Dark City,Dr.Slaa, with due respect.
Hoja kuwa Serikali ilihalalisha kununuliwa kwa mitambo ya IPTL haiwezi kuhalalisha kununua mitambo mingine chakavu tena eti tuu kwa sababu kuna maamuzi yaliyofanywa ya kipuuzi hapo awali ya kununua mitambo ya IPTL.
Hoja kuwa tusiingize hisia, kwenye siasa ninyi wanasiasa huwa mnasema kuwa politics is about perceptions, sasa kwanini kwenye hili hutaki pawepo na hizo perceptions?
Katika kuutafuta ukweli huwa unaanza na kuangalia tatizo lilipo na wakati unaendelea ndio unaweza kuupata ukweli wote , ila huwezi ukaanza na ukweli wote wakati lengo ni kufikia majibu yenye usahihi , hivyo kukubaliana nami kuwa wanamtandao wanaweza wakawa na mbinu hii kwa ajili ya kwenda 2010 ....unaelekea kuupata ukweli so go on searching.
Nasisitiza kuwa hatuwezi kununua mitambo chakavu kwa Bilioni 60,halafu tunasema kuwa ni kwa masilahi ya Taifa.
Dowans , kama leo tunawatambua basi kesi ya Gire kama alivyosema Mwanakijiji basi ni bora ikafutwa kwani kama tumemshitaki kwa kuingiza taifa hasara halafu wakatiu huo huo tunanunua mitambo aliyoleta sasa ni hasara gani?
Hivi ni kazi ya wabunge kuionyesha serikali inatakiwa kununua mitambo kwa mtu fulani?
TANESCO kama wanataka Mitambo watangaze tender na watu watajitokeza na tutaweza kupata mitambo mipya kwa masilahi ya Taifa hili.
Dark City,
Thanks. Ninakuelewa kuhusu wanasiasa na perceptions. Nilidhani hapa kwenye JF we are above perceptions and we attempt to search for truth and only truth. This is my only objective sina sababu nyingine.
Hoja ya Double Standards, ni hoja dhidi ya wale wanaokataa na hawasemi kitu dhidi ya ununuzi wa mitambo chakavu ya IPTL. I am not in any way justifying the same.
Issue ya kutangaza Tender is very plausible, lakini what are the facts hata kabla hatujatangaza Tender. What has emerged now that merits this subject to be debated. Kwangu mimi inaelekea bado kuna wingu zito limejificha katika swala hili ndiyo maana niko very eager, kupata ukweli wa kilichoko ndani ya Kamati ya Mashirika ya Umma na Kamati ya Nishati na Madini.Kati yetu nani anajua exactly what are the points of contention? Kama yuko ayaweke jamvini tuyachambua, ndiyo maana ninasisitiza kuwa swala zito kama hili is not only a matter of political interest, and therefore we must raise above our narrow political interests and argue and debate objectively and constructively.
Ndiyo maana ninafikiri hoja ni kwa Kamati hizi mbili zikae na kutupatia Taifa hili missing information.Maneno mazito sana hayo nilokuza MH.Dr.Slaa , ndio maana wengine tunatafuta kujua nini kinaendelea kati ya kamati hizi na ununuzi wa mitambo chakavu.
Campanero,Dakta Slaa inaonekana Mbunge Kijana tayari anaijua hiyo "missing information" ndio maana anatoa mapendekezo/hoja kwa kujiamini - mwambie aje atupe hiyo taarifa tusiyo nayo tumuelewe la sivyo ataishia kuwa kama Waziri Kijana aliyeingilia Sheria ya Manunuzi!
Mtazungushana hadi miguu iote sugu! Nunueni mitambo ya Dowans, walipeni kina Rostam, mwachilieni Gire, yaishe tusonge mbele.. hii kambi ni lazima tuanze kutoka sasa. Viongozi tumewachagua wenyewe, na tuwe tayari kuishi na kuona matokeo yake. Mkitaka kitu tofauti tuchague viongozi wengine!!!
Ochu, heshima mbele mkuu
Asante kwa analysis yako but with due respect I have to differ with your opinion.
Kama sheria ya Tanzania ndio imeanishwa kutumika katika huo mkataba basi uchambuzi wa sheria hapo juu waweza kuchukua mkondo wake.
Lakini, as i can feel it, this was a kind of International Business Transaction na inanifanya nichelee kukubaliana na wewe kuhusu hizo principles ulizoweka hapo juu unless umeona mkataba unasimamiwa na sheria ya nchi gani au kanuni zipi; yote yanawezekana, unaweza kuta Tanzania courts do not have jurisdiction on the matter na kwamba ikitokea kukiwa na msuguano wa mkataba, labda Iternational Arbitration will take over mfano mzuri ni Kesi ya IPTL na TANESCO ambayo ilifanyika hapa marekani.
Deal kubwa kama hiyo, I am sure jamaa watakuwa wameweka kifungu kinachoonyesha sheria ya nchi gani itatumika au vitu kama Incoterms au UCP.
Kwa hiyo tukiupata huo mkataba itakuwa vema na rahisi kuuchambua otherwise we are just dealing with some kind of speculation.
**************
Inavyoonekana Mawakala wa mafisdadi hawakosekani. Wako kila mahali, watajaribu kuweka uhalali katika kila haramu, wataliita giza kuwa mwanga, watachimbua kila sheria, watachunguza kila kipengele, kanuni, taratibu -- watatembea kila urefu wa kilometre hapa duniani na hata ahera ili tu watafute kisingizio cha kuwaibia Watanzania masikini.
INAONEKANA KAMA VILE HAKUNA SERIKALI HAPA KUZUIA HII. SERIKALI INAYO KILA HAKI KUSTOP -- KWANI LAZIMA??? WANANCHI TUSIKUBALI MAFISADI WATUZIDI KETE, TUSIKUBALI KABISAAAAAAAAAAA!
Mkandara,Mh. Dr. Slaa..
with due respect, mkuu wangu ZItto amechemsha!.. kachemsha big time kama alivyochemsha Masha ktk issue ya vitambulisho.. Ni kosa kubwa kwa kamati yake kuingilia swala ambalo sasa hivi halipo ktk siasa isipokuwa ni utekelezaji wa serikali.. hapa mkuu nakubaliana na Mwakeyembe 100 kwa 100..Hatuhitaji siasa ambazo zinakuja na fikra za muda mfupi!..Pili, kama kiongozi wa Chadema utelezaji mbovu wa sera nzima ya umeme ni silaha kwake na chama chake sio kazi yake yeye ku solve matatizo ya uongozi uliopo...tena kwa maamuzi mabaya kama haya.
Kitu kimoja alichotazama Zitto ni kuhusiana na nchi kuwa kizani?.. hii point haina mantiki kabisa kwa sababu hadi sasa hivi hatujainunua mitambo hiyo na nchi haipo kizani..hivyo muda huu unaotumika kubishana na kuundwa kwa kamati ni muda ambao ungetumika kuagiza mitambo mipya yenye guarantee ya warrant ya miaka mingi zaidi...Licha ya yote hayo mitambo ya Dowans ni chakavu kinyume cha kanuni na sheria za manunuzi ya mitambo..
Kutumia siasa na sababu ya mitambo ya IPTL ni makosa yanayorudiwa hivyo inazidisha kuonyesha jinsi tulivyo wafinyu ktk kufikiria..Ni sababu kama hizi ndizo zilizotuingiza ktk mikataba feki na mkingine ya kuuza mali zetu kwa bei ya NJUGU kwa sababu tumefikiria zaidi gharama badala ya vipengele muhimu zaidi ktk manunuzi kulingana na biashara inayokusudiwa..Tumefunga mikataba ya migodi yetu ya madini kwa sababu ya kufikiria gharama, tumeshindwa hata kusimamisha usafiri Dar kwa sababu ya kufikiria gharama, tumeshindwa kuweka vifaa na huduma nzuri bandarini kwa sababu tunafikiria gharama..Vitu vyote hivi kwa muda mrefu vimetugharibu zaidi na pia tumepoteza bishara kubwa kwa sababu sisi wagumu sana ktk maisha ku plan long term strategically hata iwe maisha yetu binafsi..
Hakuna hadithi hapa mkuu wangu, serikali iliyopo madsarakani ilituahidi kuwa mitambo ya Richmond ni ya muda mfupi tu na kwamba nchi yetu ina inest ktk uzalishaji umeme kwa nguvu za jua, makaa ya mawe na pia kuifanyia ukarabati mitambo iliyopo ili tatizo la umeme lisiwe tatizo la kudumu.. Hiyo promise iko wapi?..miaka mitatu sasa tunazungumzia kitu ambacho huwezi kunambia kwamba hawa watu walifikiri sisi wajinga sana kutuletea Richmond kampuni feki wakatuibia fedha zetu halafu leo tumefikia maamuzi ya kununua mali tuliyoibiwa..
mchezo huu ni sawa na wizi wa Vibaka ambao wanakuja kuibia taa za gari lako kisha kesho yake ukizitaka inabidi uzinunue tena toka kwao.. kwa sababu hakuna jinsi sheria zetu ni butu.. Ni maisha ambayo sasa hivi nyie viongozi mnataka kuyaingiza hata ktk utendaji kazi wa serikali..
Upuuzi mtupu..hakuna habari ya nchi kuwa kizani wakati mnalipia fedha kila siku kwa mkataba feki..kisa mnaogopoa nchi kuwa kizani kama kweli walikuwa na nia njema kwa nini waisifikirie hilo kabla Richmond hawajaingia nchini..besides, hakuna hata kiongozi mmoja aliyesimamishwa mahakamani hadi sasa...hizo objective arguement zitaanzia wapi?..
Ndiyo maana ninafikiri hoja ni kwa Kamati hizi mbili zikae na kutupatia Taifa hili missing information.
Dark City hapo ndipo kwenye mgogoro. Najiuliza kwanini chadema na wao wanajiona kama wako responsible na maamuzi ya ccm? Ni lini chadema wakawa washauri wa chama tawala? Maybe thats the case na tulikuwa hatujui. Nadhani ndio maana halisi ya mambo kama wizara vivuli,kamati nk. Ni mfumo usio rasmi.
Hata hivyo mbali na uchumi kuyumba,wananchi kukaa gizani si ndio sababu nzuri za kuindoa ccm madarakani kwa kushindwa utekelezaji? Ama kuna muungano wa kisisiri kati ya vyama hivyo?
Naona once again ni "Maslahi ya Taifa"
Lets wait and see...
Kiranja,
Asante kwa maswali yako mazuri sana. Nadhani hoja yako inakosa kwa misingi kadhaa:-
i) Hoja yako na maswali yamejikita katika Kifungu cha 2 cha Majukumu ya Kamati ya Mashirika ya Umma kwa mujibu wa Kanuni ya Bunge ambayo umeinukuu. Kwa bahati mbaya hapa nilipo sina Kanuni hivyo ninategemea umeinukuu vizuri hadi ukatuwekea hapa. Lakini-
a) hukugusia kabisa majukumu ya Kanuni kama yalivyo kwenye kipengele cha 3, 4, na 5.Vipengele hivyo vyote vinatoa nafasi kwa Kamati ya Mashirika ya Umma kushughulikia utekelezaji wa Maelekezo ya Kamati ( ingelikuwa busara ungelianzia kwa utafati kama Kamati hiyo iliwahi wakati wowote ilipokuwa inapitia mahesabu imewahi kutoa Mapendekezo yeyote ili kuinusuru hali waliyoikuta wakati wa utekelezaji wa jukumu lao. Ni jukumu lao sasa kufuatilia "utekelezaji wa maagizo yao". Generalization ni hatari sana. Hivyo vyema, kama unazo taarifa kuhusu mapendekezo hayo ungelituwekea hapa ili tufahamu hisia inayoanza kujengeka. Ni vyema Tanzania tusiruhusu "hisia" katika mambo makubwa kama haya.
b)Kifungu cha 2 cha Kanuni uliyoinukuu hapo juu kinazungumzia "tathmini ufanisi". Ni mpaka utakaponiambia kuwa Kamati ya Mashirika ya Umma haijafanya "tathmini" na au haina mamlaka ya kufanya tathmini ya ufanisi wa Tanesco, ndipo nitakapoona kuwa hoja yako ina msingi. Lakini iwapo Kamati katika taratibu zake za kawaida imefanya Tathmini ya shirika la Tanesco, basi ni vizuri "tathmini" hiyo ikafanyiwa mjadala kwa hoja zake bila kuunganishwa na chochote kinachohusiana na maswala ya Richmond/Dowans. Iwapo Kuna mambo ambayo Kamati ya Mashirika ya Umma imeyagundua ambayo ni kwa maslahi ya Taifa, sidhani ni vyema kuyakataa kwa vile tu Kamati nyingine imekwisha kufanya uamuzi. Ndiyo msingi wa hoja ya Kamati mbili kukutana ili mambo mapya yaliyojitokeza yafanyiwe kazi. Mimi nafikiri this is where our system becomes healthy, and with checks and balances. Hatuwezi kuyakataa mambo ambayo Kamati imegundua kwa kuwa tu tumefanya uamuzi, hata katika system ya Mahakama, kuna flexibility katika mazingira fulani fulani. Kama nimesoma sahihi ni kuwa Kamati ya Nishati na Madini ilikuwa haijawahi kuisikiliza TANESCO kama TANESCO . Hatuwezi kuadhibu Taifa kutokana na Technicalities na grounds ambazo hazina tija kwa maoni yangu. Iwapo Kamati mbili zitakaa kwa manufaa ya Taifa, mimi ninaamini kabisa mawazo ya watu wengi yana tija zaidi daima.
c) Kanuni ya 5 uliyonukuu inazungumzia Kufuatilia "utekelezaji wa Sera..." hivyo sioni kabisa mantiki ya hoja yako kwani huwezi kufuatilia utekelezaji wa Sera bila pia kutazama maswala yanayohusu capacity ya Taasisi husika.
2)Kiranja, Wakati nakubaliana nawe kuwa ununuzi wa mitambo hii inaweza kuwa mbinu mmoja ya Wanamtandao kupata fedha za uchaguzi kwa 2010, lakini hoja hii bado ni dhaifu sana, kwani huwezi kuadhibu Taifa zima likakosa umeme kwa sababu za kisiasa. Kuna njia nyingi zaidi za kudhibiti wanamtandao kuliko hii. Hivyo, objective debate na kupata definitive solution kwa maswala ya athari ya ukosefu wa umeme yasichanganywe na maswala ambayo kwangu yanahitaji majibu na hatua za aina tofauti kabisa. Let us sit down and think, and think aloud for the good of our country and avoid simplistic answers to complicated issues as this one.
4) Hoja ya kuwa TANESCO ilizembea kuagiza mtambo unaostahili tangu azimio la Bunge, kwangu pia is non issue. Uzembe wa uongozi wa TANESCO uwe dealt with squarely, bila kuhusisha na maswala ya msingi.
5) What I dont like is having double standards in our country. Tumeruhusu Serikali ijadiliane na IPTL kununua mitambo ya IPTL ambayo imetusumbua kwa zaidi ya miaka 15 sasa, na ni chakavu zaidi kuliko mitambo ya Richmond /Dowans at least one kama ilivyoripotiwa kwenye vyombo vya Habari. I have no problem kama issue ni kufanya independent assesment ya Wataalamu, hata kama inamaanisha kuingia gharama ya kuwapata wataalamu hao, iwapo tu tutathibitishiwa kuwa mitambo hiyo ni cheaper kuliko ku import mitambo ya aina hiyo hiyo au mipya kabisa. Wakati huo huo tunakataa kununua mitambo ya Richomond/ Dowans.
6) Maswala ya kijinai ya Richmond/Dowans yashughulikiwe kwa utaratibu wa Kawaida, na tunaweza kabisa kutenganisha maswala haya.
7) Swali la kwamba Serikali iliisha kulipa Richmond Dowans advance ya US$ 35 Million appears to me as a new revelation. But this is a separate issue and I think at this stage we need the Government to tell us the full story about its relations na watu hawa.Hata Bunge halikupewa Taarifa hii, and if this is true, this is very serious in my opinion. Hatujaambiwa pia kwanini Dowans hawajalipa hadi leo US $ 10 million ambazo wanatakiwa kutulipa kwa kila siku waliyochelewesha kuingiza umeme kwenye National Grid. Let us discuss the matter soberly na tutafikia ukweli na solution kuliko kujenga hisia.
Kamati hizi sioni wakija na jipya hata wakikaa kwani tayari kila mwenyekiti wa Kamati kwa muda wake ameshaweka msimamo ama wake au wa kamati yake hadharani kupitia vyombo vya habari.
Zitto akisema inunuliwe ,
Shelukindo akisema hatuwezi kununua mitambo chakavu .
Nafikiri kuna tatizo kubwa kuliko tunavyoliona hapa na kulijadili hapa wakati muafaka ukifika yatawekwa hadharani yale yaliyofichika.