Dodoma: Ajali yaua Watatu akiwemo DAS Handeni

Dodoma: Ajali yaua Watatu akiwemo DAS Handeni

Watu Watatu wamefariki dunia akiwemo Katibu Tawala (DAS) wa wilaya ya Handeni mkoani Tanga Mwalimu Boniface Maiga Jumaa baada ya Gari mbili kugongana mkoani Dodoma usiku wa kuamkia leo.

Ajali hiyo pia imesababisha majeruhi kadhaa akiwemo Mbunge wa Handeni Mhe.Omary Abdallah Kigoda.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Dodoma SACP Gilles Muroto amethibisha.

ITV BreakingNews
View attachment 1503466View attachment 1503467
pole sana Wafiwa na Mungu awape nafuu ya mapema majeruhi.
 
Kufa kufaana, wasure wameanza kuomboleza,moyoni wanapiga jalamba na kumshukuru mungu kichinichini.
 
T
Majanga kama haya sio ya kufanyia mzaha tumieni akili,acheni utoto.
Tatizo yakiwapata nyinyi binadamu ndiyo mnataka na wenzenu waumie kama nyinyi ila yakiwapata mnaowasaka kwa bunduki muwaue huwa mnashangilia.

Mmeshachagua upande wa shetani lazima mkubali na wenzenu washangilie pindi Mungu anapojibu maombi yao.

Utoto uko wapi hapo ?
 
T
Tatizo yakiwapata nyinyi binadamu ndiyo mnataka na wenzenu waumie kama nyinyi ila yakiwapata mnaowasaka kwa bunduki muwaue huwa mnashangilia.

Mmeshachagua upande wa shetani lazima mkubali na wenzenu washangilie pindi Mungu anapojibu maombi yao.

Utoto uko wapi hapo ?
Utoto ni huu upuuzi ulioandika na kupost.
 
Hii gari inaonyesha ni Landrover discovery 3 or 4 automatic alikutana na kitu lazima maana rim na tairi bado nzima
 
Mkuu Owo Mkyalo, tutangulize utu, japo kufa kufaana, lakini kunapotokea kifo cha ghafla cha ajali au majanga, hatua ya kwanza ni compassion na huruma kwa kutoa pole na sio kuwazia fursa za kufa na kufaana, this is inhuman.
P
Alipofariki mzee Mahiga kulitokea nini? Au huo utu na compassion ni kwa baadhi ya watu tu?
 
Back
Top Bottom