Dkt. Bashiru: Baada ya mzee Kikwete kuingia kura zetu (CCM) zilianza kuporomoka

Wametafuta ugomvi nje ya CCM imeshindikana. Sasa wanaanza kutafuta ugomvi ndani ya CCM yenyewe. Wanachotafuta watakipata muda so mrefu

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini mimi naona kama huyu jamaa yaani Katibu Mkuu ccm amezungumza kwa mafumbo. Hapo ni wazi kuwa awamu hii ya tano umelemewa na mzigo mkubwa baada ya kukosa maarifa ktk uongozi wa juu.

Toka tuanze mfumo wa vyama vingi hakuna uchaguzi uliotia aibu nchi yetu ndani na nje kama huu wa serikali za mitaa uliofanyika mwaka jana. Hata Bashiru mwenyewe hilo analifahamu vema lkn hana namna zaidi ya kupaka nyumba ya udongo rangi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uchaguzi wa serikali za mitaa wa hivi karibuni kabisa watu wameususia mbona, Bashiru anasema idadi ya wapiga kura inaongezeka vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo Mkuu kuna usemi usemao "fumbo mfumbe mjinga, mwerevu aling'amue"
Hilo halina ubishi kwani wenyeviti wote wa ccm waliopatikana hawakuchaguliwa na wananchi. Wale ni wenye viti wa "viti maalum". Aibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna Tusi jipya la kumnyima Usingizi Mzee Kikwete

Kama aliweza kuvumilia matusi akiwa Amiri jeshi ndio ashindwe akiwa Mwana kijiji wa Msoga?, kuna kitu wanakitaka toka kwa Jk lakin wanakosa pa kuanzia na Jk ni mjanja kawazidi hatua elfu moja
Nakubaliana nawe. JK is very smart na anajua kucheza na emotions
 
Je, huu pia ni mtizamo wa mwenyekiti wake na uongozi wa ccm? Jamani nchi si kama timu ya mpira ambapo kushindwa kwa timu kocha kutoolewa kafara hata kama wengine wana matege mipira inapenya na kuingia golini. Kumbe matege si ya kocha. Kila mtu anajua mpira hata shabiki anapanga timu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CCM chama cha wanyonge, nawaona CCM wenzangu hapo aka wanyonge wenzangu.

Enzi za Mzee Kikwete chama kiliporwa kwa wanyonge wakakichukua mafisadi CDM, sasa chama kimerudi tena kwa wanyonge na maendeleo yanakuja kwa kasi balaa, Unyonge ni sifa nzuri sana jamani na ni raha sana kuwa mnyonge na ukachagua chama cha wanyonge CCM.. Tumeamua kuwa wanyonge.
Unafurahi kuitwa mnyonge?
Hizi akili hizi!!!! Dah

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maneno haya waachiwe wananchi wa kawaida lakini katibu mkuu ni mkubwa mno kumshutumu moja kwa moja. Haisaidii kusema tu bora angeshauri kuwepo na sheria ya kuwashtaki marais wastaafu. Kama wanalindwa na sheria au katiba kumtuhumu hakusaidii nchi zaidi ya manufaa kwa mtoa tuhuma.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
bagamoyo,
Ni imani yangu mh katibu mkuu ameteleza kwani Jakaya sio mtani wake,Ukimuacha Nyerere,Jakaya ndiye mwana demokrasia wa kweli nchi hiii,Hizi kashfa na kejeli kwake ni kama mizaha ya kawaida na wajukuu zake nyumbani.
 
Bashiru huyu nahisi siye watakuwa wamemfanyia plastic surgery, maana huyu ambaye ni katibu mkuu hana weredi hata chembe.

CCM ilikwisha poteza legitimacy mbele ya watanzania hata ideology yao ime change abruptly. Hakuna ujamaa na kujitegemea wapo very randomly wameachana na ideology wamejiingiza kwenye unyonge, wakilindwa na dola, ndo maana bila dola hakuna CCM.

Hayati Horace Kolimba aliwahi kusema CCM imepoteza dira na mwelekeo,hakuna aliyekuja kulifanyia tafiti hilo,lakini katibu Mkuu Kinana alithubutu kukinusuru chama chao kwa kufika kwa wananchi(grassroot) si wanachama, bali wananchi na kuwaaminisha na kurudisha imani ya chama kwao.

Tofauti na leo katibu mkuu na timu yake wanafikia hotel za gharama, wanaelezwa matatizo ya mjini nakuishia mjini kisha wanaita media kwa ajili ya coverage, na hii ndo CCM ya wanyonge.

Kumnanga Kikwete hakukijengi chama, wachawi ni wao wenye kuendekeza siasa za ukanda na ubinafsi.
 
CCM ya leo inataka kupandia ngazi kwa kumchafua Mzee Kikwete!! huu siyo uugwana hata kidogo mwachane Mzee wa Msoga apumzike - nyie tatueni matatizo yenu wenyewe - kwanza hizo memo za kimataifa kuhusu demokrasia na utawala bora mmeshazijibu? mziwazuge watanzania !!
 
Mpumbavu huyu kwani nani kamuambia kura za ccm zitaongezeKa kwa jpm,
Uchaguzi serikali za mitaa kura zilizopigwa zilikua ngapi,
Watu wamekata tamaa kwa kua wanajua sanduku la kura ni majizi matupu.nchi iko ktk hali ya taharuki, hakuna amani ya kweli
January 19, 2020


Katibu Mkuu wa CCM Dkt Bashiru anaichambua safari ya kisiasa ya CCM toka mwaka 2015, ambapo kura za CCM ziliporomoka na Magufuli alipata 58%. Fitna na misukosuko ikawa jadi ya chama. Wasemakweli wakawa maadui wa chama na kupelekea kuitwa na Halmashauri Kuu ya Chama NEC wakapewa adhabu na wengine kufukuzwa

WanaCCM wenye nia njema wakaanza kukaa kando na chama kikaanza kuendeshwa na wachache wababaishaji. Watu wanapata kazi ndani ya CCM bila ujuzi wanapata nafasi hizo kiushikaji. Miradi mingi inayohusu watu (Maendeleo ya Watu) ikafa.

Hata idadi ya wapiga kura ikaanza kuporomoka kutokana na wananchi kukosa imani na CCM. Watu hawana imani na vyombo vya kusimamia uchaguzi chini ya serikali ya CCM.

Dkt. Bashiru katika kikao hicho na wanaCCM anasema wote tunaona Baada ya miaka minne ya Magufuli mambo yamebadilika, yale ya Kikwete niliyoyabainisha yamefutika. Sasa Watu wanaimani na uchaguzi, idadi ya wapiga kura imepanda na kupanda maradufu sana.

Mkazo ktk Maendeleo ya Watu umezidi kusisitizwa sambamba na Maendeleo ya Vitu chini ya Awamu ya Tano.

Bashiru anaendelea kujadili na kuwaomba rai wanaCCM tusibishanie ndege, flyovers, madaraja na SGR reli Mpya maana sote tunaona Maendeleo hayo ya Vitu na Maendeleo ya Watu hivyo tusikazanie ktk kitu 'matumaini', bali vitu halisi tunavyoviona na kuvishika. Matumaini ni matamanio kama mapenzi huwezi kuvipima au kuvishika na hayana uhalisia hivyo haya Maendeleo ya Vitu kama ndege ni maendeleo dhahiri tusiyabishanie.

Bunge limekuwa na heshima hakuna vurugu. Demokrasia na Haki za binadamu imezidi kuzingatiwa kama ilivyoainishwa na Katiba yetu ya nchi. Chaguzi kama za Serikali za Mitaa November 14, 2019 chini ya wizara ya TAMISEMI zimefanyika bila vurugu na CCM imeshinda kwa kishindo asilimia 98%.

Source: Millard Ayo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom