figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,493
- 54,900
Heshima kwenu wakuu,
Wakili Godfrey Elia John Sabato Wasonga, amewasilisha Maombi Mapya Mahakama kuu ya Dodoma jana jioni akipinga Uchaguzi wa Chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) unaotegemea kufanyika kesho.
Maombi hayo yanaweza kusajiliwa rasmi leo asubuhi hii kwenye Ofisi ya Msajili wa mahakama na Kupewa namba.
Taarifa zaidi zinakuja.
Mahakama kuu ya Dodoma hapo jana iliruhusu Uchaguzi kuendelea baada ya Mapingamizi yaliyowekwa awali kutupiliwa Mbali na Mahakama.
Stay tuned.
=====
UPDATES; 1830hrs:
Kesi namba 15 ya 2017 iliyokuwa imefunguliwa leo mjini Dodoma, na wakili Godfrey Wasonga imetupiliwa mbali na Jaji Kalongora wa mahakama kuu kanda ya Dodoma. Kesi hii ni ya pili kwa wakili Wasonga kutupiliwa mbali baada ya nyingine kutupwa jana.
Wakili Godfrey Elia John Sabato Wasonga, amewasilisha Maombi Mapya Mahakama kuu ya Dodoma jana jioni akipinga Uchaguzi wa Chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) unaotegemea kufanyika kesho.
Maombi hayo yanaweza kusajiliwa rasmi leo asubuhi hii kwenye Ofisi ya Msajili wa mahakama na Kupewa namba.
Taarifa zaidi zinakuja.
Mahakama kuu ya Dodoma hapo jana iliruhusu Uchaguzi kuendelea baada ya Mapingamizi yaliyowekwa awali kutupiliwa Mbali na Mahakama.
Stay tuned.
=====
UPDATES; 1830hrs:
Kesi namba 15 ya 2017 iliyokuwa imefunguliwa leo mjini Dodoma, na wakili Godfrey Wasonga imetupiliwa mbali na Jaji Kalongora wa mahakama kuu kanda ya Dodoma. Kesi hii ni ya pili kwa wakili Wasonga kutupiliwa mbali baada ya nyingine kutupwa jana.