Dkt. Tulia Ackson alilenga nini kupotosha kuwa mhimili mmoja ni mkubwa kuliko miingine? Alijikosha, alijipendekeza?

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Kila nikijaribu kukumbuka na kutafakari zaidi kuhusu kauli za huyu Mama alizozitoa mbele ya Rais wa JMT kuwa mihimili yote haiko sawa, kwamba mhimili wa dola ni mkubwa zaidi kuliko miingine. Hii kauli binafsi naichukulia kua ni ya kujikosha na kujipendekeza, si kauli ya kutamka kwenye media mbele ya macho ya umma.

Spika wa aina ya Dkt Tulia hata kama kuna jambo linalohatarisha ustawi wa taifa ikatokea likafanywa na serikali ataangalia tu wala hatofanya uamuzi wowote kwa vile dola ndio mhimili mkuu? Maana Dola siyo Mungu wala malaika kwamba haikosi.

Tunatambua kua kwa katiba yetu hii iliyopo dola ndiyo kila kitu lakini usiifanye mihimili miingine kutokujiamulia mambo yake ya uhuru, lakini kila mhimili una mipaka ya majukumu yake huru bila kuingiliwa na mwingine. Huyu alimaamisha kwamba Ndungai alikosea kwa kauli zake? Alikuwa anamaanisha kua mhimili wa bunge si lolote wala chochote?

Tukiwa na bunge chini Spika aina ya Dkt Tulia ni hatari sana kwa ustawi wa taifa na kwa maslahi vya taifa. Niwashauri wanaccm wenzangu, hata kama kuna wakati tunatakiwa kulinda maslahi vya chama lakini Dkt Tulia hafai kabisa . Huyu mwanamama anataka kulitia bunge Kibogoyo liwe kama mihuri wa gogongea kupitisha hoja za serikali hata kama hazifai.

Hawa ndio wasomi wetu, wapo radhi kupotosha ili kulinda maslahi yao binafsi.Haijalishi wewe ni CCM au upinzani, tafadhali kemea watu wa aina hii kwa maslahi ya taifa letu. Tuachane na watu aina ya Tulia hawatufai.
 
Bunge - Kutunga Sheria
Mahakama - Kutafsiri hizi sheria
Serikali - Kutekeleza kwa mujibu wa sheria na kanuni
Rais msimamizi mkuu wa hayo yote...
 
Kajitathmini kagundua yeye ni zao la mwendazake. Wenzake wengi wenye rangi rangi kama zake washapigwa mitama na tanganyika jeki nyingi.
Yupo jahazini na jahazi limetoboka, anachofanya ni kushika chochote ilimradi aokoe “uhai” wake😃😃
 
Kuna HATARI kubwa Sana kwa BUNGE kumchagua mtu anayeamini kuwa Rais ni "MKUU" wa Mihimili yote ya DOLA.

Bunge na Rais wote Wana NGUVU sawa. Rais anaweza KULIVUNJA Bunge na Bunge linaweza KUMUONDOA Rais MADARAKANI.

Kwenye hii video hapa chini Tulia anajaribu kuwapotosha Watanzania kuwa mhimili wa urais ni mkubwa kuliko mihimili mingine kitu ambacho siyo sahihi.


Tulia anajua ukweli ila anachojaribu kufanya ni "kumhonga" Rais kwa kumuonyesha kuwa atajisalimisha kwake(Submission) ili achaguliwe kuwa Speaker wa Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani anajua kuwa hapa Tanzania Rais ana influence kubwa katika uchaguzi wa Speaker wa Bunge.

Unaweza kujionea mwenyewe jinsi tulivyo na katiba mbovu.Imagine anaechagua Speaker wa Bunge ni Rais na wala siyo Bunge na ndiyo maana Tulia ameanza kujipendekeza kwa Rais mapema ili apate nafasi hiyo.

Taifa haliwezi kuendelea kwa mihimili ya nchi kumwabudu na kumtumikia Rais.Tunahitaji katiba ambayo itaipa mihimili separation of power.

Anachojaribu kufanya Tulia ni kuuza mhimili wa Bunge ili tu asikose tonge na ndiyo maana hata alichukua form za kugombea usipika bila ya kujiuzulu kwanza unaibu speaker kitu ambacho ni kinyume na katiba yetu.Alifanya hivyo ili akikosa usipika basi aendelee kuwa naibu speaker.Ni mambo ya kupigania tonge.

Watu wa namna hii ambao wanatanguliza maslahi yao binafsi mbele badala ya kutanguliza maslahi ya Taifa mbele ni hatari sana kwa Taifa letu na ndiyo wamefanya nchi hii isiweze kufanya lolote la maana ndani ya miaka 60 ya uhuru.
 
Tuweke siasa pembeni....

Kimamlaka ya utekelezaji wa shughuli za nchi , MIHIMILI YOTE IPO SAWA!! Hakuna Mhimili mmoja uliomzidi mwenzake kwa sababu kila Mhimili, umepewa shughuli yake!

Na hicho ambacho tumezoea kuita Mihimili kipo kwenye Ibara ya 4 ambayo inataja VYOMBO 3 vyenye MAMLAKA YA KUTEKELEZA SHUGHULI ZA NCHI, na vyombo hivyo ni:-

1. Serikali,
2. Bunge, na
3. Mahakama.

Serikali ambayo kiongozi wake ni Rais imepewa MAMLAKA YA UTENDAJI, Bunge limepewa MAMLAKA ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma, huku Mahakama ikipewa MAMLAKA ya kutekeleza utoaji haki.

Sasa katika utekelezaji wa hay mamlaka, hivyo VYOMBO 3 VINATAKIWA kuwa huru!

Kwamba, serikali hata kama wewe ndo hazinamwenye pesa zote , majeshi na kila kitu bado MAMLAKA yako yanabaki kwenye UTENDAJI TU! Hata kama Ikulu yote imejaa wanasheria lakini bado haiwezi kusema wanataka kutunga sheria za kuendesha nchi wao wenyewe kwa sababu ni Bunge ndio imepewa Mamlaka!

Bunge nalo hata kama Wabunge WOTE wawe wanasheria waliobobea lakini bado hawawezi kusema kwavile sheria wanatunga wao basi hata suala la utoaji haki itabidi litekelezwe na bunge kwa sababu waliopewa MAMLAKA ya utoaji haki ni Mahakama!!

Kwahiyo tunaposema Mihimili yote ipo sawa maaana yake ni USAWA KATIKA UTEKELEZAJI WA MAMLAKA walizopewa kwa mujibu wa katiba!

Tatizo linakuja pale watu wanapojaribu kuaminisha hiyo the so-called MHIMILI ni sawa katika mazingira mbalimbali bila kujua usawa unaosemwa ni wa kwenye kutekeleza mamlaka waliyopewa na Ibara ya 4. Na usawa huo ni kwa Mhimili mmoja kutoingiliwa na mwingine

Generally, Ibara ya 33 (2) inasema:-
Rais atakuwa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.
REMEMBER... hapo juu, yaani Serikali, Bunge na Mahakama ni VYOMBO TU VILIVYOPEWA MAMLAKA YA KUTEKELEZA SHUGHULI ZA NCHI lakini Rais ndie MKUU WA NCHI!
 
Wabunge hao hawapo mule ndani
Kuna HATARI kubwa Sana kwa BUNGE kumchagua mtu anayeamini kuwa Rais ni "MKUU" wa Mihimili yote ya DOLA.

Bunge na Rais wote Wana NGUVU sawa. Rais anaweza KULIVUNJA Bunge na Bunge linaweza KUMUONDOA Rais MADARAKANI.

Kwenye hii video hapa chini Tulia anajaribu kuwapotosha Watanzania kuwa mhimili wa urais ni mkubwa kuliko mihimili mingine kitu ambacho siyo sahihi.View attachment 2084890

Tulia anajua ukweli ila anachojaribu kufanya ni "kumhonga" Rais kwa kumuonyesha kuwa atajisalimisha kwake(Submission) ili achaguliwe kuwa Speaker wa Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani anajua kuwa hapa Tanzania Rais ana influence kubwa katika uchaguzi wa Speaker wa Bunge.

Unaweza kujionea mwenyewe jinsi tulivyo na katiba mbovu.Imagine anaechagua Speaker wa Bunge ni Rais na wala siyo Bunge na ndiyo maana Tulia ameanza kujipendekeza kwa Rais mapema ili apate nafasi hiyo.

Taifa haliwezi kuendelea kwa mihimili ya nchi kumwabudu na kumtumikia Rais.Tunahitaji katiba ambayo itaipa mihimili separation of power.

Anachojaribu kufanya Tulia ni kuuza mhimili wa Bunge ili tu asikose tonge na ndiyo maana hata alichukua form za kugombea usipika bila ya kujiuzulu kwanza unaibu speaker kitu ambacho ni kinyume na katiba yetu.Alifanya hivyo ili akikosa usipika basi aendelee kuwa naibu speaker.Ni mambo ya kupigania tonge.

Watu wa namna hii ambao wanatanguliza maslahi yao binafsi mbele badala ya kutanguliza maslahi ya Taifa mbele ni hatari sana kwa Taifa letu na ndiyo wamefanya nchi hii isiweze kufanya lolote la maana ndani ya miaka 60 ya uhuru.View attachment 2084900

Wabunge CHAGUENI mtu ANAYEJUA MAMLAKA ya BUNGE.
 
Kila nikijaribu kukumbuka na kutafakari zaidi kuhusu kauli za huyu Mama alizozitoa mbele ya Rais wa JMT kuwa mihimili yote haiko sawa, kwamba mhimili wa dola ni mkubwa zaidi kuliko miingine. Hii kauli binafsi naichukulia kua ni ya kujikosha na kujipendekeza, si kauli ya kutamka kwenye media mbele ya macho ya umma.

Spika wa aina ya Dkt Tulia hata kama kuna jambo linalohatarisha ustawi wa taifa ikatokea likafanywa na serikali ataangalia tu wala hatofanya uamuzi wowote kwa vile dola ndio mhimili mkuu? Maana Dola siyo Mungu wala malaika kwamba haikosi.

Tunatambua kua kwa katiba yetu hii iliyopo dola ndiyo kila kitu lakini usiifanye mihimili miingine kutokujiamulia mambo yake ya uhuru, lakini kila mhimili una mipaka ya majukumu yake huru bila kuingiliwa na mwingine. Huyu alimaamisha kwamba Ndungai alikosea kwa kauli zake? Alikuwa anamaanisha kua mhimili wa bunge si lolote wala chochote?

Tukiwa na bunge chini Spika aina ya Dkt Tulia ni hatari sana kwa ustawi wa taifa na kwa maslahi vya taifa. Niwashauri wanaccm wenzangu, hata kama kuna wakati tunatakiwa kulinda maslahi vya chama lakini Dkt Tulia hafai kabisa . Huyu mwanamama anataka kulitia bunge Kibogoyo liwe kama mihuri wa gogongea kupitisha hoja za serikali hata kama hazifai.

Hawa ndio wasomi wetu, wapo radhi kupotosha ili kulinda maslahi yao binafsi.Haijalishi wewe ni CCM au upinzani, tafadhali kemea watu wa aina hii kwa maslahi ya taifa letu. Tuachane na watu aina ya Tulia hawatufai.
Kujipendekeza, uzandiki na unafiki ndio sifa ya CCM
 
Kila nikijaribu kukumbuka na kutafakari zaidi kuhusu kauli za huyu Mama alizozitoa mbele ya Rais wa JMT kuwa mihimili yote haiko sawa, kwamba mhimili wa dola ni mkubwa zaidi kuliko miingine. Hii kauli binafsi naichukulia kua ni ya kujikosha na kujipendekeza, si kauli ya kutamka kwenye media mbele ya macho ya umma.

Spika wa aina ya Dkt Tulia hata kama kuna jambo linalohatarisha ustawi wa taifa ikatokea likafanywa na serikali ataangalia tu wala hatofanya uamuzi wowote kwa vile dola ndio mhimili mkuu? Maana Dola siyo Mungu wala malaika kwamba haikosi.

Tunatambua kua kwa katiba yetu hii iliyopo dola ndiyo kila kitu lakini usiifanye mihimili miingine kutokujiamulia mambo yake ya uhuru, lakini kila mhimili una mipaka ya majukumu yake huru bila kuingiliwa na mwingine. Huyu alimaamisha kwamba Ndungai alikosea kwa kauli zake? Alikuwa anamaanisha kua mhimili wa bunge si lolote wala chochote?

Tukiwa na bunge chini Spika aina ya Dkt Tulia ni hatari sana kwa ustawi wa taifa na kwa maslahi vya taifa. Niwashauri wanaccm wenzangu, hata kama kuna wakati tunatakiwa kulinda maslahi vya chama lakini Dkt Tulia hafai kabisa . Huyu mwanamama anataka kulitia bunge Kibogoyo liwe kama mihuri wa gogongea kupitisha hoja za serikali hata kama hazifai.

Hawa ndio wasomi wetu, wapo radhi kupotosha ili kulinda maslahi yao binafsi.Haijalishi wewe ni CCM au upinzani, tafadhali kemea watu wa aina hii kwa maslahi ya taifa letu. Tuachane na watu aina ya Tulia hawatufai.
Tulia alikuwa anaongea legally na administatively.

Nchi ina dola ambayo ina mihimili mitatu, executive ambayo inatoa mkuu wa nchi, amri jeshi mkuu na kiongozi wa serikali. Huyu ana mandate ya kukusanya kodi na kuwagawia mahakama ili wajiendeshe, kuwagawi bunge ili wajiendeshe.

JPM aliwahi kumjibu Paskali Mayalla kuwa, kuna mhimili "ulijichimbia chini zaidi".

Rais kama mkuu wa nchi, picha yake inakaa mahakamani kwa nafasi ya ukuu wa nchi. Rais picha yake iko bungeni kwa nafasi ya ukuu wa nchi. Lakini hakuna picha ya spika mahakamani, wala hakuna picha ya jaji mkuu bungeni au ofisi yoyote ya serikali.

Pengine siku tukipata katiba mpya kama tunataka, tuwe na mfumo kama Israel, Uingereza au Ujerumani. Rais awe mkuu wa nchi ceremonious ila tuwe na waziri mkuu ambae atakuwa ni kiongozi wa serikali na CinC ambae bado nafasi yake ya kukusanya kodi na mahakama na bunge kuleta "bakuli"' bado kunamfanya kiongozi wa serikali kuwa na uzito sana ukilinganisha na wenzie kwenye judiciary na legislature.

Kwa umasikini ulio nchini na fursa zilizo nchini, tungekuwa na think tank ya nini tufanye walau nchi yetu iongeze export earnings izalishe ajira ipuze imports kwa kukuza uwekezaji nchini.

Haya tunayoyajadili, hao wakuu wa bunge, serikali na mahakama, posho zao za ustaafu zimenona kweli. Ni lini walala hoi nao wataona fursa ya kuzalisha wakauza kwa bei nzuri kwa soko linaloeleweka na bei nzuri ili hata wakitaka nao kusomesha watoto wao Feza wawe na financial muscles.

J3 njema.
 
Kuna HATARI kubwa Sana kwa BUNGE kumchagua mtu anayeamini kuwa Rais ni "MKUU" wa Mihimili yote ya DOLA.

Bunge na Rais wote Wana NGUVU sawa. Rais anaweza KULIVUNJA Bunge na Bunge linaweza KUMUONDOA Rais MADARAKANI.

Kwenye hii video hapa chini Tulia anajaribu kuwapotosha Watanzania kuwa mhimili wa urais ni mkubwa kuliko mihimili mingine kitu ambacho siyo sahihi.


Tulia anajua ukweli ila anachojaribu kufanya ni "kumhonga" Rais kwa kumuonyesha kuwa atajisalimisha kwake(Submission) ili achaguliwe kuwa Speaker wa Bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani anajua kuwa hapa Tanzania Rais ana influence kubwa katika uchaguzi wa Speaker wa Bunge.

Unaweza kujionea mwenyewe jinsi tulivyo na katiba mbovu.Imagine anaechagua Speaker wa Bunge ni Rais na wala siyo Bunge na ndiyo maana Tulia ameanza kujipendekeza kwa Rais mapema ili apate nafasi hiyo.

Taifa haliwezi kuendelea kwa mihimili ya nchi kumwabudu na kumtumikia Rais.Tunahitaji katiba ambayo itaipa mihimili separation of power.

Anachojaribu kufanya Tulia ni kuuza mhimili wa Bunge ili tu asikose tonge na ndiyo maana hata alichukua form za kugombea usipika bila ya kujiuzulu kwanza unaibu speaker kitu ambacho ni kinyume na katiba yetu.Alifanya hivyo ili akikosa usipika basi aendelee kuwa naibu speaker.Ni mambo ya kupigania tonge.

Watu wa namna hii ambao wanatanguliza maslahi yao binafsi mbele badala ya kutanguliza maslahi ya Taifa mbele ni hatari sana kwa Taifa letu na ndiyo wamefanya nchi hii isiweze kufanya lolote la maana ndani ya miaka 60 ya uhuru.View attachment 2084900
Tatizo wanaolihitaji katiba hawajitokezi wazi. Wameishia kuwatanguliza Cdm . Huku wao unafiki ukiwasumbua
 
Back
Top Bottom