Dowans: Another Richmond in making?

Dowans: Another Richmond in making?

Ama Kweli Uungwana Ni Vitendo.
Yani sasa nchi ni kama hata haina Rais.
Na mwenyewe sasa yuko wapi?
Hao mambo ya ZIMBABWE SI YASHAISHA?
VIPI KUHUSU ZILE HOTUBA ZAKE SIJUI NI ZA KILA MWISHO WA MWEZI?
SALVA NAYE MBONA KIMYA?
MBONA HAKUNA ANAYEKAMATWA?
KUNA WANAOSUBIRIWA WAFE?

Watanzania tumeshachoka na hotuba zake za kila mwisho wa mwezi ambazo hazina kichwa wala miguu. Umekaa na watu wazima ndani ya chumba na meza uliyokalia wewe kuna kinyesi, na kila mtu aliyekuwepo katika chumba kile anaona kuna kinyesi. Wote wanasubiri uwaambie kinyesi kile kimefikaje pale juu ya meza na vipi utaondoa kinyesi kile maana wewe ndio mwenye nyumba. Lakini unajibaraguza baraguza kuongelea vitu ambavyo wote hawana hamu wala hawataki kuvisikia. Lakini hugusii chochoye kuhusu kile kinyesi.

Mwezi uliopita alitaka kuzungumzia mafanikio makubwa ya Sullivan Summit, bahati mbaya tukamwahi hapa JF na kusema kama angetoa hotuba basi ingekuwa ni kuhusu SS.

Mwezi huu anaweza kuzungumzia Zimbabwe wakati sisi wenyewe tuna matatizo chungu nzima. Mhishimiwa JK Watanzania tunataka kujua kinyesi juu ya meza yako kimefikaje na je utakiondoa vipi au nani mwenye jukumu la kuondoa kinyesi hicho. Tumechoka na uwongo kila kukicha. Hebu kuwa mkweli wa nafsi yako na uzungumze na Watanzania kile ambacho wengi wetu tunataka kukisikia toka kwako.
 
Good point mwanatanu, kama MKATABA SI HALALI kwa nini wasubiri hadi Aug 1? . Bado hela zinapelekwa au? na kuna mtu aliwahi kuandika kwamba kuna Account maalumu imewekwa kwa ajili ya kupokea hizo hela? kweli hiyo account Ipo? na ilianza lini? Watu wa Bank au wachumguzi please tusaidie kwenye hilo.
 
Aisee hilo la hela kurudi ni ndoto... Mark my words no money will be paid, na hata wakipelekwa mahakamani hii itakua kesi ya miaka 50 kama ya valambia by then stakeholders watakuwa wamepumzika mahali pema peponi...
 
Mkataba miaka 2...umeisha lini rasmi? Why usubiri leo 1st August?..au ndo umekwisha kiaina...?
kama Mkataba ulikuwa Feki...hatua gani zinachukuliwa...pesa kurudishwa na wahusikwa kusukumwa Rumande...kama kusamehewa basi mali zao zitaifishwe....
kama Mwalim alitaifishwa mali za watu(japo wengine walipata kihalali), kwanini JK leadership wasichukue serious measures kukomesha Uonevu huu wa watanzania...

Mtindo wa kuwafanya watanzania Majuha umekwisha...!!!
 
Sasa hao DOWANS jamani....yani nasikia kutapika tu (msunyo)
 
Hatujawahi kuwalipa Dowans hela. Hela ipi mnataka irudi? Tupunguze kukurupuka.
 
mimi sikubali!je malipo ambayo walikwisha lipa inakuwaje?na wamegundua mkataba si halali walioingia mkataba batili watachukuliwa hatua gani?kusitisha tu haitoshi lazima tuambiwe kama zile pesa zetu zilizolipwa si kihalali zitarudishwa!


Heshima Mkuu Hollo
Naona hicho kitakuwa ni kitu kingine kinachopima akili zetu. Naoana kipimo cha kwanza kimeonesha kuwa watanzania si wajinga, tuliposema tunaibiwa sasa imethibitika kuwa kweli tumeibiwa, na wezi na walifanya mambo ya udanganyifu wanafahamika. Sasa akili yetu na uwezo wetu wa kujitawala utapimwa kutokana na jinsi tutakavyoshughulikia watu hao. Inaonekana wazi kabisa kuwa watumishi wa serikali na wa chama tawala wameshiriki kuiba mapesa. Sasa sijui kama watachaukuliwa hatua za kweli au watakaripiwa tu, au wengine watawatetea kama baadhi ya wabunge wetu na viongozi wa chama walivyoanza kuwatetea.
 
Dr. Iddriss Rashid katoa Press Release LEO ambayo inaonesha kuwa mkataba huo hautokuwepo kufikia August mosi mwaka huu. Najua hii ni habari njema kwa walio wengi na mbaya kwa wachache.

Taarifa zaidi tutafahamishana hapa.

Kwa wanaoangalia TBC wanaweza kuona hii habari muda si mrefu

Hodi janvin wakulu.

wanesema 'if God cooks no smoke'
 
Wandugu Naomba Mnikumbushe, Hivi Huu Mkataba Wa Richmond Haukuanza 2006, Kwanza Kwa Mwaka Moja Yaani Miezi 12 Na Baadaye Kuongezwa Kuwa Miezi 24? (sijui Hiyo Ni Dharura Gani). Sasa Kama Ni Miezi 24, Si Inakwisha 2008 (yaani Mwaka Huu) Sasa Mkataba Umekatishwa Wapi. Au Ndio Wadanganyika Tumesahau Na Sasa Tuna Shangilia Bure.

Macinkus
 
Nafikiri hapa wataunda tume muda si mrefu kuangalia pesa zitarudishwaje.

Na hii inawezekana ndio mwisho wa mapendekezo ya bunge. Nafikiri watanzania na wabunge inatakiwa wawe makini wote waliohusika na mikataba feki mahakamani tu
 
nasikitika hatua hii imechelewa sana..next time tuchukue hatua mapema kwa mambo ambayo yanaitia hasara nchi. .na hawa jamaa hawawezi kutulipa fidia cha muhimu tuzuie hiyo mitambo kama fidia. au mnaonaje wadau??
 
Hii sasa ni usanii wa daraja la juu zaidi, kampuni feki ila eti mkataba mpaka Agosti 1, yeah right! Halafu hakuna chochote kuhusu kurudishiwa fedha zetu na riba juu, na sijui wataendelea kulipwa hadi hyo Agosti 1? Yaani hatuna serikali, tuna majuha yamejibweteka pale hayaoni mbele ya pua na matumbo yao... ovyo kabisa!
 
Kama kawaida, cheap popularity, utavunjaje mkataba uliokwisha? na kama kweli ni batili, kwanini mpaka August 1 na si leo July mosi?

Hii ngoma ndo kwaaaanza inaanza, walicho tusaidia hapa ni kukiri kwamba kweli Dowans na baba yake Richmondi ni wizi mtupu na ubatili. Sasa tunataka tuanzie hapa warudishe kila walicho kwapua kinyume cha sheria, lakini pia wote walio husika kufanikisha wizi huu tuone sheria ikichukua mkondowake ipasavyo!

La sivyo watueleze kama sheria ya wizi ni kwa ajili ya wezi wa miwa tu na mikungu ya ndizi!
 
Mh. Ngeleja aliulizwa na mtangazaji wa tbc1 kuhusu pesa tulizokuwa tunawalipa dowans itakuwaje akajibu kuwa hili tutalishughulikia baadae ila watanzania wakumbuke kuwa NASI TULIKUWA TUNATUMIA GESI YAO PIA hili jibu ni wazi kuwa hakuna pesa itakayyo rudi baada ya muda utasikiwa wanasema thamani ya gesi waliokuwa wanatuuzia ama tuliokuwa tuanitumia ina thamaniya pesa tulizokuwa tunawalipa thats means hakuna pesa itakayorudi hilo tusahau pesa kurudishwa!!
 
Tuweni Makini Sana, Kama Mkataba Ulikuwa Unaisha July30,2008. Ina Maana Beyond That, Hakuna Mkataba! Sasa Kama Mtu Anatoa Notisi Ya Kuvunja Mkataba Unaoisha, Na Notisi Hii Anaitoa Ndani Ya Mkataba Na Mkataba Bado Uko Hai, What Are The Remedies? Huenda Kuna Dili Linasukwa Hapa Kumbeba Tena Richmond
Mimi Si Mtaalamu Lakini Kwenye Mkataba Ya Ujenzi, Ukimpa Mwenzako Notisi Ya Kumwondoa Kwenye Mkataba Huwa Unabeba Yafuatayo
1. Kumlipa Gharama Zote Za Kumwondoa Site(demobilisation0

2. Loss Of Profits
3.distrurnances
4. Loss Of Opprtunities
5. Overheads Cost

Isije Ikawa Hii Notisi Ya Dr Rashid Ni Kumsaidia Richmond, Ili Wamlipe Kuondoa Yale Mamtambo Yake Feki Pale Na Kumlipa Hizo Gharama Hapo Juu. Mafisadi Wanaona Km100 Mbele.
 
Kama kawaida, cheap popularity, utavunjaje mkataba uliokwisha? na kama kweli ni batili, kwanini mpaka August 1 na si leo July mosi?

Hii ngoma ndo kwaaaanza inaanza, walicho tusaidia hapa ni kukiri kwamba kweli Dowans na baba yake Richmondi ni wizi mtupu na ubatili. Sasa tunataka tuanzie hapa warudishe kila walicho kwapua kinyume cha sheria, lakini pia wote walio husika kufanikisha wizi huu tuone sheria ikichukua mkondowake ipasavyo!

La sivyo watueleze kama sheria ya wizi ni kwa ajili ya wezi wa miwa tu na mikungu ya ndizi!


Hawawezi kurudisha kitu kwa sababu Serikali iliridhia mkataba ikijua kuwa Kampeni ni feki. Hivyo huo ni uzembe wa Serikali, aliyeshindwa kutimiza wajibu wake hapa ni Serikali na sio Dowans. Wananchi tulie tu....tumeshaibiwa hivyo.
 
I want to know what happens to the service that "richmond/dowans" were supposedly providing, kuna plan b ya kupata hizo service? if there are equipments that were purchased si mali yetu, since it is our money which was used to purchase them?
 
Hongera MWANKYEMBE na kamati yako........!!!
Hongereni WATANZANIA.........!!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WOTE WENYE NIA NJEMA....
 
kampuni iliyoanzishwa kwa mtaji wa dola 100 ikapewa mkataba wa kuleta umeme kwa nchi ya watu milioni 40? Kwa dola mia moja unaweza kunua hata kompyuta ya ofisi?

Mkuu mwanakijiji, awali ya yote naomba ubadili kichwa cha mada hii, inauma sana, yaani sisi ni mandondocha? si kweli, japo mafisadi wanajitahidi kutufanya hivo lakini hatujawa bado, ndo maana tupo hapa tunamkoma nyani!

Back to issues, I beg your pardon, unamaana dola mia moja ama dola laki moja? kasome vyema mkuu labda umekosea, kwani hata mwenye shilingi alfu kumi anaruhusiwa kuanzisha kampuni ya kudeal na jambo kubwa kama hili? na je hamna vigezo ambavyo kampuni inapaswa kuwa navyo kabla ya kuingia mkataba mkubwa kama huu?
 
Back
Top Bottom