Dkt. Charles Kimei anza kupiga 'jaramba', huenda muda wowote ukamrithi aliyeleta tozo za ovyo

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,568
108,911
Kuna Watu wameteuliwa ila hawajui tu kuwa wapo katika 'Sacrifice List' ya 'Mama' kutokana na Rekodi zao mbovu na pia kwa Tamaa zao za Kuutaka sana Urais tena wa 2025.

Hakika 'Mama' kwa Kusaidiwa na Taasisi fulani 'Muhimu' nchini anaonyesha kuwa japo Yeye ni Mwanamke ila katika Umafia wa Kidiplomasia ameiva kuliko hata Wanaume hivyo 'amewatega' Wabaya wake wote ndani ya Chama kwa Ustadi mkubwa ili washindwe au wakengeuke 'Kimaamuzi' na awamalize vizuri kwa 'Kuwatumbua' bila Huruma kisha Kuwamaliza zaidi Kisiasa.

Kuna Mtu alidhani alipopeleka Karatasi kwa 'Mama' atie Saini japo fulani linaloumiza Watanzania sasa atakuwa 'anamkomoa' ili achafuke ila kwa Upumbavu wake japo ana 'PhD' yake akasahau kuwa licha ya 'Mama' kutia Saini Yeye kama mwenye Dhamana alitakiwa awahusishe Wataalam wa Kikosi Kazi cha 'Mtonyo' ambao wangemshauri kutofanya alichofanya kutokana na Hali ya 'Mtonyo' kuwa mbaya kwa sasa ila kwa kutaka Kwake Sifa na Kumuharibia 'Mama' akaenda nayo hivyo hivyo.

Baada ya kuingia 'Mtegoni' na Kujimaliza zaidi kwa Kauli yake ya 'hameni Dar es Salaam mkaishi Bujumbura' ni kwamba 'Mama' ameshaipata sababu ya 'Kumuondoa' huku pia akionekana kuwa ni Adui yake katika Uchaguzi Mkuu ujao wa 2025 na akiwa pia na Makundi 'Hatari' ndani ya Chama Tawala.

Hivyo basi kwa za 'chini chini' ambazo hazijawa rasmi bado ( ila zinatokea Jikoni pale ( Msaada Kontena ) zinasema kwamba mwenye kujua vyema Financial Management, Economost na Mtu aliyeacha Alama ya 'Kutukuka' CRDB Dr. Charles Kimei ( Mbunge ) huenda muda wowote akachukua 'Mikoba'.

Kama kweli 'Mama' atamweka hapa huyu 'Mchagga' anayejua vyema Kusimamia Fedha na Kuzizalisha kwa Maendeleo zaidi hata Mimi GENTAMYCINE nitafurahi kwani CRDB aliyoikuta Dr. Kimei si hii ambayo ameondoka na kuiacha ikiwa na Maendeleo makubwa na kuwa Financial Institution ya Mfano kabisa Kiufanisi.

Nilikuwa nimeshaanza Safari ya kwenda kuyaanza Maisha mapya Bujumbura kama tulivyofukuzwa na mwenye Dar es Salaam, Dodoma na Singida yake ila nilipotonywa tu kuwa Mzee Dr. Kimei anaweza 'Kuula' imenibidi nishukie Mdaula na nirejee zangu Dar es Salaam.

Ombi langu Kuu tu ni kwamba naziomba Mamlaka husika zimlinde Dr. Kimei na hata Dr. Kimei nae pia ajilinde vilivyo kwani moja ya Sifa Kuu ya Msomi Mpuuzi ni Umafia ( Ukatili ) na hata ndani ya Chama anajulikana na ametumika katika 'Oparesheni' kadhaa Kipindi cha Mswahili wa Msoga ( japo kwa Hayati alitulizwa kiaina ) na wenye Kazi zao.

Na nilimshangaa 'Mama' kumteua huyu.
 
Kama namuona Dr kimei anavyokula jalamba kwenye pitch ya B.O.T. japo siasa sihifahamu Kwa kina ,ila mwigulu hakuwa chaguo sahihi Kwa wizara nyeti Kama fedha.Ni mnafiki aliyejifunika mwamvuli wa uzalendo na maskafu yake ,anajifanya anaupiga mwingi kumbe Ujinga tu
 
Back
Top Bottom