Darmian
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 17,313
- 46,825
- Thread starter
- #21
Umenena vyema mkuu..Darmian ahsante sana kwa kuibua hoja muhimu na yenye kujenga mkuu.
Kwa upande wangu wazo la biashara linalofaa ni kitu muhimu sana. Lakini pia kusimamia uendeshaji na kuhakikisha wazo linakua biashara inayojiendesha ni sehemu muhimu.
Nimeona wengi wana fursa ya mtaji na kupata pesa lakini hawana wazo thabiti lamtaji lenye tija.
Tukirudi kwa huyu jamaa, ni kweli familia imembeba lakini sio kila anayetokea familia bora ameweza kufanya jambo la maana hususan kwenye biashara.
Fikiria angeweza kuamua kutembelea gari aliyopewa akafanyia anasa. Lakini kwa kuwa alikua na malengo, akaamua kuuza limsaidie kutimiza ndoto yake.
Kusave gakujamsaidia kutengeneza hiyo M 75+ lakini ni kitu muhimu sana kwa mjasiriamali. Inakupanidhamu ya pesa, watu wote waliofanikiwa, wananidhamu ya pesa, haijalishi unafanya biashara gani, kama hauna nidhamu ya pesa hautafika popote, hasa maendeleo endelevu.
Mwisho, kwa yeyote yule, ni vizuri kuwa na ndoto, namaanisha wazo lililofanyiwa kazi, malengo na mpango wa kutekelezeka.
Usipokua na wazo mathubuti, hata ukipewa 20M hautafanya jambo la maana, nafasi ya kufanikiwa ndogo sana.
Na ulipo malizia kwa kusema whatever the bussiness,NIDHAMU YA PESA ni jambo la muhimu sana.