Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,264
- 9,715
Ndugu zangu watanzania,
Haijapata kutokea ,haijapata kuonekana kwa mapokezi makubwa aliyoyapata mh Dkt Tulia Acksoni Mwansasu mbunge wa Mbeya mjini,speaker wa Bunge na Rais wa umoja wa mabunge Duniani ni mapokezi ya kishindo,ni mapokezi ya karne,ni mapokezi ya kihistoria ni mapokezi yaliyovunja rekodi,ni mapokezi yaliyoitetemesha na kulisimamisha Jiji la mbeya.watu wamehudhuria haijapata kutokea,mafuriko ya watu wamemiminika haijapata kuonekana.
Kwa hakika Dr Tulia ni mpango wa Mungu mwenyewe,anapendwa na kuheshimika na wanambeya ni haijapata kutokea ,anakubalika na kuungwa mkono ni haijapata kushuhudiwa ,itachukuwa miaka mingi sana kwa kiongozi yeyote yule kupata mapokezi aliyoyapata leo hii Dr Tulia.mtoto wa Mbeya kapokelewa kishujaa Mithili ya wanajeshi waliotoka vitani na kurejea na ushindi wa kukomboa ardhi ya nchi na Taifa lao iliyokuwa imeporwa.
Kapokelewa na watu wa rika zote na makundi yote kuanzia viongozi wa dini, serikali,mila,vijana,akina mama,wazee n.k.kishindo chake kimeteka jiji la Mbeya, kwa hakika ujio wake tokea angani aliko kuwa akiingia na ndege ya jeshi kumefanya jiji lote kulipuka kwa shangwe, nderemo na vifijo ambayo haijawahi kutokea.
Rai yangu kwa upinzani na mtu yeyote yule asithubutu kuchukua Fomu ya ubunge kugombea ubunge jimbo la Mbeya mjini maana kwa hali iliyopo kwa sasa na kwa namna Dkt. Tulia anavyopendwa na kukubalika kwa hakika itakuwa ni kupoteza muda na fedha kushindana na Rais wa IPU Dkt. Tulia Acksoni mwansasu katika sanduku la kura.
Dr Tulia siyo mtu wa kawaida ,ana nguvu fulani ndani yake isiyo ya kawaida na ya ajabu sana yenye kuonyesha uwepo wa Mungu ndani yake hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa Dr Tulia ni mcha Mungu mkubwa na mwenye kumtegemea na kumtumainia Mungu kwa kila jambo.upepo wa Dr Tulia ni mkali na wenye mvumo wa kipekee sana,ni mtu mwenye ushawishi wa hali ya juu sana. Kwa hakika kaiteka mioyo ya wana Mbeya na kutembea mioyoni mwao.
Ni faraja kwa wana Mbeya ni fahari kwa wana nyanda za juu kusini na ni Nembo kwa wana mbeya. ameuheshimisha mkoa ,amelipa hadhi jiji,amewafanya wana Mbeya watembee kifua mbele na kwa kujiamini .na kila mtu anaona anastahili kuringa na kujivunia Dr Tulia kwa kuwa ni Mbeya ndio iliyompeleka Bungeni Dr Tulia na ni Mbeya ndio iliyotoa Rais wa umoja wa mabunge Duniani kati ya nchi zaidi ya 180 wanachama wa IPU Duniani kwote.
ndio maana wana Mbeya wamefanya mapokezi ya kishindo na ya heshima kubwa sana kumpatia mtoto wao na dada yao na mbunge wao Dkt Tulia Acksoni mwansasu kwa ushindi na heshima ya kipekee aliyolipatia jiji la Mbeya.kila mmoja anajiona kuwa kupitia kura yake ya ndio kwa Dkt Tulia Taifa limepata heshima ya kutoa Rais wa IPU na mwanamke wa kwanza kutoka Barani Afrika kushinda na kushika urais wa IPU.
Kazi iendelee mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Haijapata kutokea ,haijapata kuonekana kwa mapokezi makubwa aliyoyapata mh Dkt Tulia Acksoni Mwansasu mbunge wa Mbeya mjini,speaker wa Bunge na Rais wa umoja wa mabunge Duniani ni mapokezi ya kishindo,ni mapokezi ya karne,ni mapokezi ya kihistoria ni mapokezi yaliyovunja rekodi,ni mapokezi yaliyoitetemesha na kulisimamisha Jiji la mbeya.watu wamehudhuria haijapata kutokea,mafuriko ya watu wamemiminika haijapata kuonekana.
Kwa hakika Dr Tulia ni mpango wa Mungu mwenyewe,anapendwa na kuheshimika na wanambeya ni haijapata kutokea ,anakubalika na kuungwa mkono ni haijapata kushuhudiwa ,itachukuwa miaka mingi sana kwa kiongozi yeyote yule kupata mapokezi aliyoyapata leo hii Dr Tulia.mtoto wa Mbeya kapokelewa kishujaa Mithili ya wanajeshi waliotoka vitani na kurejea na ushindi wa kukomboa ardhi ya nchi na Taifa lao iliyokuwa imeporwa.
Kapokelewa na watu wa rika zote na makundi yote kuanzia viongozi wa dini, serikali,mila,vijana,akina mama,wazee n.k.kishindo chake kimeteka jiji la Mbeya, kwa hakika ujio wake tokea angani aliko kuwa akiingia na ndege ya jeshi kumefanya jiji lote kulipuka kwa shangwe, nderemo na vifijo ambayo haijawahi kutokea.
Rai yangu kwa upinzani na mtu yeyote yule asithubutu kuchukua Fomu ya ubunge kugombea ubunge jimbo la Mbeya mjini maana kwa hali iliyopo kwa sasa na kwa namna Dkt. Tulia anavyopendwa na kukubalika kwa hakika itakuwa ni kupoteza muda na fedha kushindana na Rais wa IPU Dkt. Tulia Acksoni mwansasu katika sanduku la kura.
Dr Tulia siyo mtu wa kawaida ,ana nguvu fulani ndani yake isiyo ya kawaida na ya ajabu sana yenye kuonyesha uwepo wa Mungu ndani yake hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa Dr Tulia ni mcha Mungu mkubwa na mwenye kumtegemea na kumtumainia Mungu kwa kila jambo.upepo wa Dr Tulia ni mkali na wenye mvumo wa kipekee sana,ni mtu mwenye ushawishi wa hali ya juu sana. Kwa hakika kaiteka mioyo ya wana Mbeya na kutembea mioyoni mwao.
Ni faraja kwa wana Mbeya ni fahari kwa wana nyanda za juu kusini na ni Nembo kwa wana mbeya. ameuheshimisha mkoa ,amelipa hadhi jiji,amewafanya wana Mbeya watembee kifua mbele na kwa kujiamini .na kila mtu anaona anastahili kuringa na kujivunia Dr Tulia kwa kuwa ni Mbeya ndio iliyompeleka Bungeni Dr Tulia na ni Mbeya ndio iliyotoa Rais wa umoja wa mabunge Duniani kati ya nchi zaidi ya 180 wanachama wa IPU Duniani kwote.
ndio maana wana Mbeya wamefanya mapokezi ya kishindo na ya heshima kubwa sana kumpatia mtoto wao na dada yao na mbunge wao Dkt Tulia Acksoni mwansasu kwa ushindi na heshima ya kipekee aliyolipatia jiji la Mbeya.kila mmoja anajiona kuwa kupitia kura yake ya ndio kwa Dkt Tulia Taifa limepata heshima ya kutoa Rais wa IPU na mwanamke wa kwanza kutoka Barani Afrika kushinda na kushika urais wa IPU.
Kazi iendelee mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.