Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
- Thread starter
- #41
Mimi nakuwa mgumu kukubaliana na DR MVUNGI kwamba muungano unavunjwa kwa marekebisho ya Katiba ya Zanzibar. Muungano ni zao la Hati ya Muungano ambayo iliafikiwa na pande mbili za muungano na hatimaye kuwa sehemu ya msingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Pamoja na kuwepo serikali ya Muungano chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano, bado Zanzibar ilibaki kuwa na Katiba yake. Katiba ya Zanzibar ni zao la wananchi wa Zanzibar kwa kupitia Baraza lao la Kutunga Sheria. Hamna sehemu yoyote katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayoitiisha Katiba ya Zanzibar kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Kwa maoni yangu Raisi Kikwete hapaswi kulaumiwa kwa marekebisho ya Katiba ya Zanzibar kwakuwa Raisi wa Jamhuri sio ofisi inayoundwa chini ya Katiba ya Zanzibar wala haiwajibiki kwa Katiba ya Zanzibar. Raisi wa Jamhuri hana mamlaka yoyote halali katika Katiba ya Zanzibar. Hana ubavu kuwazuia Baraza la Wawakilishi kurekebisha Katiiba ya Zanzibar. Ni kwa maana hiyo nakubaliana na Mgongolwa kwamba suala hili ni la kisiasa zaidi kuliko kishearia.
Hata Katiba ya Jamhuri ambayo kimsingi chimbuko lake kuhusiana na muungano ni Hati ya Muungano imeshakiuka makubaliano ya msingi yaliyomo katika Hati ya Muungano lakini muungano bado upo. Mambo chingu nzima ambayo awali hayakuwa ya muungano yamefanywa kuwa ya muungano kwa marekebisho ya Katiba. Bahati mbaya wakati katiba inarekebishwa kugeuza mambo yasiyo ya muungano kuwa ya muungano vifungu vya Hati ya Muungano kuhusiana na masuala hayo vimebaki hivyo hivyo.
Hayo ni baadhi ya masuala ambayo yanaweza kijadiliwa na Mahakama ya Katiba inayotamkwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Kwamba
GEORGE JINASA
Hapa muafaka labda kuwe na Mahakama ya Katiba itakayoshughulikia migongano kati ya Katiba ya Zanzibar, 1984 na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977!