hawa mbona hawaeleweki,wanapambana na nani Sasa,wameanza kushambuliana wao kwa wao,siasa shikamoo,baada ya kuimaliza CUF na CHADEMA sasa wanawageukia maraisi wastaafu?
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini mimi naona kama huyu jamaa yaani Katibu Mkuu ccm amezungumza kwa mafumbo. Hapo ni wazi kuwa awamu hii ya tano umelemewa na mzigo mkubwa baada ya kukosa maarifa ktk uongozi wa juu.Wametafuta ugomvi nje ya CCM imeshindikana. Sasa wanaanza kutafuta ugomvi ndani ya CCM yenyewe. Wanachotafuta watakipata muda so mrefu
Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo Mkuu kuna usemi usemao "fumbo mfumbe mjinga, mwerevu aling'amue"Uchaguzi wa serikali za mitaa wa hivi karibuni kabisa watu wameususia mbona, Bashiru anasema idadi ya wapiga kura inaongezeka vipi?
Sent using Jamii Forums mobile app
Africa is shit holeJapo ni msemo unaouma ila sometimes Trump alikua sahihi...
Nakubaliana nawe. JK is very smart na anajua kucheza na emotionsHakuna Tusi jipya la kumnyima Usingizi Mzee Kikwete
Kama aliweza kuvumilia matusi akiwa Amiri jeshi ndio ashindwe akiwa Mwana kijiji wa Msoga?, kuna kitu wanakitaka toka kwa Jk lakin wanakosa pa kuanzia na Jk ni mjanja kawazidi hatua elfu moja
Unafurahi kuitwa mnyonge?CCM chama cha wanyonge, nawaona CCM wenzangu hapo aka wanyonge wenzangu.
Enzi za Mzee Kikwete chama kiliporwa kwa wanyonge wakakichukua mafisadi CDM, sasa chama kimerudi tena kwa wanyonge na maendeleo yanakuja kwa kasi balaa, Unyonge ni sifa nzuri sana jamani na ni raha sana kuwa mnyonge na ukachagua chama cha wanyonge CCM.. Tumeamua kuwa wanyonge.
Na huyu baba ubaya katengeneza sio ufike mda tuwe na aibu ccm oyee🤣🤣🤣
We jamaaa nomaaa Sana unanifanya naonekana kituko hapa😄😄😄Hapo kwenye wasema kweli wakawa maadui wa Chama nimecheka hadi nimezimia.
Ndio wananipepea hapa...
January 19, 2020
Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru anaichambua safari ya kisiasa ya CCM toka mwaka 2015, ambapo kura za CCM ziliporomoka na Magufuli alipata 58%. Fitna na misukosuko ikawa jadi ya chama. Wasemakweli wakawa maadui wa chama na kupelekea kuitwa na Halmashauri Kuu ya Chama NEC wakapewa adhabu na wengine kufukuzwa
WanaCCM wenye nia njema wakaanza kukaa kando na chama kikaanza kuendeshwa na wachache wababaishaji. Watu wanapata kazi ndani ya CCM bila ujuzi wanapata nafasi hizo kiushikaji. Miradi mingi inayohusu watu (Maendeleo ya Watu) ikafa.
Hata idadi ya wapiga kura ikaanza kuporomoka kutokana na wananchi kukosa imani na CCM. Watu hawana imani na vyombo vya kusimamia uchaguzi chini ya serikali ya CCM.
Dkt. Bashiru katika kikao hicho na wanaCCM anasema wote tunaona Baada ya miaka minne ya Magufuli mambo yamebadilika, yale ya Kikwete niliyoyabainisha yamefutika. Sasa Watu wanaimani na uchaguzi, idadi ya wapiga kura imepanda na kupanda maradufu sana.
Mkazo ktk Maendeleo ya Watu umezidi kusisitizwa sambamba na Maendeleo ya Vitu chini ya Awamu ya Tano.
Bashiru anaendelea kujadili na kuwaomba rai wanaCCM tusibishanie ndege, flyovers, madaraja na SGR reli Mpya maana sote tunaona Maendeleo hayo ya Vitu na Maendeleo ya Watu hivyo tusikazanie ktk kitu 'matumaini', bali vitu halisi tunavyoviona na kuvishika. Matumaini ni matamanio kama mapenzi huwezi kuvipima au kuvishika na hayana uhalisia hivyo haya Maendeleo ya Vitu kama ndege ni maendeleo dhahiri tusiyabishanie.
Bunge limekuwa na heshima hakuna vurugu. Demokrasia na Haki za binadamu imezidi kuzingatiwa kama ilivyoainishwa na Katiba yetu ya nchi. Chaguzi kama za Serikali za Mitaa November 14, 2019 chini ya wizara ya TAMISEMI zimefanyika bila vurugu na CCM imeshinda kwa kishindo asilimia 98%.
Source: Millard Ayo.