Do's and Dnt's kama unalipenda Gari lako

Do's and Dnt's kama unalipenda Gari lako

Chemwali

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2011
Posts
397
Reaction score
178
Wakuu,

Jamani mwenye elimu yoyote kuhusiana na utunzaji wa gari. Maana kuna watu wanakaa na magari kwa miaka mitano (5) na bado jipyaa na kuna watu gari la aina hiyo hiyo kila siku garage.

Mwenye HINTS za kuzingatia tusaidiane ili wote tufaidike.

Kwa kuanzia:-

1.Ukizima gari hakikisha unaoff kwanza Radio and Ac
2. Gari ikiwa kwenye speed ukitaka kuchange Gia kuwa makini ukiweka Reverse ni rahisi kuua Gia Box
3. n.k
 
1. Kuzingatia service cycles na vifaa genuine (filters etc)
2. Kutumia mafuta, oil, maji/coolants na vilainishi vyenye viwango vinavyotakikana
3. Kuzingatia uwezo wa gari kuhusiana na mizigo (sio gari ya tani 2, inabebeshwa tani 5!)
4. Kutumia spare za gari husika na/au ambazo zinakubalika kitaalamu
5. Kuzingatia viwango katika aspect zote za magurudumu (alignment, balance, pressure etc)
6.....
 
Fuata kanuni za udereva.

1. Kagua gari kabla hujaingia

2. Cheki maji kwenye radiator

3. Hakikisha engine haivuji po pote na safi kadri uwezavyo (kila siku)

4. Cheki kama kuna kitu loose kikaze

5. Isafishe kama wewe mwenyewe unavojisafisha

6. Hakikisha upepo wa matairi upo sawa.

7. Hakikisha taa zako zinafanya kazi vizuri

8. Breki na honi zinafanya kazi

9. Ukistart acha gari ianze yenyewe usikanyage mafuta kwa dakika moja au mbili

10. Iweke gari mahali salama kwa hali ya hewa na shughuli za kibinadamu

11. Ukiona gari ina tabia todfauti, rekebisha usingoje mpaka isimame

12. Utakapofika mwisho wa safari rudia utaratibu wote

13. Kama hutaitumia kutwa nzima ipashe moto kwa dakika 5

14. Zingatia ushauri wa thread za hapo juu kwa maana ni za msingi
 
1.Epuka sana safari fupifupi kwani kawasha gari na kuizima kabla ya nusu saa hivi,engine inakuwa haijapata joto la kutosha hivyo inasababisha uchakavu wa haraka zaidi kwa engine.
2.Kupandisha au kushusha power windows gari ikiwa imezima ni kosa la jinai! Hii inapelekea betri kufa mapema zaidi!
 
dah hii thread imenifundisha mambo mengi sana,santeni wakuu nimewapa like za kutosha
 
1. usiiweke gari chini ya mti. kinyesi cha ndege na maua yanayodondoka kwenye gari yanaua rangi haraka.,
2. hakikisha unafanya service muda unaotakiwa na kwa wataalamu.
3. tumia oil husika, coolant badala ya maji
 
Jamani mwenye Elimu yoyote hapa,maana kuna watu wanakaa na magari miaka 5 bado mpyaa na kuna watu mwaka tu kila siku gereji..je kuna mwenye HINTS za kuzingatia atupie wote tufaidike

1.Ukizima gari hakikisha unaoff kwanza Radio and Ac
2. Gari ikiwa kwenye speed ukitaka kuchange Gia kuwa makini ukiweka Reverse ni rahisi kuua Gia Box

ETC

Gari yako ya mwaka gani? yani kabla ya kuzima kila saa uzime radio na ac kwanza!!!! nunua gari za kisasa zinazojua ni muda gani radio izimwe bila ya wewe kuzima hasa unapoiwasha.
 
kuna mada niliiweka miaka kadhaa iliyopita humu Jf kuhusu namna ya kutunza magurumu ya gari. Itafuteni, bado ni nzuri. Thread Inaitwa 'Je matairi yako ni salama?
 
Heri muwasaidie kwani wengi ni wale waliojifunzia kwenye kupiga raundi mtaani, mafunzoni waliona km wamewekewa makanika na madereva wa malori/ofisi so hawakuona umuhimu wa kwenda na matokeo yake hata matunzo ya vimeo vyao hawajui
 
Haahahahahhaaa......usiweke chini ya mti....kinyesi cha kunguru kinaua gear box.


hahahahahaa....

Gari yeyote ile zingatia:
1. Service Kwa wakati, na unatumia parts ambazo ni GENUINE always
2. Tumia amfuta safi tu epuka vituo vinavyochakachua mafuta
3. Gai isiendeshwe hovyo hovyo na "kila mtu" bila sababu maalumu,
4.....
 
gari yako ya mwaka gani? Yani kabla ya kuzima kila saa uzime radio na ac kwanza!!!! Nunua gari za kisasa zinazojua ni muda gani radio izimwe bila ya wewe kuzima hasa unapoiwasha.

kawaeleza wale wenye magari ambayo radio hazijui wakatiwa kuzimwa....
 
kuna mada niliiweka miaka kadhaa iliyopita humu Jf kuhusu namna ya kutunza magurumu ya gari. Itafuteni, bado ni nzuri. Thread Inaitwa 'Je matairi yako ni salama?

Weka link boss sio kila mtu anaweza kuitafuta
 
[/B]
hahahahahaa....

Gari yeyote ile zingatia:
1. Service Kwa wakati, na unatumia parts ambazo ni GENUINE always
2. Tumia amfuta safi tu epuka vituo vinavyochakachua mafuta
3. Gai isiendeshwe hovyo hovyo na "kila mtu" bila sababu maalumu,
4.....

Ikiwezekana jaza mafuta kwenye kituo kimoja na kutosha kumalizia mizunguuko ya siku hiyo ili kama kuna tatizo la mafuta ni rahisi kufuatilia historia ya ujazaji wa mafuta (sio unajaza lita 2 kituo hiki ukipiga misele kidogo inazuka safari nyingine unajaza kituo kingine na wakati wa kurudi tena unajaza wese kituo kingine)
 
Pia hakikisha kwenye axle (ekiseli) ya mbele na nyuma unaweka tairi zinazofanana yaani trade zake kwani vitu vidogo lakini vinasaidia gari hasa kwenye brake unapokanyaga zote zinafunga katika uwiano sawa kwa kuwa trade za tyre ni za aina moja ikishindikana basi angalau tyre za mbele weka zinazofanana na za nyuma weka zinazofanana.
 
Hakikisha inafanyiwa service/matengenezo na fundi mzuri mafundi wa hovyo wanachangia sana kuua gari
 
Jamani mwenye Elimu yoyote hapa,maana kuna watu wanakaa na magari miaka 5 bado mpyaa na kuna watu mwaka tu kila siku gereji..je kuna mwenye HINTS za kuzingatia atupie wote tufaidike

1.Ukizima gari hakikisha unaoff kwanza Radio and Ac
2. Gari ikiwa kwenye speed ukitaka kuchange Gia kuwa makini ukiweka Reverse ni rahisi kuua Gia Box

ETC

Mkuu hapo namba mbili gari inapokuwa kwenye mwendo haiwezekani kupiga gear ya reverse na ukaingia, mfano ukiendesha let say gari yako ni manual wakati unabadilisha gear toka na.3 kwenda na.4 hata kama itatokea bahati mbaya gia liva umeipeleka usawa wa reverse itapiga kelele kisha wewe unaivuta kushoto kidogo inaingia

Kwa upande wa automatic hapa kidogo kuna shida kwa kuwa madereva wengi huwa tunaingia barabarani kwa kuwa ni rahisi kuliendesha ila nalo reverse haiwezi kuingia kama gari lipo kwenye mwendo kwani gia liva inapokuwa pale kwenye D wengi anapoihamisha kwenda kwenye neutral huwa wanaisogeza huku amebonyeza ile button kubwa juu ya over drive (hapa ndio penye shida kwani gari ya automatic kutoka D kwenda Neutral unasukuma tu bila kubonyeza ikifika kwenye N inagota na haiendi kwenye reverse na the same kama ukiisogeza kwenye D 2 nako inasogea ila ukitaka iende L au reverse ndio unabonyeza ile button. Hii huwa inawakumba wale wazee wa kutaka kutumia neutral kwenye mteremko wanajisahau kusogeza tu gia liva wao wanasogeza gia liva huku wamebonyeza (jaribu tu kesho uone maana gia liva ya auto inasogea freely kwenye D, N na 2 inapokuwa kwenye mwendo except kwenye L na R ndipo unabonyeza kitufe kikubwa ndio inaingia
 
Back
Top Bottom