Dkt. Gwajima: Tukatae utapeli, Binti aliyedai anaishi na nyoka akiri haikuwa kweli

Dkt. Gwajima D

JF-Expert Member
Nov 28, 2015
602
3,982
BINTI ALIYEDAI ANAISHI NA NYOKA AJISALIMISHA KWA WAZIRI DKT. GWAJIMA

Aomba radhi, adai hajawahi kufanya hivyo alidanganya.

DAR ES SALAAM.

Itakumbukwa hivi karibuni ilienea video mitandaoni kupitia televisheni ya MBENGO TV ikionesha Binti mmoja aliyekuwa amebeba nyoka mkubwa huku akidai kwamba, hufanya naye mapenzi ili kupata fedha.

Kufuatia hali hiyo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Mhe. Dkt. Gwajima , alichukua hatua ya kukemea kitendo hicho na kumtaka ajitokeze kuomba radhi kwa Umma na kuondoa taarifa hiyo mtandaoni kutokana na kukiuka maadili.

Baada ya mmiliki wa Mbengo TV, Tarzan Mustapha aliyeambatana na mtangazaji Lenny kuomba radhi Mei 11, 2024, walielekezwa kumtafuta binti huyo waliyemrekodi vinginevyo wachukuliwe hatua za kisheria kwa kukiuka sheria ya usajili wao kwa kushirikiana kupotosha jamii kwa habari za utapeli.

Leo 20 Mei, 2024 Binti huyo aitwaye Veronica Bernad Anton aliyekuwa amebeba nyoka huyo naye amejisalimisha kwa Waziri Dkt. Gwajima na kuomba radhi kama video inavyoonesha.

Waziri Dkt. Gwajima ameelekeza kutafutwa kwa mmiliki wa nyoka au ajitokeze mwenyewe kabla hatua za Serikali kumtafuta hazijaanza ambapo, itaongeza makosa yake ya kutotoa ushirikiano kwa Serikali.

Waziri Dkt. Gwajima ameiasa jamii ya wanahabari na wasanii kuachana na utapeli na mambo yote yanayochochea mmonyoko wa maadili maana akiwa Waziri mwenye dhamana na Jamii yenye makundi maalum hatafumbia macho uongo, utapeli na uovu huo.

MWISHO

NB; nawasihi wanajamii wote kuheshimu Sheria kwa maendeleo na ustawi wa jamii na kutunza maadili.

Pia soma: Epuka kusambaza maudhui yasiyo na maadili. Anayedai kumiliki nyoka na kushiriki naye tendo, ajisalimishe
IMG-20240520-WA0144.jpg

 
Tena hizi online tv zinazoripoti habari za uzushi zinazidi kwa nyingi, TCRA wapo kimya tu. Upotoshaji mwingi unafanyika na hizi online tv ili wapate watazamaji wengi kwa makusudi ya kulipwa na Youtube.
Zikiripoti habari za Chadema za Ukweli zinapigwa vita ila ziki ripoti habari za uongo na uchochezi ndio kwanza wanakaribishwa White house.

Tuna shida mahara Ndugu Waziri Dr Gwajima.
 
Kazi nzuri muheshimiwa.

Japo na swali dogo nakunukuu

"Waziri Dkt. Gwajima ameelekeza kutafutwa kwa mmiliki wa nyoka au ajitokeze mwenyewe kabla hatua za Serikali kumtafuta hazijaanza ambapo, itaongeza makosa yake ya kutotoa ushirikiano kwa Serikali."

Muheshimiwa hivi ikitokea serikali haitoi ushirikiano kwa raia, je raia anatakiwa kufanya nini ama taratibu ipi inafanyika?

Pole na hongera kwa majukumu muheshimiwa
 
Wenye ufahamu,akili,uelewa,ujanja mwingi tuliligundua hilo kitambo
Tu, kwa huyo binti ni fix tu
Hivi kwanini msimtandike vibao
Pia.....kapuz sana

Nchi sahivi kuna ujingaujinga mwingi unafanyika huku zikipewa nguvu na media uchwara.

Hivi mtu na akili yako timamu unaweza wafatilia hao mbegu sijui mbengo TV...takataka kabisa
Vi media vyote ni uchwara tu

Ova
 
Dr Gwajima nakukubali sana Mama umefanya vizuri.

Usiishie hapo Wanawake na wasichama wadogo wamejikuta wakijiingiza kwenye vitendo viovu kutokana na shuhuda za uongo.

Pia huko Instagram na face book wapo.

Na makanisani nako pia Wanawake wanaangamia kwa shuhuda za uongo zinazoambatana na imani za kidini
Nchi ina wajing wengi na hawasiki
Ndomana wanapigwa

Ova
 
Back
Top Bottom