Doreen Wa Mrema! Naamini Mume wangu Hajafumba Macho

Doreen Wa Mrema! Naamini Mume wangu Hajafumba Macho

Jayden News

Member
Joined
Aug 28, 2022
Posts
29
Reaction score
94
Ninaamini baba hajafunga macho, kama alivyoniahidi, kuwa hata akifa hatafumba macho, na ninaamini katika maneno yake."

Unadhani ndugu wa Mrema watamuachia chochote?
 
Akaendelee tu maisha yake yale ya kabla hajaolewa na marehem Mrema atakuwa na amani kuliko kushindana na watoto wa marehem hata kama Mrema hajafumba macho
 
Huyo mama miezi mitano iliyopita wakati akiolewa alituambia wazi wazi kuwa kilichompeleka kwa Mrema ni Upendo (mapenzi) na sio mali za Mrema, maana hata yeye anazo mali zake na anashughuliki zake binafsi. Sasa Mrema ameshakufa (hayupo tena) anatafuta nini tena kwa ndugu wa Mrema?

Asimame na maneno yake sasa, aje atuambie hivi;
"nimeamua kuendelea na shughuli zangu za toka awali, niliyemfuata (Mrema) hayupo tena, maisha yaendelee kwa amani!"
 
Hapaswi kuwa "part of them" namanisha yeye kama yeye Kabla hajaoelewa na mlema alikuwa anapata wapi riziki ,je? Wamekaa mda gani na mlema kweny ndoa ,haya Mambo hayahitaji hesabu kubwa .tulia mtangulize mungu
 
Wakati utasema kuna mzengeaji karibu hapo anasubiri mgao asepe na mia
 
Huyo mama miezi mitano iliyopita wakati akiolewa alituambia wazi wazi kuwa kilichompeleka kwa Mrema ni Upendo (mapenzi) na sio mali za Mrema, maana hata yeye anazo mali zake na anashughuliki zake binafsi. Sasa Mrema ameshakufa (hayupo tena) anatafuta nini tena kwa ndugu wa Mrema?

Asimame na maneno yake sasa, aje atuambie hivi;
"nimeamua kuendelea na shughuli zangu za toka awali, niliyemfuata (Mrema) hayupo tena, maisha yaendelee kwa amani!"
Apewe kiinua mgongo chake cha kuwatunzia mgonjwa wao.
Watu awe na huruma, kuishi na mgonjwa wa stage ile ilikuwa ni msaada mkubwa sana kwa watoto.

Wampe kifuta machozi acheni kuongea utumbo
 
Apewe kiinua mgongo chake cha kuwatunzia mgonjwa wao.
Watu awe na huruma, kuishi na mgonjwa wa stage ile ilikuwa ni msaada mkubwa sana kwa watoto.

Wampe kifuta machozi acheni kuongea utumbo
Thank you,
Kuna watu humu kwenye nyuzi za wajane hawakosi kutwa kuwasimanga na kuwaombea mabaya wanasahau hao Marehemu wao enzi za uhai walitafuta Mali kwa nguvu na jasho ili wapate mwisho mwema wakiwa kwenye ubavu wa wapendwa wao,

Lakini baada ya kuondoka yanakuja majitu ya Roho mbaya wanataka kuweka dhulma na uroho wa Mali wasizozitafuta.
 
Hajafumba macho ?Hebu aache fiction.
Yupo Stage 1
images - 2022-09-01T080306.494.jpeg
 
Huyo mama miezi mitano iliyopita wakati akiolewa alituambia wazi wazi kuwa kilichompeleka kwa Mrema ni Upendo (mapenzi) na sio mali za Mrema, maana hata yeye anazo mali zake na anashughuliki zake binafsi. Sasa Mrema ameshakufa (hayupo tena) anatafuta nini tena kwa ndugu wa Mrema?

Asimame na maneno yake sasa, aje atuambie hivi;
"nimeamua kuendelea na shughuli zangu za toka awali, niliyemfuata (Mrema) hayupo tena, maisha yaendelee kwa amani!"
Hata mimi natamani achukue maamuzi haya. Hayo masuala ya baba kufumba macho, aachane nayo.
 
honeymoon is over
arudi sasa akadange alipokua mwanzo
 
Thank you,
Kuna watu humu kwenye nyuzi za wajane hawakosi kutwa kuwasimanga na kuwaombea mabaya wanasahau hao Marehemu wao enzi za uhai walitafuta Mali kwa nguvu na jasho ili wapate mwisho mwema wakiwa kwenye ubavu wa wapendwa wao,

Lakini baada ya kuondoka yanakuja majitu ya Roho mbaya wanataka kuweka dhulma na uroho wa Mali wasizozitafuta.
Sisi mama yetu alifariki miaka kadhaa, baba akaoa mwanamke umri wa kati.
Mzee akawa anasumbuliwa na sukari na huyo mke mpya ndiye aliyehangaika na ugonjwa wa mzee japo tulimkatia bima lakini mahangaiko ya mgonjwa ya mara kwa mara yeye ndiye alihusika kwa karibu.
Mzee alifariki mwaka jana; wakati wa kuvunja matanga niliongea wazi kuwa asitokee mtu wa kusumbua huyu mama.

Kila alichopewa ni cha kwake asiinue kichwa mtu yeyote kumsumbua hata kidogo.

Anaishi kwa amani tu.
 
Back
Top Bottom