Dr. Kitila ampa tabu Thabo Mbeki

Dr. Kitila ampa tabu Thabo Mbeki

- I have no comment kuhusu mawaswali aliyomuuliza huyo Rais mstaafu, ila nashangaa kusikia hakujibu WHY?

- I dont care kuhusu swali la Dr. Kitila even though kwa kuwa najua ni kichwa najua kwamba alilipima na yuko right kuliuliza, nina tatizo sana na swali kutkujibiwa ndio huwa ninaita nonsense! !

Utashabikia swali ambalo hata hulijui?

Kama halikuwa swali bali tusi kwa Mbeki kwa nini ajibu?

Kama ni swali ambalo haliendani na mada husika kwa nini ajibu, hususan kama limeulizwa kifedhuli?

Hapa muite huyo Kitila unaemuaminia sana atueleze swali alilouliza kwanza kabla ya kuanza kumpamba kwa jumla jumla
 
Nadhani swali lilikuwa stahili na kama kweli ni muungwana alitakiwa kutoa majibu, kuwa na kiongozi mkubwa wa aina yake halafu unatoa majibu mepesi kwenye masuala sensitive yahusuyo maisha ya watu ni makosa makubwa. Ufafanuzi wake unahitajika ili kuweka mambo sawa-lakini kwa upande mwingine viongozi hawa wa SA wananishangazi kwe misimamo yao kwenye suala hili la ukimwi; kuna huyu aliyepo sasa yeye alisema baada ya kumbaka yule mtoto wa rafiki yake kavukavu alikimbilia bafuni kuoga ili asipate ukimwi!!! Sisi maamuma tukisikia kauli kama hizi nim rahisi kuziamini na ndio inakuwa kiam chetu
 
Mimi nna shaka kuwa hajauliza hili swali kama lilivyoanishwa hapa
Dk. Kitila Mkumbo tafadhali njoo utupe swali ulilouliza tulijadili.

Ninachokiona hapa wengi wameacha hoja ya msingi
na badala yake wanamuattack Dr. Kitila, nadhani kwa
chuki au vinginevyo. Ingalau wewe umesema jambo la
msingi sana...
 
Dr Kitila,
Nakuona humu. Fafanua. Thabo Mbeki hana mtoto wake wa kuzaa.
 
From the very outset mbeki aliweka wazi that was a very pinchin question as kitila alitaka kupotray mbele ya dunia kwamba msimamo wa mbeki kua ukimwi kuenezwa kwake ni umasikini umesababisha vifo vingi sana as yeye(mbeki akiwa rais) alipuuzia scientific investigation about kuenezwa kwa ukimwi hatimae watu wakaendelea kufa. (Kitila alitaja data,sizikumbuki).

Mbeki kwa hasira(alichange fascial expresion) alimwambia kitila "the information that you have is wrong" from statement itself na takwimu alizotoa. Mbeki alielezea vizuri sana kauli yake ya umasikini na tafiti za kisayansi kuhusu ukimwi...ila hakujibu alichouliza Dr mkumbo kwa sababu it seems hakuona kama kuna swali rather aliliona lipo kisiasa ama pengine kifitna.

My take...Kuuliza sio ujinga, na kukosea sio tusi. Sikufahamu dhamira ya kitila ila iwe ilikua ni nzuri ama mbaya watu wengi pale nkuruma walinyong'onyea..kwa lugha ya magazeti ya tanzania ungedema "kitila achafua hali ya hewa Nkuruma"
 
kitila alipaswa kujua kwamba Mbeki alivyosema ukimwi ni ugonjwa wa maskini alisema kwa muktadha gani.kwa mfano; wakati mtu anakemea uzembe wa madereva, anaweza kusema "ajali barabarani husababihwa na uzembe wa madereva" sasa hapa haina maana kwamba ni kila ajali itakayotokea itakuwa ni usembe wa dereva lakini kulingana na mazingira ya kauli;kauli inakuwa ni sahihi.Sasa mbeki alipo sema vile. alitaka kuonyesha kwamba umaskini una mchango mkubwa katika kuenea kwa ukimwi;kitu ambacho kina ukweli.
Aliyeulizwa swali ameshindwa kujibu, haya unayotoa ni mawazo yako binafsi.
Mnataka watu waulizwe maswali rahisi ili kuwafuarisha ama?


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Mkuu sixgates jee Kitila aliuliza kuhusu mtoto wa Mbeki kufa kwa UKIMWI?

Au muanzisha mada Kiingereza kimempiga chenga hapa anatulisha kasa?
 
Last edited by a moderator:
Mhadhiri Mwandamizi wa UDSM, Dr. Kitila Mkumbo jana alimpa wakati mgumu Rais wa zamani wa Afrika Kusini Thabo Mbeki.

Hiyo ilikuwa ni katika wakati wa maswali kwa Mbeki baada ya hotuba yake katika ukumbi wa Nkrumah wa UDSM.

Swali la Dr. Kitila lilijikita katika kauli ya Mbeki, wakati akiwa madarakani, kuwa UKIMWI hauenezwi na ngono ila shida na umaskini wa wananchi. Dr. Kitila alimkumbusha Mbeki juu ya kifo cha mtoto wake (wa Mbeki) kilichosababishwa na UKIMWI. 'Unaendelea kusimamia kauli yako?' aliuliza Dr.Kitila

Mbeki aliacha kujibu hilo swali. 'I will not respond to that pinching question' alisema Mbeki. Na hapo ndipo ukawa mwisho wa maswali kwa Mbeki ingawa swali la Dr.Kitila lilikuwa la pili tu.Prof. Mukandala alimaliza muda wa maswali ghafla

HUYU KITILA NKUMBO hana akili utaulizaje swali kama hilo ambalo linalenga familia ya unayemuuliza utafikiri ni mwandishi wa magazeti ya udaku aka tabloids. jukwaa lile lilikua la kuelimishana na maswali yangekua direct yanatoa ukweli bila ya kugusa mambo sensitive ya kifamilia.
 
Inaonesha kuwa mtu anaejiita "doctor" Kitila Mkumbo, hajui alifanyalo na zaidi alitaka kujionesha mbele za watu.

Kwanza kabisa, kama yeye si mwanafunzi hapo alikuwa hapaswi kuulizia maswali, hiyo ilikuwa ni fursa ya wanafunzi kuuliza ili wapate kujifunza, yeye huyo angechukuwa fursa hiyo kuwatazama wanafunzi wanachouliza, wanavyojibiwa na baadae kwenda kuvijengea hoja akiwa na wanafunzi wake.

Ikiwa hao ndio wakufunzi wa Tanzania, si hasha tunatoa wanafunzi wa vyuo ambao hata spelling hawajui.
Maswali yaliruhusiwa kwa yeyote aliyekuwa ukumbini, Dr kitila alikua na haki ya kuuliza.

Mbona kama umepata jazba kupita kiasi??


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
HUYU KITILA NKUMBO hana akili utaulizaje swali kama hilo ambalo linalenga familia ya unayemuuliza utafikiri ni mwandishi wa magazeti ya udaku aka tabloids. jukwaa lile lilikua la kuelimishana na maswali yangekua direct yanatoa ukweli bila ya kugusa mambo sensitive ya kifamilia.

Kwani uyo Mbeki alivyosema kuhusu ukimwi unasababishwa na umaskini unajua alizigusa familia ngapi ambazo zina wanandugu waliofariki kwa ukimwi au wanaougua gonjwa hili??
Uwanja ulikuwa wazi kwa swali lolote linayoigusa jamii.
Dr. Kitila aliuliza swali zuri sana.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Ninachokiona hapa wengi wameacha hoja ya msingi
na badala yake wanamuattack Dr. Kitila, nadhani kwa
chuki au vinginevyo. Ingalau wewe umesema jambo la
msingi sana...

Nadhani hakuna attack yeyote kwa Dr Kitila, watu wanaitaji tu kufahamu kama yupo humu ni vizuri atuweke sawa kuhusu swali lake.
 
- Dr. Kitila, ni mmoja wa viongozi ninayemuheshimu sana huko Chadema na ninajua kuwa ni kichwa na ndiye anayepaswakuwa MWenyekiti wa Chadema ila kwa vile huko kumejaa vilaza kuanzia wanachama na wapambe hawezi kupewa nafasi kubwa kama hiyo wataishia kupeana hao vilaza,

- I have no comment kuhusu mawaswali aliyomuuliza huyo Rais mstaafu, ila nashangaa kusikia hakujibu WHY? Sasa usipojibu ndio unatoa nafasi kwa watu kuamua wanayoyataka na kukusingizia uongo mwingi, hivi ni lini Viongozi wa Africa watajifunza kuwa wawazi? I mean ona Obama ameambiwa na MWananchi tu wa kwaida Donald Trump kuwa sio Raia wa USA, the the most powerful man in the world si angesema sio lazima ajibu, lakini imebidi mtumzima Obama aonyeshe mpaka vyeti vyake vya kuzaliwa kumjibu Trump!

- I dont care kuhusu swali la Dr. Kitila even though kwa kuwa najua ni kichwa najua kwamba alilipima na yuko right kuliuliza, nina tatizo sana na swali kutkujibiwa ndio huwa ninaita nonsense! Mbeki alitakiwa kujibu tena kwa ufasaha na kama anaamini alikosea aseme sio kukimbia swali!

- I HAVE SO MUCH RESPECT KWA DR. KITILA THAT NINAAMINI SWALI LAKE NI JUSTFIED ILA TATIZO NI VIONGOZI WA AFRICA KUJIFUNZA KWUA WAWAZI SASA NA KUACHA KUJIFICHA FICHA NYUMA YA VIVULI VYAO!

BRAVO DR. KITILA, NEXT TIME KAMA HAWAWEZI KUJIBU MASWALI YENU MSIWARUHUSU KUJA KUPOTEZA MUDA WENU HUKO KWENYE VYUO VIKUU VYETU, MAHALI PA WASOMI NI WEWE ULIYEKUBALI KWENDA SASA ULITEMEA NINI KWAMBA WASOMI WATAKUBEBA BEBA TU KAMA MTOTO MDOGO, SAAFI SANA KITILA!!

Le Mutuz!!

Sijaona umuhimu wa kuingiza neno CHADEMA kwenye mjadala huu na kuita watu vilaza.
Tujadili tu hili swali zuri la Dr. Kitila ambalo Mbeki amekua mzito kulijibu.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 

Ndio, kasa ama turtle kwa Kiingereza.


images


*Tanabahi
Kwa Kiswahili cha pwani kulishwa kasa maana yake ni kulishwa taarifa zisizokuwa na uhakika wa ukweli wake kama kulishwa kasa ambae kwa mujibu wa sheria za Kiislam uhalali na uharamu wake una utata
 
Ndo maana ya kuwa na Google.

Sio Google tu, hata Mamma na Ameoba bado hazitoi taarifa zozote kuhusiana na mtoto wa Mbeki aliyekufa kwa UKIMWI. Hayupo kwenye kumbukumbu zozote za mtandao wa intaneti.

Kama wewe unamjua jina lake tuwekee utusute
 
Tatizo letu tunafikiri UKIMWI ni ugonjwa wa MASKINI peke yao.Je inamaana hakuna matajiri wanye maabukizi ya Virusi (HIV/AIDS) Je hakuna wabunge na mawaziri walioathirika na ugonjwa huu.Je ni sisi walala hoi tu?Kwa maoni yangu Dr.Kitila aliuliza swali zuri sana ili tunapofanya jambo tuangalie na matokeo yake.
Na pili Thabo Mbeki alipaswa kuomba radhi kwa ile sentensi yake kuwa umaskini wa mtu ndio unaomletea au utakaomletea UKIMWI.Ukiangalia kwa mapana wenye pesa ndiyo waathirika zaidi kuliko hao maskini sababu ya kutumia vibaya hizo pesa zetu tulizonazo.
 
Nimeshaanza kuwa na wasiwasi na uelewa wa hawa wasomi wetu ambao ndio tunaowategemea,ndugu umeeleza vizuri sana ,huyu Dr Kitila kaonyesha umbumbumbu wa hali ya juu,na nakubaliana na mdau kuwa kuingiza hilo kwenye mambo binafsi huo ni ufinyu wa akili,hasa kwa mtu msomi kama Kitila(?)nafikiri pia huyu Dr wakati alitaka tu kujionyesha kuwa anamjua Mbeki ndani nje na mwishowe kaharibu wakati ambao wengine wangetumia kuuliza maswali,unapomuuliza mtu kwa kurejea mambo yake binafsi ana haki ya kuhamaki ,na sawa hata yeye Kitila umuulize swali na kwa kufuata mambo yake binafsi tena yanayohisi kifo sijui kama angefurahi.Kwa mila mambo ya vifo yanayomhusu mlengwa hayaletwi kwenye mijadala,huo ni kukosa heshima na adabu

Wewe ni mmoja kati ya watu mnaotaka kumjibia Mbeki swali aliloshindwa kujibu.
Swala la ukimwi linagusa familia ya kila mmoja wetu hapa duniani,
sasa nyie kama mnamuona Mbeki ni mungu na hapiswi kuulizwa maswala ambayo yeye mwenyewe ndo kaanzisha mjadala wake mtakua mnapotoka sana.
Dr. Kitila aliuliza swali zuri sana.
Watanzania acheni uoga, nyie ni mfano wa wananchi wanaoshindwa kuwauliza viongozi wao maswali ya msingi kwa kuogopa kofia za uongozi wao.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom