Dr. Bashiru, CCM ilipasuka 2015, hutaweza kuiunganisha kwa kukumbatia wasaliti

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,982
218,918
Bado sijajua hasa mwaka ambao Bashiru Ally aliingia kwenye siasa , lakini baada ya kumfuatilia kwa undani nimegundua kwamba huyu ni miongoni mwa WANASIASA WACHANGA SANA ambaye hana uwezo wa kuongoza CCM ya sasa , ameshindwa kujua kama ile CCM iliyofufuliwa na Kinana imekufa na kusambaratika kabisa.

Mwaka 2014 kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ndipo hasa kifo cha CCM kilipoasisisiwa, ukiua chama katika ngazi ya matawi ufahamu kwamba unaua chama chote hadi juu. Kwa mfano, Mtaa wa Keko Magurumbasi A kulikuwa na kiongozi wa CCM aliyeitwa Fundi , huyu aliondolewa kwenye kinyang'anyiro cha serikali za mitaa kwa mizengwe, akahamia CHADEMA.

Hakugombea chochote lakini alitumika kusambaratisha kabisa CCM Kata ya Keko, ambapo katika mitaa mitano CCM iliambulia mmoja tu tena kwa wizi. Nafahamu kwamba lengo la Bashiru Ally kuagiza marudio ya uchaguzi ni kujaribu kuondoa makovu yaliyosababishwa na uonevu lakini amesahau kwamba CCM Makao Makuu ndio chanzo cha uchafu wote huu wa kuondoa michakato halali ya kura za maoni na kukumbatia Wasaliti " walionunuliwa " ama kusaliti kwa hiyari.

CCM makao makuu imesimamia kikamilifu uvunjwaji wa katiba ya chama chao ya kupiga marufuku kura za maoni ili kuwapitisha tena Wasaliti ikiwa ni masharti ya mikataba ya ununuzi, ambapo Mwenyekiti wao Mh Magufuli alichukua nafasi ya Yesu Kristo na kuonekana akiwaambia wahamiaji kwamba " Njooni kwangu msumbukao na mizigo ya dhambi nami nitawapumzisha " Astaghafillulah ! wala hakuna mtu yeyote ndani ya ccm aliyelikemea hili , walishangilia na kupiga makofi mengi .

Sasa leo wanaCCM halali waliopigania chama chao kikamilifu wakati Bashiru akiwa UDSM, wakati wanaCCCM wanapambana kuinua chama wakishirikiana na Migiro na Kinana Bashiru hakuwepo wala wasaliti wake anaotaka kuwabeba hawakuwepo.

Nakuhakikishia Bashiru kwamba ukitaka kuimalizia CCM endelea kuwabeba wasaliti wako.

Itaendelea ...
 
Labda nyie

Ova
Pengine wewe ni mchanga katika siasa za ndani yavCCM.
Kupasuka kwa CCM kulianza na MTANDAO wa JK mwaka 2005.
Mkoani Mbeya katka uchaguzi wa MNeC, CCM waliparurana hadharani na mtandao ulidhamiria kumuondoa Mwandosya kipenzi cha wana CCM, vijana kwa wazee mkoa mzima.

Mshindi katika kuparurana huko alikuwa ni CHADEMA.
Vijana wote wakahamia huko.
Tumeshaandika sana juu ya hilo.
 
Bashiru bado kinachomsaidia ni ubabe wa mteuzi wake. Ni mitulinga lakini akili kidogo. Hana tofauti na makamba baba, thinking capacity was very very low! Kinachowasaidia ni nguvu ya dola!
Dr Bashiru anatumia zaidi sayansi ya siasa ndio maana Ufipa inafutika kwenye ramani ya siasa za Tanzania.
 
Mkuu, CCM wanakunyima usingizi sana eee, wewe tota lini umeijua CCM kiundani hivi? Bashiru umeanza kumfahamu lini? Pole sana, ila naona taratibu umeanza kuelewa somo
 
Dr Bashiru anatumia zaidi sayansi ya siasa ndio maana Ufipa inafutika kwenye ramani ya siasa za Tanzania.
Mh, sasa policcm ya nini kama kuna political science from Bashiru!. Kukataza mikutano, kuzuia hata mikutano ya ndani etc, etc, etc, etc, etc! John nilishakwambia kuwa nilikuwa nakufikiri kama somebodyreasonable amng Lumumba , kumbe na wewe ni hao hao!
Unadhani ukiweka equal political environment na CDM mtaambulia hata mtaa mmoja?
 
Mh, sasa policcm ya nini kama kuna political science from Bashiru!. Kukataza mikutano, kuzuia hata mikutano ya ndani etc, etc, etc, etc, etc! John nilishakwambia kuwa nilikuwa nakufikiri kama somebodyreasonable amng Lumumba , kumbe na wewe ni hao hao!
Unadhani ukiweka equal political environment na CDM mtaambulia hata mtaa mmoja?
Akirudi kujibu nistue mkuu
 
Mh, sasa policcm ya nini kama kuna political science from Bashiru!. Kukataza mikutano, kuzuia hata mikutano ya ndani etc, etc, etc, etc, etc! John nilishakwambia kuwa nilikuwa nakufikiri kama somebodyreasonable amng Lumumba , kumbe na wewe ni hao hao!
Unadhani ukiweka equal political environment na CDM mtaambulia hata mtaa mmoja?
Katika mazingira ya sasa Chadema wamepoteza ushawishi kwa wananchi kwa sababu kile kilichowapa umaarufu ndio hicho kinachompa umaarufu Rais Magufuli namaanisha vita dhidi ya rushwa na ufisadi.

Tena Dr Magufuli ameenda mbali zaidi kwa kuweka ulinzi wa rasilimali zetu na kuwapa mrejesho wa keki ya taifa wananchi wanyonge!
 
Back
Top Bottom