwa.

Source:Mwananchi Jumatano
Sioni cha ajabu hapo...mle mle!
 
Kwa elimu yake anajiamini siyo wasomi uchwara.
 
Huyu Dr nimezoea kumsikia tu hapa JF, but uraiani hajulikani kabisa!! kwanza hana mvuto wa kisiasa, aendelee tu kushika chaki

Kujibizana na wewe ni kujitafutia BAN tu.Wewe ni wa kupuuza tu ....
 
Sioni cha ajabu hapo...mle mle!

Hizo ni dalili za kufirisika sera kichwani mkuu,kumbuka st john sio kua wanasoma ni wakristu tu!dunia ya leo ukiona mtu anajenga hoja za udini na ukabila ujue kaishiwa hoja kichwani
 
Usijali atafika na kule Zarau Islamic University, Makorora Tanga.......tafadhali hakikisaha unakuwepo
Hizo ni dalili za kufirisika sera kichwani mkuu,kumbuka st john sio kua wanasoma ni wakristu tu!dunia ya leo ukiona mtu anajenga hoja za udini na ukabila ujue kaishiwa hoja kichwani
Nawashangaa mnavyoniquote vibaya...hamna sehemu yoyote nimehusisha mambo ya dini...nyie mnajishtukia tu!
 
Dr kitila unatuboa wana iramba magharibi. Njoo, tukupe jimbo kaka. Kama hilo hulitaki sema.
 
Historia iko wazi, Kombozi zote wakati wa kudai uhuru Afrika na haki za msingi kote duniani zilikuwa na mkono wa WASOMI vyuoni hasa vijana. Kwa kuwa tunataka UKOMBOZI wa kweli wa FIKIRA, KIUCHUMI, KISIASA, hatuna budi kujenga kizazi kilichopo shuleni ili kikuwe na mabadiliko ya kweli ktk fikra zao ktk leo na kesho yao.

ALUTA CONT..... Dr!!!!!!!! VIVA M4C!!!!!
 
Kupenda kazi....kusema kweli CDM ipo juu kama rubani hewani, kila siku CC-Mafisadi inazidi kubakiwa na vikongwe....wale wa-today wanawaona kama Chocklate za Bamia
 
Back
Top Bottom