Does this [Interview] give answers on our mining contracts??

Does this [Interview] give answers on our mining contracts??

Mkwawa

Katika Serikali ya CCM ondoa ndoto ya kutoa madaraka mikoani, wilayani na hata vijijini. Wanajua siku wakifanya hivyo tu, wananchi wataamka usingizini.

Lazima madaraka yawekwe kwenye central government ili yaweze kupikwa na wanasiasa au wafanyakazi wengine wa Serikali ambao wamebeba damu ya chama kwenye mishipa yao kuliko damu yao wenyewe.
 
http://www.mwananchi.co.tz/mwananchisite/Mwananchi/Habari/Habari3.asp





Serikali yafunga mgodi wa dhahabu Musoma

Na Mathias Marwa, Musoma

SERIKALI imesitisha shughuli za uzalishaji wa dhahabu kwenye mgodi wa Buhemba Gold Mine (BGM) katika Kata ya Buhemba, Wilaya ya Musoma Vijijini mkoani Mara, kutokana na madini hayo kupungua katika eneo hilo.

Mkuu wa Wilaya za Musoma Mjini na Vijijini, Saveli Maketa, aliwaeleza wafanyakazi 350 wa mgodi huo kuwa serikali imefikia uamuzi huo kutokana na sababu hiyo, lakini kuwahakikishia kuwa hakuna atakayefukuzwa kazi na wataendelea kulipwa mishahara yao kama kawaida.

"Serikali imetenga eneo lingine la kuchimba dhahabu baada ya dhahabu ya hapo kupungua, lakini hakuna mfanyakazi atakayefukuzwa na wote mtalipwa mishahara yenu kwa kipindi chote ambacho mtakuwa hamfanyi kazi," alisema.

Maketa aliwaeleza wafanyakazi hao kuwa mgodi huo wa Buhemba ni mali ya serikali pamoja na mali nyingine, ikiwamo mitambo yake na kwamba hata mishahara wanayolipwa ni ya serikali kupitia kwa mwekezaji kutoka Afrika Kusini.

"Mgodi, samani zote za ofisi, mali zote za hapa mgodini na mishahara yenu ni mali ya serikali ya Tanzania, hivyo ni mali zenu. Hao mnaowaita makaburu hawana chochote hapa bali wao ni mawakala tu wa serikali," alisema Maketa.

Alifafanua kuwa serikali haiwezi kumudu kukaa na wafanyakazi hao wote 350 wakati hakuna uzalishaji, hivyo utaratibu umepangwa wa kuwarejesha baadhi yao kwao ingawa wataendelea kulipwa mishahara yao na wengine watabaki katika eneo hilo kufukia mashimo, kusawazisha eneo hilo na kupanda miti ili kuhifadhi mazingira.

Alisema, wafanyakazi hao hawatapata malipo ya muda wa ziada kwa kuwa hakuna uzalishaji kwa sasa, ila baada ya uzalishaji mpya kuanza kwenye eneo jipya ambalo tayari limeishapangwa.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema pia kwamba serikali ina akiba maalum benki inayotokana na mapato ya mgodi huo ambayo iko chini ya Bodi ya Wadhamini wakiongozwa na Gavana wa Benki Kuu (BoT) na kwamba akiba hiyo ndiyo itakayotumika kuwalipa mishahara.

Akijibu maswali ya wafanyakazi hao, Maketa aliwaeleza kuwa serikali itatoa fedha kwa ajili ya eneo lingine jipya la mgodi huo katika eneo hilo la Buhemba, lakini itachukua takriban miezi saba kuanzia sasa.

Kwa mujibu wa DC, mgodi huo umewekeza kiasi cha Sh18 bilioni, ikiwamo mishahara ya wafanyakazi, mitambo na samani zote za ofisi.

Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Migodi, Ujenzi, Nishati na kazi nyinginezo (Tamico) kanda ya ziwa, Stephen Mageta, alisema pamoja na ujumbe mzuri wa DC kwa wafanyakazi hao, lakini wanataka serikali iwahakikishie kwa maandishi kuwa hawatawafukuza kazi na kwamba watalipwa mishahara yao wakati huo wa mpito.

"Wafanyakazi tulikuwa hatuamini kwamba mgodi huu ni mali yetu, sisi tunajua ni mali makaburu kutokana na unyanyasaji, vipigo tunavyopigwa, mishahara midogo na matusi juu," alisema Mwenyekiti wa Tamico tawi la Buhemba, Edward Ng'wenge.

Meneja wa mgodi huo, Jian Duvenage alikataa kuzungumza lolote na waandishi wa habari mgodini hapo na badala yake alimuomba DC aongee naye faragha.

Gazeti hili toleo la Novemba mosi, mwaka huu lilichapisha habari zikimkariri Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, akiutaka mgodi huo, pamoja na mambo mengine waonyeshe ankara zao na takwimu za mrahaba wanaolipa tangu waanze kuchimba dhahabu.

"Endapo BGM itapuuza, agizo hilo litaliwasilisha bungeni na nikishindwa nitakwenda kuwatetea wananchi mahakamani," alisema Mkono ambaye pia ni wakili.
 
Tunasubiri kuona matokeo ya aliyosema Mheshimiwa Mbunge Mkono. Akipeleka hili swala Bungeni atafungwa mdomo na Speaker. Atafute court order ya kutaka apewe nakala ya mkataba unaotumika kuchimba hiyo dhahabu, kiasi kilichopatikana tangu uchimbaji uanze, na kiasi ambacho wananchi wamelipwa.

Yasibakie kuwa maneno tu.

Augustine Moshi
 
Last Week Niliona Matangazo Ya Kazi Mpya Za Barrik Kulikuwa Na Possition Kama 3 Hivi Na Kila Mwezi Kampuni Hiyo Inakuwa Na Position Za Nafasi Kadhaa Za Wafanya Kazi Kuuliza Kwanini ? Watu Wengi Pale Hawakai Sana Inasemekana Wanaenda Kuchuma Na Kuondoka Zao So Kuanzia Tarehe 10 Mwezi Huu Watu Kama 6 Hivi Wameshaacha Kazi Bila Sababu Za Msingi

Hiyo Ndio Barrik Ya Mwanyika
 
Wanabodi,
Samahani nitakurudisheni nyuma kidogo..
Nimesoma mwanzo huyu mnyapala wa kisheria akisema kuwa mwaka 2005 Barricks walilipa fedha kibao kwa serikali yetu na hata kuwa katika hasara!
On the other hand, even with the current incentives, presence of large-scale mines in Tanzania have, in addition to multiplier effect said above, generated revenue to the government and its institution in terms of royalty, import duties, VAT for non-mining items, employment tax for all employees (local and exparts), pension fund. For instance, revenue to government from Bulyanhulu for 2005 amounted to US$30millon while from North Mara it was 11.0 million dollars. While these payments are being made, the mines are still making losses and the shareholders do not expect any return.

Jamani huyu mwanasheria hana habari kuwa Barricks ni Public company na huuza hisa kwa wananchi, hivyo wenye hisa wanapata reports za uzalishaji wake kiasi kwamba huwezi kuweka madai wazi kiasi hicho wakati ni UONGO mkubwa..
Report ya Barricks kwa wenye hisa imesema Barricks ktk mwaka huo 2005 ktk machimbo ya Bulyanhulu walichimba kiasi cha ounce 311,000 kwa gharama ya USd $358 kwa ounce.
Sasa huyu mshirika wetu haya mahesabu yalitolewa anataka kutuambia kuwa Barricks walifanya kuwaongopea wenye hisa zao!
Zaidi ya hapo machimbo ya Mara pekee zilipatikana ounce 250,000 kwa mwaka huohuo. Tulawaka imesifika kwa udogo wake kuwa ina high returns. Buzwagi na Nyanzaga ni sehemu nyingine mpya za Barricks ambazo zinategemea kuanza uzalishaji mwaka huu haya yote ni UONGO?
 
Bado tuna safari ndefu sana ya kumpata kiongozi wa nchi, kwa sasa tuna watawala.

iko siku tutampata kiongozi mzalendo ambaye atakuwa na nguvu ya kusema hapana kwa ufedhuli huu, kiongozi kama Hugo Shavez mwenye mapenzi na nchi na watu wake.

Uvumilivu wa watanzania karibu utafika mwisho, kama mkoloni aliondoka hawa mafethuli wahesabu siku zao.

Nikiangalia mchakato wa uchaguzi wa ccm, napata hofu, wale wapinzani 10 wa urais walikuwa na pesa nyingi sana, walizipata wapi..........
 
Wanabodi,
Samahani nitakurudisheni nyuma kidogo..
Nimesoma mwanzo huyu mnyapala wa kisheria akisema kuwa mwaka 2005 Barricks walilipa fedha kibao kwa serikali yetu na hata kuwa katika hasara!


Jamani huyu mwanasheria hana habari kuwa Barricks ni Public company na huuza hisa kwa wananchi, hivyo wenye hisa wanapata reports za uzalishaji wake kiasi kwamba huwezi kuweka madai wazi kiasi hicho wakati ni UONGO mkubwa..
Report ya Barricks kwa wenye hisa imesema Barricks ktk mwaka huo 2005 ktk machimbo ya Bulyanhulu walichimba kiasi cha ounce 311,000 kwa gharama ya USd $358 kwa ounce.
Sasa huyu mshirika wetu haya mahesabu yalitolewa anataka kutuambia kuwa Barricks walifanya kuwaongopea wenye hisa zao!
Zaidi ya hapo machimbo ya Mara pekee zilipatikana ounce 250,000 kwa mwaka huohuo. Tulawaka imesifika kwa udogo wake kuwa ina high returns. Buzwagi na Nyanzaga ni sehemu nyingine mpya za Barricks ambazo zinategemea kuanza uzalishaji mwaka huu haya yote ni UONGO?

Mkandara,
huyo atakuwa mmoja wa waandishi waliolipiwa nauli na hoteli ya nyota tatu kisha akaanza kuimba sifa hizo bila kujua maana alipokuwa anaandika taarifa yake hiyo tayari alishakunywa wine ambayo hajawahi kunywa maishani mwake. Inasikitisha sana tunapoibiwa na halafu watu wananza kutukashifu kwa habari nyepesi nyepesi hivyo.
 
jamani, mimi nadhani figure its doesn't matter, tuangalie je! sisi tunaweza ku afford hizi gharama za kusimamia na kuchimba madini?

hebu ingia humu na kuijua hii kampuni vizuri:

http://www.alexstewart.com

na kwani hakuna uwezekano wa kuongea na hii kampuni iweze kupunguza kodi?

nadhani ushauri wa mwananchi una nguvu kama una faida zaidi, sioni sababu ya kupiga sana kelele bila ya vigezo vya kielimu
 
Tutaelimishaje jamii na kuelewa utaratibu wa kujua mikataba ya kimataifa na mikataba ya nyumba ya kupanga inasainiwa vipi?

Tunalalamika ajira hakuna Tanzania, ila ajira inapokuja tunaona tunaibiwa, na vilevile, pamoja na kuwa ni ajira umuhimu wa kazi yenyewe na heshima yake inatakiwa kuwa vipi?

Maana kila kitu tunaona tunaibiwa, kila kitu tunaona ni ghali, je! ni nani awezae kufanya biashara na kupenda kupata hasara ama faida ndogo?

Watanzania tujiulize haya, kuliko kukaa mitaani karibu na mitaro michafu huku tukilia kuwa serikali hitujali huku sisi wenyewe ndio wachafuzi wa mitaro hiyo.

Ninapata hasira sana Watanzania wenzangu jamani
 
Mujy,

sina hakika kama umesoma mada hii toka mwanzo au nyengine zifananazo kama IPTL, ATC, NBC etc nadhani ktk haya madini hakuna tofauti sana na hapo ndio JF tunapiga kelele.....anyway later
 
It appears that our government is about to agree with mining companies to maintain the current low royalty rates. The Commissioner of Mines is reported to have recently argued that increasing the royalty rates would scare off miners. He claims that we must charge low rates because we have bad infrastructure, and a largely unskilled labor force.

While the distinguished Commissioner is afraid to scare foreign mining companies, he seems to be quite happy to scare us badly. A 3% royalty rate is extraordinarily scary!

The Commissioner states that some countries are doing away with royalties! Good! We don't want royalties either! We want part ownership of the mines in our country. Royalty rates of 3% for gold, 5% for diamonds and 12.5% for gas are day light robbery.

People who come here, dig big holes in our land and dump huge amounts of toxic mining waste in our rivers should be willing to let us have at least 50% of the profit.

It is better to remain with our gold in the ground than to give it away for a mere 3% of the profit (or of the revenue, whichever is applicable – they hide such truths).

Consider the case of the LIHIR Gold Mine in Papua New Guinea. You can find it here: http://www.lihir.com.pg The mine operator, Rio Tinto, owns 16.3% of it. A Papua New Guinean Company, Mineral Resources PNG Ltd, owns 6.8% of the shares. It holds them in trust on behalf of the people of the island where the mine is (Lihir). The remaining 76.9% of the shares are owned by institutions and the general public.

The infrastructure of Papua New Guinea is much worse than that of Tanzania. They do not have a railway system, and no roads link the capital city with the regional centers. The labor force is much less developed than that of Tanzania. All but one of the mines there have their own power plants, for they are not located anywhere near the national grid.

It is mischievous for the Commissioner of Mines to argue that we must accept royalty rates that are as low as 3% only for gold, because of our poor infrastructure. And, may I ask, why does the Commissioner not address the possibility of part ownership? Why must we only consider a royalty arrangement?

Augustine Moshi
 
Nadhani ni muda muafaka kujua hasa ni wapi tulijikwaa!
Nimeipata hii hapa. Kuna vingi vya kufikirisha kwenye uzi huu .
 
Back
Top Bottom