DNA za Uganda kuhamia Tanganyika?

tpaul

JF-Expert Member
Feb 3, 2008
21,847
18,253
Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kupepesa macho wala kutikisa masikio. Huko nchini Uganda kimeuma sawasawa. Ndivyo unavyoweza kusema. Mashirika mbalimbali ya habari yakiwemo BBC na DW yameripoti kwamba kasi ya upimaji wa DNA kwa wanandoa wa kiume umepamba moto kwa siku za hivi karibuni na kwamba 56% ya vipimo vimebainisha kwamba watoto waliopimwa sio watoto wa kibaiolojia kwa akina baba wanaowalea.

Jambo hili limekuja baada ya wanaume wa Uganda kushtukia wake zao kuzaa nje ya ndoa na kuwabambika watoto. Wanaharakati wa ndoa na haki za watoto wanalaani upimaji huu na wanatoa wito kwa serikali kusitisha zoezi hili haramu mara moja. Madai yao makubwa ni kuwa wanaopata shida baada ya vipimo ni watoto. Hivyo, wanaomba zoezi hilo lisitishwe haraka iwezekanavyo ili kuokoa ndoa na kuleta utengamano wa kifamilia na kijamii.

Kwa jinsi hali ilivyo, kuna uwezekano wanaume kutoka Tanganyika nao wakaiga mtindo huu wa kupima DNA kwa wingi. Je, huu upimaji ukihamia nchini Tanganyika kutakuwa na usalama? Na, je wewe mwanaume unakubali kulea mtoto wa nje ya ndoa kwa kisingizio kwamba ukipima DNA ndoa itavunjika?

MAONI YANGU

Pamoja na kwamba uchepukaji kwa akina mama na kuzaa nje ya ndoa na kisha kuwachomekea waume zao watoto sio jambo zuri, mimi naona akina mama wanajaribu kubalance mzani kwa kuwa akina baba nao wamekuwa wakitoka nje ya ndoa na wakizaa watoto huwaleta kwenye familia na kukubaliwa na mwanamke bila shurti. Sasa kwanini ndoa ivunjike pale mama anapozaa nje ya ndoa lakini baba akizaa nje ya ndoa huleta mtoto na kuasiliwa na mke wake bila tatizo lolote?

Nawasilisha.
 
hii imenikumbusha kisa cha mzee mmoja jirani yetu, alikuwa na watoto wengi na wake wengi..siku moja akakusanya wanawe wote kwenda kuwapima dna,sijui alikuwa anaandika wosia.. cha ajabu akakuta wote karibia kumi na kitu ni wa kwake kasoro mmoja, mtoto wake wa kwanza (30+yrs) alafu ndio alikuwa wa ujanani.. nilimsifu huyu mzee alimpa milioni kadhaa kama kwaheri akamwambia amtafute mama yake amueleze baba yake ni nani..

mambo ya kupima dNA yamesababishwa na maisha kuwa magumu.. mtu unaweza ukajikuta maisha yamekupiga ukatafuta sababu za kupunguza gharama...
 
Kwanza unatakiwa kujua kwenye ndoa ubepali lazima uwepo ili ndoa idumu, kuna maamuzi ambayo mwanaume sihitaji ushauri wa mke kuyafanya, tukija kwenye hili swala shida kubwa hua inaanzia pale ambapo wanazaa nje alafu Wana kaa kimya unakuja kufahamu baadae Sana, bora aseme mapema kama mna achana muachane mapema Kila mmoja ashike hamsini zake, wanaume hua tuna ujasiri wa kusema ili liwalo na liwe

Tena serikali inge rahisisha hilo zoezi na kupunguza gharama zake ili watu wengi wajue kama Wana kuza wa kwao au wame pigwa za uso
 
Tatizo ni umaskini tu nikiwa nipo wealth sioni sababu ya kuacha kulea watoto ata kama wote sio wangu, ila nikiwi hivi kma nilivyo sasa ivi nitakufukuza kama mbwa .
 
Haya mambo hayakuanza Leo, ndio ukitaka kuchunguza sana unaweza kukuta wewe si mtoto wa Baba yako, au babako sio mtoto wa babake🤣🤣🤣

Ndo wahenga wanasema funika kombe mwanaharamu apite, tatizo siku hizi hatufuniki, na hata ukifunika mwanaharamu analibutua🤣🤣🤣
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom