Dkt Mvungi: Muungano Ulishavunjika!

Buchanan

JF-Expert Member
May 19, 2009
13,199
1,969
Nimeangalia kipindi cha Pambanua cha Channel Ten ambapo David Ramadhan alikiongoza akiwa amewakaribisha Dkt Sengodo Mvungi ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Alex Mgongolwa wa Kituo cha Haki za Binadamu ambapo Dkt Sengodo Mvungi amedai kwamba mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 ya kuanzisha "Nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" ni kuvunja Jamhuri ya Muungano kwa sababu nchi ni Jamhuri ya Muungano na si vinginevyo. Kwa hiyo Jamhuri hiyo ilishavunjika tangu mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ambayo alidai kwamba "yalichomekewa!" Ni kwa sababu kulikuwa na swali kwenye kura za maoni: "Je, unataka mabadiliko ya Muundo wa Serikali baada ya uchaguzi wa Oktoba, 2010" ambalo alidai ni swali pana sana! Katika Orodha ya Mambo ya Muungano Dkt Mvungi alidai kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano nayo ni jambo la Muungano, kwa hiyo kuivunja Katiba hiyo ni kuvunja moja kati ya mambo ya Muungano. Pia amedai Wagombea wenza ni "batili" kwa sababu wanatoka "katika nchi nyingine!" Amedai kwamba saratani imeula Muungano wetu mpaka uko mahututi, tutafute suluhisho la kuachana na wazanzibari kwa amani tusije tukapigana. Tutapendana zaidi kuliko Wakenya na Waganda!

Kwa upande wa Alex Mgongolwa amedai kwamba tukae chini tutafute suluhisho kwa mazungumzo.

JK wetu ndio huyo hana habari kwamba hata urais wake wa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" haupo! Tujadili!
 
Lol... Kazi ipo... Hana habari JK yupo zake Kagera ana-campaign URAHISI wa Tanganyika bila ya kujua...
 
Anagombea urais wa nchi ambayo haipo kisheria! Kaaazi kweli kweli!

Sasa basi itabidi tuiweke kisheria, ukiangalia baadhi ya mambo utagundua Tanganyika ipo, kunamawaziri ambao si wa mungano hawa ni watanganyika, ukiangalia nembo ya Tanganyika ndio nembo ya Tanzania. Kwahiyo Tanganyika ipo lakini sio kisheria, na wazenj wamepiga kelele sana muungano unamatatizo,
 
Hivi huko kwenye kampeni hawatoi muda wa wapiga kua kuuliza maswali. Au ndo danganya watoto wanapangwa watu kuuliza maswali ya ya kitoto.

Huu muungano kwa maoni yangu unaweza kusurvive zaidi CUF wakishindaat least kwa muda fulani.Lakini sio CCM. CUF watahitaji muungano sana kuongoza zenj. CCM zenj wanataka kuchomoka kivyao as soon as possible.
 
Hivyi ninyi mnamlalamikia nani?
hakuna kiongozi wa nchi hii ambaye anajali masuala ya muungano.
Dawa ni kwenda mahakamani kuishtaki jamhuri na serikali ya zanzibar kwa kutishia uhai wa UWEPO WA TANZANIA
 
Nimeangalia kipindi cha Pambanua cha Channel Ten ambapo David Ramadhan alikiongoza akiwa amewakaribisha Dkt Sengodo Mvungi ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Alex Mgongolwa wa Kituo cha Haki za Binadamu ambapo Dkt Sengodo Mvungi amedai kwamba mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 ya kuanzisha "Nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" ni kuvunja Jamhuri ya Muungano kwa sababu nchi ni Jamhuri ya Muungano na si vinginevyo. Kwa hiyo Jamhuri hiyo ilishavunjika tangu mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ambayo alidai kwamba "yalichomekewa!" Ni kwa sababu kulikuwa na swali kwenye kura za maoni: "Je, unataka mabadiliko ya Muundo wa Serikali baada ya uchaguzi wa Oktoba, 2010" ambalo alidai ni swali pana sana! Katika Orodha ya Mambo ya Muungano Dkt Mvungi alidai kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano nayo ni jambo la Muungano, kwa hiyo kuivunja Katiba hiyo ni kuvunja moja kati ya mambo ya Muungano. Pia amedai Wagombea wenza ni "batili" kwa sababu wanatoka "katika nchi nyingine!" Amedai kwamba saratani imeula Muungano wetu mpaka uko mahututi, tutafute suluhisho la kuachana na wazanzibari kwa amani tusije tukapigana. Tutapendana zaidi kuliko Wakenya na Waganda!

Kwa upande wa Alex Mgongolwa amedai kwamba tukae chini tutafute suluhisho kwa mazungumzo.

JK wetu ndio huyo hana habari kwamba hata urais wake wa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" haupo! Tujadili!
Mkuu Buchanan, namkubali Prof. Mvingi kama msomi wa sheria aliyebobea kama ambavyo nitamkubali Prof. Mwakiembe, ila sizikubali comments zake kwenye baadhi ya issues kwa sababu yeye Mvungi, ameshajipambanua kushiriki siasa, na ndivyo ambavyo Prof. Mwakiembe atakavyo jipambanua kulinda mauza uza yote ya CCM.

Honest opinion kwenye hili, inatakiwa kutoka kwa wanasheria independent kama Prof. Shivji.

Kusu Zanzibar kuwa nchi ndani ya nchi, nilisema yafuatayo,
Zanzibar na Tanzania ni kama Baba na mwana. Wewe ndiye baba, unaitwa baba kwa sababu ndiye mkuu wa kaya, bread winner mwenye mamlaka yote.

Inapotokea mtoto wako umpendaye akaanza kulia kutwa kucha kwamba kwa nini ni wewe tuu unaitwa baba, na yeye anataka lazima aitwe baba, na kuendelea kulia kwa makelele mpaka unakosa amani, lakini wife alipomwambia 'nyamaza baba', ghafla alinyamaza na kuanza kufurahi sana, na yeye ameitwa Baba!, akamwambia mama na mimi ni baba. Jee wewe baba wa ukweli, utakasirika au kununa kuwa mwanao amechukua nafasi yako ya kuitwa baba, ama na yeye anataka kuitwa baba jina tuu lakini sio baba chochote, kwa vile powers za ubaba hana!.

Ndivyo ilivyo kwa JMT, Zanzibar kwanza walianza kwa kuomba bendera yao, wakapewa, kisha wakaomba wimbo wao wa taifa, wakapewa, kisha wale wagambo wao, (KMKM na JKU) kumpigia saluti rais wao, wakapewa, ndipo juzi wakajitwalia jina la 'nchi' na kuliingiza kwenye katiba ya Zanzibar ili hali kwenye katiba ya JMT, Zanzibar sio nchi ni sehemu tuu ya JMT. Jee JMT inasababu wa kuwakatalia kujiita majina yoyote inayoyataka hata wakiuita Falme za Zanzibar na kiongozi wao akawa Sultani Seif/Shein etc.

Zanzibar ni nchi kweli kama Zanzibar ndani ya Tanzania, kama mwanao atakavyoitwa baba ndani ya nyumba yenu, lakini nje ya nyumba, mwanao ni mtoto tuu, hana ubaba wowote mbele ya macho ya umma, ndivyo ilivyo nchi hii mpya ya Zanzibar, ni nchi jina tuu, haina uinchi yoyote mbele ya mataifa, ni nchi kwa maana ya eneo na jina tuu, isiyo na nguvu zozote za dola na za kinchi yaani sovereignty. Sasa unamashaka na jina tuu?.

Zanzibar nchi jina ndani ya muungano, sio nchi kimataifa na haina sovereignty!.
Pasco
 
kwa hiyo wazanzibar watapiga kura kuchagua rais wa muungano kwa ajili gani..............wakati mambo yote ya muhimu yaliyokuwa chini ya muungano sasa yapo chini ya zanzibar km nchi....
 
Nimeangalia kipindi cha Pambanua cha Channel Ten ambapo David Ramadhan alikiongoza akiwa amewakaribisha Dkt Sengodo Mvungi ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Alex Mgongolwa wa Kituo cha Haki za Binadamu ambapo Dkt Sengodo Mvungi amedai kwamba mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 ya kuanzisha "Nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" ni kuvunja Jamhuri ya Muungano kwa sababu nchi ni Jamhuri ya Muungano na si vinginevyo. Kwa hiyo Jamhuri hiyo ilishavunjika tangu mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ambayo alidai kwamba "yalichomekewa!" Ni kwa sababu kulikuwa na swali kwenye kura za maoni: "Je, unataka mabadiliko ya Muundo wa Serikali baada ya uchaguzi wa Oktoba, 2010" ambalo alidai ni swali pana sana! Katika Orodha ya Mambo ya Muungano Dkt Mvungi alidai kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano nayo ni jambo la Muungano, kwa hiyo kuivunja Katiba hiyo ni kuvunja moja kati ya mambo ya Muungano. Pia amedai Wagombea wenza ni "batili" kwa sababu wanatoka "katika nchi nyingine!" Amedai kwamba saratani imeula Muungano wetu mpaka uko mahututi, tutafute suluhisho la kuachana na wazanzibari kwa amani tusije tukapigana. Tutapendana zaidi kuliko Wakenya na Waganda!

Kwa upande wa Alex Mgongolwa amedai kwamba tukae chini tutafute suluhisho kwa mazungumzo.

JK wetu ndio huyo hana habari kwamba hata urais wake wa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" haupo! Tujadili!

alikuwa Harold Sungusia -
 
Mkuu Pasco umesema vizuri lkn si baadaye watataka vya ziada...
Ni kweli, tayari wameshayaomba mafuta na gesi asilia yatolewe kwenye orodha ya Muungano, na pia wamepitisha rasmi sheria ya kura za maoni ili baadaye waje wapige kura ya maoni kuhusu Muungano, hawakujua kuwa Nyerere ni Mkatoliki, ndoa ya Katoliki haina talaka, hata mke alete vitimbi gani vya kudai talaka, ndio maana CCM imemuweka pale Dr. Shein, maana Seif hata akishinda kura, hapewi nchi asijehatarisha muungano wetu huu adhimu ulioasisiwa na waasisi wa taifa letu tukufu.
 
Walichosema wataalam hao ni kweli na sahihi. Huwezi kuwa na Muungano wa Tanzania na Wakati huo na Nchi ya Zanzibar. Katika moja ya threads nililizungumza hili. Hata huu uchaguzi ni batili kwa sababu nchi inayoitwa Tanzania tayari imeishamegwa kipande na Kisheria haipo. Sijui hata hao wanaowania Ubunge kutoka Zanzibar wanajua wanalolifanya. Kuna mgogoro wa Kikatiba na jambo hili linaweza kutupeleka pabaya. Kwenye Gazeti la Mwanahalisi toleo la Jumatano tarehe 25/8/2010 kuna mada inazungumzia suala hili.
 
Buchanan, namkubali Prof. Mvingi kama msomi wa sheria aliyebobea kama ambavyo nitamkubali Prof. Mwakiembe, ila sizikubali comments zake kwenye baadhi ya issues kwa sababu yeye Mvungi, ameshajipambanua kushiriki siasa, na ndivyo ambavyo Prof. Mwakiembe atakavyo jipambanua kulinda mauza uza yote ya CCM.

Honest opinion kwenye hili, inatakiwa kutoka kwa wanasheria independent kama Prof. Shivji.

Kusu Zanzibar kuwa nchi ndani ya nchi, nilisema yafuatayo,
Zanzibar na Tanzania ni kama Baba na mwana. Wewe ndiye baba, unaitwa baba kwa sababu ndiye mkuu wa kaya, bread winner mwenye mamlaka yote.

Inapotokea mtoto wako umpendaye akaanza kulia kutwa kucha kwamba kwa nini ni wewe tuu unaitwa baba, na yeye anataka lazima aitwe baba, na kuendelea kulia kwa makelele mpaka unakosa amani, lakini wife alipomwambia 'nyamaza baba', ghafla alinyamaza na kuanza kufurahi sana, na yeye ameitwa Baba!, akamwambia mama na mimi ni baba. Jee wewe baba wa ukweli, utakasirika au kununa kuwa mwanao amechukua nafasi yako ya kuitwa baba, ama na yeye anataka kuitwa baba jina tuu lakini sio baba chochote, kwa vile powers za ubaba hana!.

Ndivyo ilivyo kwa JMT, Zanzibar kwanza walianza kwa kuomba bendera yao, wakapewa, kisha wakaomba wimbo wao wa taifa, wakapewa, kisha wale wagambo wao, (KMKM na JKU) kumpigia saluti rais wao, wakapewa, ndipo juzi wakajitwalia jina la 'nchi' na kuliingiza kwenye katiba ya Zanzibar ili hali kwenye katiba ya JMT, Zanzibar sio nchi ni sehemu tuu ya JMT. Jee JMT inasababu wa kuwakatalia kujiita majina yoyote inayoyataka hata wakiuita Falme za Zanzibar na kiongozi wao akawa Sultani Seif/Shein etc.

Zanzibar ni nchi kweli kama Zanzibar ndani ya Tanzania, kama mwanao atakavyoitwa baba ndani ya nyumba yenu, lakini nje ya nyumba, mwanao ni mtoto tuu, hana ubaba wowote mbale ya macho ya umma, ndivyo ilivyo nchi hii mpya ya Zanzibar, ni nchi jina tuu, haina uinchi yoyote mbele ya mataifa, ni nchi jina isiyo na nguvu zozote za dola. Sasa unamashaka na jina tuu?.

Zanzibar nchi jina!.
Mfano huu si mwafaka. Mfano stahiki ni ule mtoto anataka kurithi mali na madaraka wakati ungali hai. Akizidi kukuzonga bila shaka atakuua. Ndivyo walivyofanya akina Karume na Seif na BLWZ na SMZ.
 
Ibara ya 46B ya katiba inasema bayana:
Wajibu wa viongozi Wakuu wa vyombo vya Mamlaka ya Utendaji kudumisha Muungano
(1) Bila ya kuathiri wajibu wa kila raia uliotajwa katika ibara ya 28 ya Katiba hii, viongozi wakuu wa vyombo vyenye mamlaka ya utendaji
katika Jamhuri ya Muungano vilivyotajwa katika ibara ya 4 ya Katiba hii, watawajibika, kila mmoja wao katika kutekeleza madaraka
aliyopewa kwa mujibu wa Katiba hii au Katiba ya Zanzibar, 1984, kuhakikisha kuwa analinda, kuimarisha na kudumisha umoja wa
Jamhuri ya Muungano.

(2) Kwa madhumuni ya masharti ya ibara ndogo ya (1), kila mmojawapo wa viongozi wakuu wa vyombo vyenye mamlaka ya utendaji
katika Jamhuri ya Muungano kabla ya kushika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii ataapa kuitetea na kudumisha
umoja wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii.

(3) Viongozi wakuu wanaohusika na masharti ya ibara hii–
(a) Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(b) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(c) Rais wa Zanzibar; na
(d) Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.

Je ni uhaini?????????
 
Ibara ya 46B ya katiba inasema bayana:
Wajibu wa viongozi Wakuu wa vyombo vya Mamlaka ya Utendaji kudumisha Muungano
(1) Bila ya kuathiri wajibu wa kila raia uliotajwa katika ibara ya 28 ya Katiba hii, viongozi wakuu wa vyombo vyenye mamlaka ya utendaji
katika Jamhuri ya Muungano vilivyotajwa katika ibara ya 4 ya Katiba hii, watawajibika, kila mmoja wao katika kutekeleza madaraka
aliyopewa kwa mujibu wa Katiba hii au Katiba ya Zanzibar, 1984, kuhakikisha kuwa analinda, kuimarisha na kudumisha umoja wa
Jamhuri ya Muungano.

(2) Kwa madhumuni ya masharti ya ibara ndogo ya (1), kila mmojawapo wa viongozi wakuu wa vyombo vyenye mamlaka ya utendaji
katika Jamhuri ya Muungano kabla ya kushika madaraka yake kwa mujibu wa Katiba hii ataapa kuitetea na kudumisha
umoja wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii.

(3) Viongozi wakuu wanaohusika na masharti ya ibara hii–
(a) Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(b) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano;
(c) Rais wa Zanzibar; na
(d) Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano.

Je ni uhaini?????????

It is treason in strict terms!
 
It is treason in strict terms!

and complicated sort of, to harmonise the Union constitution with the Zanzibar constitution the union constitution must be changed substantially.It means the whole structure of the Union Constituion will change.

Are the people responsible aware of that ?
 
and complicated sort of, to harmonise the Union constitution with the Zanzibar constitution the union constitution must be changed substantially.It means the whole structure of the Union Constituion will change.

Are the people responsible aware of that ?

Is that the way of dealing with the highest criminal act in the land (ie treason), by condoning it?
 
Back
Top Bottom