Dogo wa miaka 19 aliyefungua biashara ya 75M+

Dogo wa miaka 19 aliyefungua biashara ya 75M+

Kwanza nampongeza kijana,
Pili,kuna vijana wengi sana wa aina yake hapa Tanzania,tena wanamawazo makubwa na unique kushinda hili wazo lake,
Tatizo linakuja kwenye uwezeshwaji.Huyo amepata bahati kuzaliwa ktk familia yenye nafuu ya maisha,Hana kikubwa cha ajabu tumshangae.
 
Nilikuwa kwenye Youtube channel ya Millard Ayo nikakutana na stori ya kijana mmoja kwa jina Scott ambaye ni Mtanzania,aliyefungua biashara ya restaurant ya Pizza na ikanivutia kuangalia video hiyo..

Kwenye maelezo yake amesema alikuwa na lengo la kuwa na biashara yake kabla hajafikisha umri wa miaka 20+..

Alianza kusave fedha ambazo nyingine alikuwa akilipwa na mama yake alipokuwa anamsaidia katika kazi zake..

Pia aliuza gari aina ya Toyota Altezza aliyopewa zawadi na baba yake ili aongezee kwenye mtaji huku pia akiomba backup kutoka kwenye familia yake..

Katika maelezo yake nikagundua huyu kijana pongezi ninazoweza kumpa ni kuwa na idea ya biashara na kuishi katika ndoto zake and nothing else..maana inaonyesha familia yake iko vizuri,kwahiyo suala la mtaji sio big deal sana..



Wakuu katika jukwaa hili mnalipi la kuongea kuhusu kijana huyu na je biashara ni kweli inaanzia kwenye idea au both idea na mtaji vinaitajika ila kuanzisha biashara??
Tangu mwanzo huyo alkua na maisha mazuri ktk familia yao
 
Watanzania bhna bdo sana yani mtu amekua spoon feed tangu mdogo, mtaji kapewa ukute hata anaconection nzuri tu n hata plan pia,halaf unategemea awamotivate watoto wa peasant.
 
Halaf swala la kuuza gari si hoja ukute ameuza gari huku anayo mengne mawili au matatu yakutembelea so what's the point na Kuna vinguchiro vngne hapo juu vinasema ooh wengne wanakula bata sijui hawana nidham ya fedha kwani nani kasma ukila bata huna nidham ya hela kuna wengne huku self hustler wamepiga hatua kubwa na bdo mtu anakula bdo so sidhan kwamba huyo dogo kafanya k2 cha ajabu sana zaidi ya kiki tu, yani unategemea sisi wengne hata elf10 tu kupewa na mzazi ilikua mbinde maswali kibao sasa unataka kufananisha anayepewa gari
 
Hahahah wabongo bwana, mpeni credits zake tu mazee. Mi sijamfuatilia ila wacha nitaangalia hio clip yake nimskilize. Ila pizza na million 75+ ndipo ambapo sioni connection ya moja kwa moja. Ama amejenga hio ofisi kwa pesa hizo hizo from scratch maana navojua biashara huwa tunakodi majengo!
Ukiangalia na kusikiliza clip utaelewa!
 
Vitoto vya kibepari.Hakuna kipya hapo,ukiona kuna tajiri ujue kuna maskini anayemnyonya.
Halafu utasikia wajinga wachache watakwambia vijana waige mf wa scot.

Mfumo mbovu utaendelea kutengeneza tabaka tawala na tabaka tawaliwa.Wakati huyu anapewa Alteza ya kutembelea mwanafunzi wa kisarawe hana hata uniform za shule.
Endelea kulalamika hivyo hivyo, kama kulalamika kuliwahi kumletea mtu maendeleo!
 
In business PERSPECTIVE.
It doesn’t matter what amount of capita one is starting with. Amepewa, amekopa, ame save, or... But what's matter is PRODUCTION.
Nmeona kwenye interview hata mtangazaji (kwa hali ya mshangao) akiuliza mara mbili mbili alipopata mtaji na kusisitizia kumbe haja hustle.
Unaweza uka hustle ukapata mtaji then usi produce chochote kwenye biashara lengwa. Heko kwa dogo kwa umri wake na status yake kwa wengine ndo ingekua nafasi ya kula bata kisawa sawa lakini ule uthubutu tu wa kuuza gari na kupata pesa kwaajili ya business ni nzuri kuonyesha kwamba he gonna be a good business man in the future!
 
Mtaji ni wa muhimu sana haijalishi ni kiasi kidogo. Wazo na mtaji vinategemeana sana.
 
Write your reply... hivi kuna mtu asiyependa kuzaliwa familia kama hiyo, kingine ujue wazazi wake walihaso au mababu zake mpaka mtoto wao kuja kupata ahueni, kijisemea kwamba umrtokea chini hadi mafanikio sio fashen hiyo, jaribu kuchua kama funzo kwamba ukipambana leo mwanao atakuja kupata unafuu kama hivyo.

mafanikio ni mfanikio tu, pesa ni pesa haijarisho umeipataje wewe walaumu wazazi wako ambao wamekufanya uwe na hali hiyo.
 
Ndo maana mimi nikasema nampongeza kwa kuwa na idea na uthubutu wa biashara..ila kwenye jinsi alivyopata mtaji No
Hahaha, ulitaka na yeye ahenye kutafuta mtaji ndio umsifie ?? Hahaha mkuu hata kuwa na akili ya kuwaomba wazaz wake mtaji wa kufanya ujasiriamali inatosha. Kama unamkubali mkubali kwa kila kitu usinungu' nike kwa sabab dogo hajahangaika kama ww kufanya kaz za watu ili apate mtaji
 
Back
Top Bottom