The Listener
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 993
- 213
Kuna Bwana Mmoja na mkewe walikuwa wakijadiliana idadi ya watoto wanaowataka baada ya kuwa tayari walikuwa wamekwishazaa watoto wawili wa kike waliokuwa wakipishan kwa miaka mitano. Bwana mkubwa akawa anahitaji sana kupata mtoto wa kiume. Katika kuhakikisha kuwa azma yake inatimia alijaribu kupata ushauri toka kwa rafiki yake wa karibu aliyekuwa anafanya kazi ya udaktari wa mifugo. Mungu si Athumani mkewe akashika ujauzito lakini baada ya miezi tisa akajifungua mapacha wa kike. Hadi leo hii anawashauri watu kwamba wasijaribu kupata ushauri wa madaktari wa mifugo katika utabibu wa masuala ya kibinadamu