Dogo wa miaka 19 aliyefungua biashara ya 75M+

Dogo wa miaka 19 aliyefungua biashara ya 75M+

Darmian

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
17,313
Reaction score
46,825
Nilikuwa kwenye Youtube channel ya Millard Ayo nikakutana na stori ya kijana mmoja kwa jina Scott ambaye ni Mtanzania,aliyefungua biashara ya restaurant ya Pizza na ikanivutia kuangalia video hiyo..

Kwenye maelezo yake amesema alikuwa na lengo la kuwa na biashara yake kabla hajafikisha umri wa miaka 20+..

Alianza kusave fedha ambazo nyingine alikuwa akilipwa na mama yake alipokuwa anamsaidia katika kazi zake..

Pia aliuza gari aina ya Toyota Altezza aliyopewa zawadi na baba yake ili aongezee kwenye mtaji huku pia akiomba backup kutoka kwenye familia yake..

Katika maelezo yake nikagundua huyu kijana pongezi ninazoweza kumpa ni kuwa na idea ya biashara na kuishi katika ndoto zake and nothing else..maana inaonyesha familia yake iko vizuri,kwahiyo suala la mtaji sio big deal sana..



Wakuu katika jukwaa hili mnalipi la kuongea kuhusu kijana huyu na je biashara ni kweli inaanzia kwenye idea au both idea na mtaji vinaitajika ila kuanzisha biashara??
 
Mi nampa pongezi kwa hapo alipofikia. Si haba kwa kweli. Hata kuwa na mtaji na kukamilisha ndoto yako ni kazi nayo, kwa sababu tumeshashuhudia watu kibao wanapewa mitaji mwisho wa siku wanaishia kuunguza pesa yote na hakuna cha maana kilichofanyika.

Muhimu MAINTAINANCE. Kama ataweza kumantain hicho alichofanya hapo anaweza kufika mbali.
 
Darmian ahsante sana kwa kuibua hoja muhimu na yenye kujenga mkuu.

Kwa upande wangu wazo la biashara linalofaa ni kitu muhimu sana. Lakini pia kusimamia uendeshaji na kuhakikisha wazo linakua biashara inayojiendesha ni sehemu muhimu.

Nimeona wengi wana fursa ya mtaji na kupata pesa lakini hawana wazo thabiti lamtaji lenye tija.

Tukirudi kwa huyu jamaa, ni kweli familia imembeba lakini sio kila anayetokea familia bora ameweza kufanya jambo la maana hususan kwenye biashara.

Fikiria angeweza kuamua kutembelea gari aliyopewa akafanyia anasa. Lakini kwa kuwa alikua na malengo, akaamua kuuza limsaidie kutimiza ndoto yake.

Kusave hakujamsaidia kutengeneza hiyo M 75+ lakini ni kitu muhimu sana kwa mjasiriamali. Inakupanidhamu ya pesa, watu wote waliofanikiwa, wananidhamu ya pesa, haijalishi unafanya biashara gani, kama hauna nidhamu ya pesa hautafika popote, hasa maendeleo endelevu.

Mwisho, kwa yeyote yule, ni vizuri kuwa na ndoto, namaanisha wazo lililofanyiwa kazi, malengo na mpango wa kutekelezeka.
Usipokua na wazo mathubuti, hata ukipewa 20M hautafanya jambo la maana, nafasi ya kufanikiwa ndogo sana.
 
Back
Top Bottom