Mpinzire
JF-Expert Member
- Jan 18, 2013
- 7,220
- 12,939
Hoja ya kwanza kwamba aliwataka wanachama wa Chadema wakae kimya kusema wakae kimya ni kweli maana Issue iliyopo Mahakama kiutaratibu hatupaswi kuitolea majibu mpaka mahakama itoe hukumu ili Dkt hakukosea ila ndo utaratibu wa ulivyo Duniani.Tangu astaafu ubalozi na kurudi nchini Dr Slaa amekuwa akitoa kauli zenye utata ambazo mwishoni humrudia yeye mwenyewe.
1. Kwanza, Dr Slaa aliwaataka wafuasi na wanachama wa wachadema wakae kimya na kuacha kudai kuwa Mbowe sio gaidi na hana hatia. Nadhani akilini mwa Dr Slaa alijua lazima Mbowe atatiwa hatiani. Cha kushangaza DPP anafuta mashtaka yote kwa Mh Mbowe na Wenzake.
Aibu ikamwangukia Dr Slaa kwa kudandia kesi asiyoijua imetokea wapi.
2. Pili, Juzi Dr Slaa kasema Ripoti ya CAG imepotoshwa, kwa maana ikishafikishwa mbele ya bunge haitakiwi kuwa public document. Kumbe sheria ilifanyiwa marekebishi na Sasa Report ya CAG ikiwekwa mbele ya bunge inakuwa ni Mali ya Umma. Hivyo jamii inaruhusiwa kuijadili.
Aibu ikamwangukia Dr Slaa kaishia kuomba radhi kuwa amekosea na alipitiwa alidhani sheria ya mwaka 2009 bado inatumika.
3. Jambo la tatu Dr Slaa amedai kwamba Kuna uwezekano ya kwamba CHADEMA ndio wanahusika na kumlima risasi Lissu na akatumia issue ya huko nyuma kutetea hoja yake bila kujua ukweli wa Jambo. Juzi wamelumbana na heche kwenye club house na kuishia kusema amenukuliwa vibaya hakumaanisha hivyo.kwa bahati nzuri CHADEMA bado wanheshimu mzee, wangeweza kumfungulia kesi ya ya madai.
Hivyo walio karibu na Dr Slaa wamshauri ya kwamba alidai amestaafu siasa basi aendelee kustaafu, maana Ni Kama amerudi kwenye siasa.
Pia ajifunze kutoka kwa akina Musiba waliotoa kauli wasizo kuwa na uhakika nazo leo zimewafunga wamejificha hata Uhuru wa kuongea hawana.
Dkt Slaa wala hakuwazia kama Mbowe angefungwa na wala hakuweka percent kuwa DPP asingeweza kufuta kesi ila tukiweka maneno mengi pembeni DPP kafuta sio kwa maamuzi yake ila kwa Kauli kutoka kwa Mh Rais, kwa bahati mbaya ili hatulioni kama tatizo la Muhimili wa Serikali kuingilia mihimili mingine kwasababu ili limetugusa sisi. Ila kitendo cha Mahakama kusema Mbowe kakutwa na kesi ya kujibu alafu DPP siku ya pili anakuja hana nia ya kuendelea na kesi ilikuwa udhaifu mkubwa wa mihimili yetu!
Angalau wangeiwahi pale Mahakama iseme kuwa hawajamkuta Mbowe na kesi ya kujibu ikaishia hapo! Lakini kwakuwa ili linatufurahisha sisi acha lipite, tumefunika kombe mwanaharamu apite.
Kuhusu Tundu Lissu kupigwa risasi ilo ata Tundu Lissu aliwahi kusema kama ata Mbowe alihusika vyombo vya usalama vikibaini vimkamate tu! Tukio la Lissu tumeliweka kisiasa kwakuwa tu mwenyewe ni mwanasiasa nayeye akalibeba kisiasa lakini tu shambulio la Lissu usije kusema Chadema hawahusiki! Ila si Chama ila kuna viongozi ndani ya chama chenu wanalijua vema na ndiyo walilipanga shambulio lile na ndiyo maana Lissu anashindwa kurudi sababu tena sio Magufuli ila mwenyewe anajua hajui kwasasa rafiki yake ni nani wala adui yake ni nani!
Sent using Jamii Forums mobile app