Dr. Isaac Ndodi, jirekebishe

Dr. Isaac Ndodi, jirekebishe

Ni imani za kisabato anachanganya na science ya tiba.Nimeenda hadi ofisini kwake na wale wahudumu wake almos wote ni wasabato.Mimi mwenyewe huwa namsikiliza nikiona kwangu positive nachukua na nikioana negative naacha.Lakini jambo ambalo kwangu negative kwa mwingine ni positive.Na biblia ndivyo ilivyo kila mtu anatafsiri kivyake na ndio maana kuna utitiri wa madhehebu.
Nb nimeenda hadi ofisini kwake na nadhani anachohubiri vingine havifuati

Unaona unavyojichanganya sasa?
 
Ndio hivyo mkuu.Bible kila mtu anatafsiri kivyake.Si unakumbuka ya kina Kibwetere wa Uganda???Nimekumbuka kuna wale Sabato masalia waliotaka kupanda ndege bure kwenda ulaya.

Kumbe yote haya unayajuwa tukikemea imani za kijinga hamtuelewi, sasa Ndodi anahubiri mswahili asioe wala kuolewa na mzungu bado na akili zako utasema yuko sawa ni kiimani zaidi?
 
Mkristo anachukia Yesu Kristo anapotangazwa kwa mataifa yote??? Mkristo wa wapi wewe?

Kushauriwa usinywe pombe haina maana anayetoa ushauri ni mjinga, ila anayeukataa ndio nina uhakika hana sababu ya msingi anayoweza kutoa kuthibitisha pombe au vileo vina faida au manufaa gani katika maisha yake. Mkristo wa KWELI anatambua kuwa mwili ni hekalu la roho mtakatifu, hivyo kuliharibu na kulitia unajisi kwa pombe sio hekima wala sio Ukristo.

Sioni kinachokuchukiza anapomtangaza Yesu Kristo, hata waandishi maarufu wanaheshimika duniani kama Dr. Ben Carson (MD) ameandika vitabu maarufu kama Gifted Hands, Think Big, Big Picture na anamtangaza Yesu Kristo ndani yake.

Kama kweli ni Mkristo wa kweli, usione aibu kumtangaza Yesu Kristo maana YEYE pia atakuonea aibu mbele ya Baba yake. Na pia kusikiliza kipindi sio lazima.

Samahani lakini.

Yeye ameombwa atoe andiko linalokataza Watu weusi kuoa wazungu basi. Kama hana la kuongea akahutubie sabatoni na si kwenye TV maana wengine tunataka kuangalia vipindi vya maana. Vipindi si kama wanaangalia wasabato akitaka hivyo aende kwenye matv ya dini yapo mengi tu.
 
Yeye ameombwa atoe andiko linalokataza Watu weusi kuoa wazungu basi. Kama hana la kuongea akahutubie sabatoni na si kwenye TV maana wengine tunataka kuangalia vipindi vya maana. Vipindi si kama wanaangalia wasabato akitaka hivyo aende kwenye matv ya dini yapo mengi tu.

Asante mkuu kwa ufafanuzi huu muruwa maana hapa nilishanyang'anywa hadi Ukristo wangu.

Hawa ndio wale utawakuta kwenye vituo vya daladala na mibiblia yao wanapigiwa watu kelele huku wenyewe wakiamini wanahubiri Injiri ya Kristo.
 
Wape maskini mvinyo wasahau shida zao.
Wakizimuka shida zinzrudi, unawapa tena Konyagi, wakizinduka unawapa vodka, wakizinduka wanajikuta back Ni mskini, unawapa tena dozi ingine,mwisho wanakuwa addicted hawana uwezo vodka/konyagi watabaki na bongo then kufa
 
I second with that, wasabato na shangazi zangu wasilamu mimi huaga siwaelewi kabisa, nimejaribu kuwaelewa nimeshindwa. Nime give-up.

Hata siku moja huwezi kuwaelewa maana wewe si mmoja wao
 
Nipe tofauti kati ya beer na alcohol.

Bia ni kinywaji kinachotengezwa na kimea mf shayiri, tufaa(apple) pea,.....(malt)

Itakuwa pombe endapo itachachushwa (fermented)

Alcohol ni spirit...inaformula (CH)nOH....n in-represent number za Carbon-Hydrogen bond...
Kinachofanya kuwa alcohol ni hiyo Group OH...

Alchol maarufu katika vinywaji vyote vye alcohol ni C2H2OH....(.Ethyl Alcohol)

Alcohol yenye Carbon moja CHOH inaitwa Methyl Alcohol ambayo ni hatari kwa mtumiaji maana metabolism yake inatoa sumu kali iitwayo Methaldehyde...hii huaribu Optic Nerve na kumfanya mtu kuwa kipofu au kusababisha kifo kabisa..

Pombe za kienyeji ambazo hazifuati formula za uchachushaji hutengeneza aina hii ya pombe..

Ndio maana kwenye Bia zote utakuta wameandika 4.5% alcohol or 0% alcohol

Ahsanta
 
Jamaa nilianza kumsikiliza kitambo na nikamkubali sana,kama muinjilisti na pia tabibu wa magonjwa kwa dawa za asili.tatizo ni pale alipoakuwa akiulizwa kuhusu gharama zake,zinasaidia vip watu wahali ya chini,sikuona kama anajari zaidi ya kujitetea kuwa anaziandaa kwa gharama kubwa...,akaulizwa kuhusu kiingilio,hapa napo hapakuwa na jibu la kibinaadamu zaidi ya kufa kufaana.

Okey haikuwa ishu saana,nikaendelea kumsikiliza,maana baadhi ya tiba anatoa maelekezo moja kwa moja na wengine tunaokota machache hapo.

Alipoanza mafunzo ya ujasilia mali na ufugaji kuku,nikaanza kupata wasi wasi kuwa huyu,ni mtaalam sawa,ila pia ana kipaji cha uongeaji ambacho kama hauko makini utaamini kila anachokuambia,sasa nikahisi akili yangu inanikumbusha kuwa hata baadhi. Ya aliyokuwa akifundisha huko nyuma ni sehemu ile ile ya karama aliyopewa ya maneno mengi.

Kuna siku alisema kula chakula huku unakuywa maji utapata kitambi,mwaka wa kumi sasa nafanya hayo sioni tumbo la kizembe.

Anafundisha mengi sana yenye tija tatizo ni hilo,mwepesi sana mdomoni,kinachosababisha wakati mwingine kuhama mada,kusahau hata alikuwa anazungumzia nini.ndilo hilo pia linasababisha kuongea ambayo hata hayapo.

Sent from my radio
 
Hata mim zaman nilikuwa nawaona hawa jamaa vichaa kamili.Mfano hawatumii majani ya chai na wanatumia "mchaichai" kwa sbb majan ya chai yana madhara kwa bindadam.Ni dhahiri sasa wao ndio wazima na tunaowapinga ndio vichaa wa ukweli.

madhara ya D 5, haya kwa akili zako unadhania ni wasabato tu hawatumii majani ya chai? Na kwa wasabato si kwamba ukitumia ni dhambi wao kawaida wana elimu ya afya ambapo wanafundisha mambo mengi sana ikiwemo, swala la kunywa maji maji safi na salama. hivyo usipende kukariri mambo
 
kumbe shida ni alipoiponda pombe!Kama kweli wewe ni mkristo haitakuboa ukiona mtu anasoma biblia au kuhubiri habari za Yesu,vinginevyo Ukristo wako utakuwa na mushkeli.

nikweli.ndugu.
 
msilewe kwa mvinyo maana ndani ya mvinyo kuna ufisadi. hapa atukanwe nani tena bibilia au?
 
Bia ni kinywaji kinachotengezwa na kimea mf shayiri, tufaa(apple) pea,.....(malt)

Itakuwa pombe endapo itachachushwa (fermented)

Alcohol ni spirit...inaformula (CH)nOH....n in-represent number za Carbon-Hydrogen bond...
Kinachofanya kuwa alcohol ni hiyo Group OH...

Alchol maarufu katika vinywaji vyote vye alcohol ni C2H2OH....(.Ethyl Alcohol)

Alcohol yenye Carbon moja CHOH inaitwa Methyl Alcohol ambayo ni hatari kwa mtumiaji maana metabolism yake inatoa sumu kali iitwayo Methaldehyde...hii huaribu Optic Nerve na kumfanya mtu kuwa kipofu au kusababisha kifo kabisa..

Pombe za kienyeji ambazo hazifuati formula za uchachushaji hutengeneza aina hii ya pombe..

Ndio maana kwenye Bia zote utakuta wameandika 4.5% alcohol or 0% alcohol

Ahsanta

Nashukuru kwa kunifahamisha, kati ya alcohol na beer ni kinywagi kipi kinafaa kitumiwa au kunywewa?
 
Back
Top Bottom