Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Nimeangalia kipindi cha Pambanua cha Channel Ten ambapo David Ramadhan alikiongoza akiwa amewakaribisha Dkt Sengodo Mvungi ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Alex Mgongolwa wa Kituo cha Haki za Binadamu ambapo Dkt Sengodo Mvungi amedai kwamba mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar, 1984 ya kuanzisha "Nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" ni kuvunja Jamhuri ya Muungano kwa sababu nchi ni Jamhuri ya Muungano na si vinginevyo. Kwa hiyo Jamhuri hiyo ilishavunjika tangu mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ambayo alidai kwamba "yalichomekewa!" Ni kwa sababu kulikuwa na swali kwenye kura za maoni: "Je, unataka mabadiliko ya Muundo wa Serikali baada ya uchaguzi wa Oktoba, 2010" ambalo alidai ni swali pana sana! Katika Orodha ya Mambo ya Muungano Dkt Mvungi alidai kwamba Katiba ya Jamhuri ya Muungano nayo ni jambo la Muungano, kwa hiyo kuivunja Katiba hiyo ni kuvunja moja kati ya mambo ya Muungano. Pia amedai Wagombea wenza ni "batili" kwa sababu wanatoka "katika nchi nyingine!" Amedai kwamba saratani imeula Muungano wetu mpaka uko mahututi, tutafute suluhisho la kuachana na wazanzibari kwa amani tusije tukapigana. Tutapendana zaidi kuliko Wakenya na Waganda!
Kwa upande wa Alex Mgongolwa amedai kwamba tukae chini tutafute suluhisho kwa mazungumzo.
JK wetu ndio huyo hana habari kwamba hata urais wake wa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" haupo! Tujadili!
Kwa upande wa Alex Mgongolwa amedai kwamba tukae chini tutafute suluhisho kwa mazungumzo.
JK wetu ndio huyo hana habari kwamba hata urais wake wa "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" haupo! Tujadili!