Dkt. Wilbrod Slaa: Utekaji wote unaondelea nchini ni sheria ya idara ya Usalama wa Taifa ya mwaka 2024

Dkt. Wilbrod Slaa: Utekaji wote unaondelea nchini ni sheria ya idara ya Usalama wa Taifa ya mwaka 2024

Retired

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2016
Posts
50,136
Reaction score
96,161
Anaandika: Dr. Wilbrod Slaa

Msingi wa vitendo vyote vya utekaji unaoendelea nchini ni Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa (TIS) ya mwaka 2024. Bila kurekebisha sheria hii, Watanzania wataendelea kutekwa, kupotezwa na kudhulumiwa hadi tutoweke kabisa kama taifa huru.

Sheria hiyo imeipa TIS mamlaka makubwa ya kukamata watu, lakini bila kuweka utaratibu bayana wa:

(a) Wanapomkamata mtu, wampeleke wapi? Tofauti na Jeshi la Polisi lenye vituo maalumu vya kushikilia watuhumiwa, TIS haina vituo vinavyotambuliwa kisheria vya kuwapokea waliokamatwa.

(b) Hakuna mwongozo wa kisheria unaoeleza nini kifanyike baada ya mtu kukamatwa na TIS. Kwa mfano, Polisi wanapaswa kuhakikisha kuwa ndani ya saa 4 baada ya kumkamata mtu, maelezo (statement) ya mtuhumiwa yanakuwa yamechukuliwa, huku haki za mtuhumiwa zikiwa zimeainishwa wazi katika Sheria na katika taratibu za Police General Orders (PGO). Kwa upande wa TIS, sheria yao haina mwongozo wowote kuhusu haki za waliokamatwa wala hatua zinazofuata baada ya kukamatwa.

(c) Sheria ya TIS imeiruhusu Idara kutumia silaha nzito, pingu na vifaa vingine vya kiusalama, lakini tofauti na Polisi, hakuna mahali sheria inapotamka wazi kuhusu vifaa hivyo vinahifadhiwa wapi, vinatumiwa kwa utaratibu gani, na ni nani anawajibika kuvihifadhi.

Hayo ni baadhi tu ya mapungufu makubwa ya sheria hiyo. Kwa ujumla, sheria hii imeifanya TIS kuwa taasisi isiyoguswa, isiyodhibitiwa na isiyoajibika kwa namna yoyote kwa umma au kwa vyombo vingine vya dola.

Kwa hiyo, kama raia — hususan wasomi — tumeshiriki kimya kimya kuzalisha mazingira haya ya kinyume na utawala wa sheria kwa kukubali kupitishwa kwa sheria hii mbovu bila kupiga kelele. Sasa tunavuna tulichopanda.


My take: TLS Mwabukusi hamuwezi kuipinga hii sheria mahakamani kama Olengurumwa alivyopinga sheria ya kutoshitaki akina Rais na wenzake?
 
Anaandika: Dr. Wilbrod Slaa

Msingi wa vitendo vyote vya utekaji unaoendelea nchini ni Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa (TIS) ya mwaka 2024. Bila kurekebisha sheria hii, Watanzania wataendelea kutekwa, kupotezwa na kudhulumiwa hadi tutoweke kabisa kama taifa huru.

Sheria hiyo imeipa TIS mamlaka makubwa ya kukamata watu, lakini bila kuweka utaratibu bayana wa:

(a) Wanapomkamata mtu, wampeleke wapi? Tofauti na Jeshi la Polisi lenye vituo maalumu vya kushikilia watuhumiwa, TIS haina vituo vinavyotambuliwa kisheria vya kuwapokea waliokamatwa.

(b) Hakuna mwongozo wa kisheria unaoeleza nini kifanyike baada ya mtu kukamatwa na TIS. Kwa mfano, Polisi wanapaswa kuhakikisha kuwa ndani ya saa 4 baada ya kumkamata mtu, maelezo (statement) ya mtuhumiwa yanakuwa yamechukuliwa, huku haki za mtuhumiwa zikiwa zimeainishwa wazi katika Sheria na katika taratibu za Police General Orders (PGO). Kwa upande wa TIS, sheria yao haina mwongozo wowote kuhusu haki za waliokamatwa wala hatua zinazofuata baada ya kukamatwa.

(c) Sheria ya TIS imeiruhusu Idara kutumia silaha nzito, pingu na vifaa vingine vya kiusalama, lakini tofauti na Polisi, hakuna mahali sheria inapotamka wazi kuhusu vifaa hivyo vinahifadhiwa wapi, vinatumiwa kwa utaratibu gani, na ni nani anawajibika kuvihifadhi.

Hayo ni baadhi tu ya mapungufu makubwa ya sheria hiyo. Kwa ujumla, sheria hii imeifanya TIS kuwa taasisi isiyoguswa, isiyodhibitiwa na isiyoajibika kwa namna yoyote kwa umma au kwa vyombo vingine vya dola.

Kwa hiyo, kama raia — hususan wasomi — tumeshiriki kimya kimya kuzalisha mazingira haya ya kinyume na utawala wa sheria kwa kukubali kupitishwa kwa sheria hii mbovu bila kupiga kelele. Sasa tunavuna tulichopanda.
Alie allow haya mnamfaham na alikuwa ana nia njema but hakufikiria mbali madhara yake

Kaondoka kaacha balaa
 
I guess was magufuli, nia njema ipi? fafanua
He wants flexibility kudeal na watu wanaoitafuna system, kwenye macho yake idara ilikuwa imefungwa mikono, incapable of doing anything, so hiyo sheria ilitungww to free them ili aweze kuwatumia for whatever reason

Some of seniour ccm member didnt like this, maana after this sheria mambo yao yakawa yanavujishwa kwa mkuu.
Too bad hakujua watu anao waachia watafanya kazi gani na hii sheria
 
Anaandika: Dr. Wilbrod Slaa

Msingi wa vitendo vyote vya utekaji unaoendelea nchini ni Sheria ya Idara ya Usalama wa Taifa (TIS) ya mwaka 2024. Bila kurekebisha sheria hii, Watanzania wataendelea kutekwa, kupotezwa na kudhulumiwa hadi tutoweke kabisa kama taifa huru.

Sheria hiyo imeipa TIS mamlaka makubwa ya kukamata watu, lakini bila kuweka utaratibu bayana wa:

(a) Wanapomkamata mtu, wampeleke wapi? Tofauti na Jeshi la Polisi lenye vituo maalumu vya kushikilia watuhumiwa, TIS haina vituo vinavyotambuliwa kisheria vya kuwapokea waliokamatwa.

(b) Hakuna mwongozo wa kisheria unaoeleza nini kifanyike baada ya mtu kukamatwa na TIS. Kwa mfano, Polisi wanapaswa kuhakikisha kuwa ndani ya saa 4 baada ya kumkamata mtu, maelezo (statement) ya mtuhumiwa yanakuwa yamechukuliwa, huku haki za mtuhumiwa zikiwa zimeainishwa wazi katika Sheria na katika taratibu za Police General Orders (PGO). Kwa upande wa TIS, sheria yao haina mwongozo wowote kuhusu haki za waliokamatwa wala hatua zinazofuata baada ya kukamatwa.

(c) Sheria ya TIS imeiruhusu Idara kutumia silaha nzito, pingu na vifaa vingine vya kiusalama, lakini tofauti na Polisi, hakuna mahali sheria inapotamka wazi kuhusu vifaa hivyo vinahifadhiwa wapi, vinatumiwa kwa utaratibu gani, na ni nani anawajibika kuvihifadhi.

Hayo ni baadhi tu ya mapungufu makubwa ya sheria hiyo. Kwa ujumla, sheria hii imeifanya TIS kuwa taasisi isiyoguswa, isiyodhibitiwa na isiyoajibika kwa namna yoyote kwa umma au kwa vyombo vingine vya dola.

Kwa hiyo, kama raia — hususan wasomi — tumeshiriki kimya kimya kuzalisha mazingira haya ya kinyume na utawala wa sheria kwa kukubali kupitishwa kwa sheria hii mbovu bila kupiga kelele. Sasa tunavuna tulichopanda.


My take: TLS Mwabukusi hamuwezi kuipinga hii sheria mahakamani kama Olengurumwa alivyopinga sheria ya kutoshitaki akina Rais na wenzake?
Hii Sheria Ilipokuwa inapitishwa watu walikuwa Busy na Mambo Mengine.TISS sasa hivi wanaweza kufanya Chochote,Popote na hakuna Yeyote anayeweza kuwafanya Lolote.Hata Rais Samia haweza kuwafanya Lolote.Kiufupi TISS ni kundi la Kigaidi dhidi ya Watanzania
 
He wants flexibility kudeal na watu wanaoitafuna system, kwenye macho yake idara ilikuwa imefungwa mikono, incapable of doing anything, so hiyo sheria ilitungww to free them ili aweze kuwatumia for whatever reason

Some of seniour ccm member didnt like this, maana after this sheria mambo yao yakawa yanavujishwa kwa mkuu.
Too bad hakujua watu anao waachia watafanya kazi gani na hii sheria
Duh! Magufuli sijui aliwafanya nini baadhi ya watanzania.
Me naona kama yeye ndie aliwatumia hao Tiss vibaya, hasa kuwa expose pengine kuliko sasa hivi.

Usalama wa Taifa unafaa kulifanyia kazi Taifa sio kiongozi. Iweje mwanasiasa ambae amegeuka remote control ya Usalama wa taifa aonekane alichofanya alikuwa sahihi?
 
Dkt Slaa amemshukia Samia kusaini sheria inayowapa Usalama wa Taifa Kinga bila kuzingatia madhara yake kwa umma katika utekelezaji wa sheria hiyo.

Ameyasema hayo kupitia jukwaa la Sauti ya Watanzania alipokuwa anazungumzia hali ya nchi kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Sikiliza video kwenye link upate undani wa alichokizungumza


View: https://youtu.be/LthDMIBnZEQ?si=rL6ng2HpU5-tmDCA
 
Kipindi cha shujaa Mzee alikuwa balozi na alipoulizwa suala la utekaji sijui alijibuje vile nimesahau.
Hata alipoulizwa kutoa comment kwenye kesi ya ugaidi ya Mbowe sijui alijibuje vile.

Safarini Khartoum Sudani.
 
Kipindi cha shujaa Mzee alikuwa balozi na alipoulizwa suala la utekaji sijui alijibuje vile nimesahau.
Hata alipoulizwa kutoa comment kwenye kesi ya ugaidi ya Mbowe sijui alijibuje vile.

Safarini Khartoum Sudani.
Alijibu kuwa HAKUBALIANI na matendo OVU ya utekaji.Huyu mzee ni mzalendo sana na Huwa hapepesi macho kwenye mambo ya kihuni kama yale yanayopingwa na hamphrey polepole
 
Back
Top Bottom