Dk. Slaa: Tutajibu mapigo

Dk. Slaa: Tutajibu mapigo

Kimsingi itakuwa vigumu sana kwa Tv zetu kuonyesha video inayopingana na Taarifa ya Serikali, Labda wapeleke Tv za nje au za mashirika ya Dini

Kwa taarifa yao ni kuwa mkanda huo utagawiwa kwa umma pia. Hivyo hata TV zikibana watu watauona kwenye sebule za watu; vijiweni na hata kwenye baa. Kwa taarifa tu ni kuwa hakuna sumu mbaya inayoenea kwa haraka kama ile inayosambazwa kupitia mtandao huru (nguvu binafsi). Sote sasa tunajua kilichomtoa yule Rais wa Tunisia. ... Si kupitia vyombo vya habari vya umma ila mitandao. Taarifa zikafikia watu, waliposhtuka watu wako barabarani. Endapo TV zitagoma kuonyesha zitazidisha kiu ya watanzania kuusaka ukweli. Ukweli unatabia moja, huwa haufichwi mvunguni maana utatoka tu siku moja.
Aluta Continua CDM!
 
Title yake itakuwaje??

Ya polisi tuliambiwa "ukweli juu ya matukio ya arusha"
 
Issues siyo video wala namna police walivyofanya kudhibiti uhuni wa Chadema uliokuwa kwenye cover la maandamano. Issue ni IQ ya viongozi wa Chadema kulazimisha maandamano ili hali wakijua hayo madhara kuwa yangetokea. Kwa sasa hatuhitaji kuona madhara kwenye CD. Ni upuuzi mtupu.

Tutahitaji kuona viongozi wa Chadema wanachuliwa hatua stahiki za kisheria kukomesha kundi lingine la namna hiyo lisije ibuka. Mbona vyama vingine viko peace na waelewa sana, iweje Chadema iwe chanzo cha kila aina ya uhuni sasa hivi?! Hatuwezi tukawa na genge la wahamasishaji fujo, tena wanahamasisha kwa watu ambao ni destitute kabisa, hawana mbele wala nyuma na kuelewa chochote kinachoendelea Duniani.
 
Issues siyo video wala namna police walivyofanya kudhibiti uhuni wa Chadema uliokuwa kwenye cover la maandamano. Issue ni IQ ya viongozi wa Chadema kulazimisha maandamano ili hali wakijua hayo madhara kuwa yangetokea. Kwa sasa hatuhitaji kuona madhara kwenye CD. Ni upuuzi mtupu.

Tutahitaji kuona viongozi wa Chadema wanachuliwa hatua stahiki za kisheria kukomesha kundi lingine la namna hiyo lisije ibuka. Mbona vyama vingine viko peace na waelewa sana, iweje Chadema iwe chanzo cha kila aina ya uhuni sasa hivi?! Hatuwezi tukawa na genge la wahamasishaji fujo, tena wanahamasisha kwa watu ambao ni destitute kabisa, hawana mbele wala nyuma na kuelewa chochote kinachoendelea Duniani.

Kwa taarifa yako watanzania si mambumbu tena, hatuko tayari kuona nchi yetu inaendelea kutawaliwa na genge la mafisadi, hatuko tayari kuona raslimali za taifa zikiendelea kutafunwa na kakundi kadogo ka wezi ili hali watanzania walio wengi wakifa kwa njaa na magonjwa yanayo tibika, Hatuko tayari kuona genge la wahuni wachache wakituchagulia vibaraka wao na kuwaweka eti wawe ndo viongozi wetu ili waendelee kulinda wizi na ufisadi wao, Enough is enough, we are tired, we need our freedom back, which for sure is very near!

Kawambie hao walokutuma kwamba 'aisee sasa si mwaka 47, hata ule mkanda tulo chakachua wameustukia, na sasa wanatoa wa kwao, ambao hata tukizuia TV zisiuonyeshe, technologia ita tuumbua, watauweka bure kwenye mtandao, na hapo ndo tutazidi kuumbuka, kwani utaonekana dunia nzima, si hivyo tu, siku hizi TV zipo kila kona, watanunua hiyo mikanda na watatuona' Halafu kibaya zaidi, huo mkanda watauuza kama njugu, na chama kitazidi kuongeza pato kutokana na mkanda huo'

......Kanyafu peleka huo ujumbe haraka kwa bosi wako..
 
Nisichokubaliana na baadhi yenu humu ni hili la WATANZANIA kufa kwa malengo ya KISIASA kama ilivyotokea Arusha na kabla ya hapo Pemba. Hakuna kifo kinachokubalika lakini hili la vifo vya kisiasa halina TIJA wala maana yoyote kwa Mtanzania wa kawaida. Ni afadhali Mtanzania afe kwa kudai.... AJIRA, kulalamikia bei ya kilo ya unga, bei ya mkate, bei ya umeme, bei ya maji, karo kubwa za shule, huduma mbaya za elimu kwenye mashule ya UMMA na mambo yanayofanana na hayo.
Tusiendelee kuua watu wetu kwa malengo ya KISIASA ambayo hayawabadilishii lolote watu wetu. Wakati wa kampeni, Dr Slaa alisisitiza mara kwa mara juu ya kutomwaga damu ya Watanzania ili aende IKULU. Ni nini kinafanyika sasa?

Mkuu mbona unajikanyaga na kujikanganya? unakata nini na unakubali nini? Soma vizuri penye nyekundu.
Nani kakwambia arusha waliandamana ili kusudi wafe?kama hayo yalikuwa ndiyo makusudi yao, kulikuwa na sababau gani kuomba kibali Polisi cha kufanya maandamano ya Amani? tatizo umekurupuka ukasahau watu wa Arusha hawakuandamana ili wapambane bali waliandamana ili kuwasirisha madai ya dhidi ya dhuluma waliyofanyiwa kwa kuporwa uongozi wanaoutaka wao.
Shame! Ni Polisi ndiyo waliouwa watu. Mbona siku ya mazishi Polisi hakuwapo hata mmmoja, idadi ya wana-Arusha ilikuwa kubwa zaidi na zaidi, lakini hujasikia wala kusoma kuwa kuna walijikwaa achilia mbali kuwa majeruhi? POLISI wameua.
Mimi sikubali mtu yeyote kuuliwa anapodai kitu chochote cha haki. Kama si cha haki akamatwe atiwe ndani. Katika vita ruksa kuua.

Mbona unakuwa mzushi hivyo? Wapi Dr Slaa amemwaga damu ya mtanzania? Wapi amesababisha damu ya mtanzania kumwagika? Hivi umewahi kutafakari busara yake imezuia damu kiasi gani isimwagike? hata hili lililofikishwa na mtoa mada huoni Dr Slaa akisababisha watu kumwaga damu. anataka kuweka wazi ukweli. Huitaji kukaa katika ujinga(kwa kufichwa ukweli) wa CCm ili uendelee kutawaliwa.

Taratibu Mkuu, soma tena na tena.
 
Umakini wa Serikali upo wapi? Ni hatari kwa serikali kufanya uchakachuaji kwa kila jambo.

Aibu yao kusema mkanda umechakachuliwali wakati ukweli hata wao wanaujua hakuna kilichochakachuliwa ila wametoa vipengele muhimu vya chanzo na sababu na jinsi vulugu zilivyofanywa......huwezi kusema kuwa wananchi kushambulia polisi kwa mawe ilikuwa ni sawa.huo ni uongo na wala si kweli kuwa chadema wanaweza kuonyesha mkanda mzima bila kuchagua maeneo muhimu.....huwezi kuweka hutuba nzima ya ndesa na slaa zenye masaa matatu,maandamano ya asubuhi na ya jioni yenye karibu masaa matatu.tv gana inaweza kuweka masaa sita kuonyesha matukio hayo tu.....labda tungoje tuone huo mkanda ambao hautakuwa umechujwa utakuwaje
 
Issues siyo video wala namna police walivyofanya kudhibiti uhuni wa Chadema uliokuwa kwenye cover la maandamano. Issue ni IQ ya viongozi wa Chadema kulazimisha maandamano ili hali wakijua hayo madhara kuwa yangetokea. Kwa sasa hatuhitaji kuona madhara kwenye CD. Ni upuuzi mtupu. Tutahitaji kuona viongozi wa Chadema wanachuliwa hatua stahiki za kisheria kukomesha kundi lingine la namna hiyo lisije ibuka. Mbona vyama vingine viko peace na waelewa sana, iweje Chadema iwe chanzo cha kila aina ya uhuni sasa hivi?! Hatuwezi tukawa na genge la wahamasishaji fujo, tena wanahamasisha kwa watu ambao ni destitute kabisa, hawana mbele wala nyuma na kuelewa chochote kinachoendelea Duniani.

Hapo kwenye nyekundu unaweza kutoa uthibitisho wa vurugu, ghsia, maandamano na uhuni wowote unaoujua wewe hata ile ya wazee wastaafu kupigwa pale daraja la "Surender" ama Kivukoni Front kuwa CHADEMA walihusika.Anzia 2005 hadi 2011, maana vimetukia katika awamu ya SASA (ya nne).

Ukishindwa, kwa uungwana njoo uombe radhi.
 
uchakachuaji inaelekea kuwa utamaduni wa serikali na vyombo vyake vya dola. eeeh! Rais aliyechakachua analazimisha kila eneo pawe na uchakachuaji?? Yaani TBC1 kwa sasa huwezi kuiamini tena, Habari leo pia ni vilevile.
 
Nisichokubaliana na baadhi yenu humu ni hili la WATANZANIA kufa kwa malengo ya KISIASA kama ilivyotokea Arusha na kabla ya hapo Pemba. Hakuna kifo kinachokubalika lakini hili la vifo vya kisiasa halina TIJA wala maana yoyote kwa Mtanzania wa kawaida. Ni afadhali Mtanzania afe kwa kudai AJIRA, kulalamikia bei ya kilo ya unga, bei ya mkate, bei ya umeme, bei ya maji, karo kubwa za shule, huduma mbaya za elimu kwenye mashule ya UMMA na mambo yanayofanana na hayo.
Tusiendelee kuua watu wetu kwa malengo ya KISIASA ambayo hayawabadilishii lolote watu wetu. Wakati wa kampeni, Dr Slaa alisisitiza mara kwa mara juu ya kutomwaga damu ya Watanzania ili aende IKULU. Ni nini kinafanyika sasa?

Some people are so naive!
Unasema
"Ni afadhali Mtanzania afe kwa kudai AJIRA, kulalamikia bei ya kilo ya unga, bei ya mkate, bei ya umeme, bei ya maji, karo kubwa za shule, huduma mbaya za elimu kwenye mashule ya UMMA na mambo yanayofanana na hayo."

My friend,politics defines all of the above.
 
Sijui wataoneshea kupitia tv gani? StarTv ni ya Diallo ambaye ni mwana CCM anayetegemea kuchaguliwa kuwa mkuu wa mkoa;TBC1,ITV na Channel 10 walionesha iliyochakachuliwa lol! tusubiri tuone!!
Kuna haja ya CHADEMA Kuwa na TV Station jamaniiiiiiii!
 
Nisichokubaliana na baadhi yenu humu ni hili la WATANZANIA kufa kwa malengo ya KISIASA kama ilivyotokea Arusha na kabla ya hapo Pemba. Hakuna kifo kinachokubalika lakini hili la vifo vya kisiasa halina TIJA wala maana yoyote kwa Mtanzania wa kawaida. Ni afadhali Mtanzania afe kwa kudai AJIRA, kulalamikia bei ya kilo ya unga, bei ya mkate, bei ya umeme, bei ya maji, karo kubwa za shule, huduma mbaya za elimu kwenye mashule ya UMMA na mambo yanayofanana na hayo.
Tusiendelee kuua watu wetu kwa malengo ya KISIASA ambayo hayawabadilishii lolote watu wetu. Wakati wa kampeni, Dr Slaa alisisitiza mara kwa mara juu ya kutomwaga damu ya Watanzania ili aende IKULU. Ni nini kinafanyika sasa?

Mkuu wacha kujikanyaga kanyaga wewe.

Kama unajua unachokisema, huwezi kupinga mtanzania kuuwawa kwa masuala ya kisiasa then unaunga mkono mtu huyo huyo kuuwawa akidai huduma kamam ulivyoziorodhesha.

Kama ungejiruhusu bongo yako kufikiria vizuri ungegundua kwamba hizo huduma zote unazotaja kuanzia ajira, bei ya unga, bei ya mkate, bei ya umeme, bei ya maji, karo kubwa za shule, huduma mbaya za elimu kwenye mashule ya umma na mengine yanayofanana na hayo yanaunganishwa au kufanyika kwa kupitia kiranja wao mmoja tu anaitwa siasa.
Siasa haijaacha jambo lolote linalohusiana na ustawi wa jamii hapa tanzania kama ilivyo duniani kwa nchi za wenzetu.

Nadhani ukajipange, uje kivingine labda unaweza kusomeka, lakini hadi hapo hakuna kitu cha maana ulichozungumza.
 
Issues siyo video wala namna police walivyofanya kudhibiti uhuni wa Chadema uliokuwa kwenye cover la maandamano. Issue ni IQ ya viongozi wa Chadema kulazimisha maandamano ili hali wakijua hayo madhara kuwa yangetokea. Kwa sasa hatuhitaji kuona madhara kwenye CD. Ni upuuzi mtupu. Tutahitaji kuona viongozi wa Chadema wanachuliwa hatua stahiki za kisheria kukomesha kundi lingine la namna hiyo lisije ibuka. Mbona vyama vingine viko peace na waelewa sana, iweje Chadema iwe chanzo cha kila aina ya uhuni sasa hivi?! Hatuwezi tukawa na genge la wahamasishaji fujo, tena wanahamasisha kwa watu ambao ni destitute kabisa, hawana mbele wala nyuma na kuelewa chochote kinachoendelea Duniani.
Nadhani sasa hivi huna adabu kabisa hata kama ni uhuru wa kutoa mawazo kwenye jamvi hili lakini huwezi ukaja na pumba zako hapa eti tulioandamana Arusha hatuna akili na hatujielewi nadhani wewe bado uko kwenye enzi za ujima ambapo unafikiri sisi wana Arusha ni matahira na mazezeta kwamba tutaweza kuburutwa na wanasiasa kwa nini sasa CCM na pesa zenu zote za kuhonga na dola mkononi hamjaweza kabisa kutushawishi tukatulia,Kama unasema hatujiwezi sio CCM iliyotupeleka hapo ,wewe ni Mjinga sana Kanyafu,wakati watu wanazoa rasilimali za taifa kujineemesha ,watu wanapindisha sheria kubambika viongozi watakao linda maslahi yao hapo Arusha wewe unabariki,Nadhani mumechelewa sana Wananchi tumeamka hatuhitaji wana siasa kutuhamasisha tumehamasika wenyewe kudai haki zetu
 
Nisichokubaliana na baadhi yenu humu ni hili la WATANZANIA kufa kwa malengo ya KISIASA kama ilivyotokea Arusha na kabla ya hapo Pemba. Hakuna kifo kinachokubalika lakini hili la vifo vya kisiasa halina TIJA wala maana yoyote kwa Mtanzania wa kawaida. Ni afadhali Mtanzania afe kwa kudai AJIRA, kulalamikia bei ya kilo ya unga, bei ya mkate, bei ya umeme, bei ya maji, karo kubwa za shule, huduma mbaya za elimu kwenye mashule ya UMMA na mambo yanayofanana na hayo.
Tusiendelee kuua watu wetu kwa malengo ya KISIASA ambayo hayawabadilishii lolote watu wetu. Wakati wa kampeni, Dr Slaa alisisitiza mara kwa mara juu ya kutomwaga damu ya Watanzania ili aende IKULU. Ni nini kinafanyika sasa? -

WE WILDCARD! KWELI KICHWANI ZIMOOOO??? YAANI HADI UMRI HUU HUJUI KUKONECT PROCESS YA SIASA NA MAISHA YA KILA SIKU YA MWANANCHI? MODS - PLEASE SCRUTINISE VYETI VYA HII KICHWA!
 
Nisichokubaliana na baadhi yenu humu ni hili la WATANZANIA kufa kwa malengo ya KISIASA kama ilivyotokea Arusha na kabla ya hapo Pemba. Hakuna kifo kinachokubalika lakini hili la vifo vya kisiasa halina TIJA wala maana yoyote kwa Mtanzania wa kawaida. Ni afadhali Mtanzania afe kwa kudai AJIRA, kulalamikia bei ya kilo ya unga, bei ya mkate, bei ya umeme, bei ya maji, karo kubwa za shule, huduma mbaya za elimu kwenye mashule ya UMMA na mambo yanayofanana na hayo.
Tusiendelee kuua watu wetu kwa malengo ya KISIASA ambayo hayawabadilishii lolote watu wetu. Wakati wa kampeni, Dr Slaa alisisitiza mara kwa mara juu ya kutomwaga damu ya Watanzania ili aende IKULU. Ni nini kinafanyika sasa? -

WE WILDCARD! KWELI KICHWANI ZIMOOOO??? YAANI HADI UMRI HUU HUJUI KUKONECT PROCESS YA SIASA NA MAISHA YA KILA SIKU YA MWANANCHI? MODS - PLEASE SCRUTINISE VYETI VYA HII KICHWA!

The Following User Says Thank You to kweleakwelea For This Useful Post:

Mwita Maranya (Today)​
 
Nadhani sasa hivi huna adabu kabisa hata kama ni uhuru wa kutoa mawazo kwenye jamvi hili lakini huwezi ukaja na pumba zako hapa eti tulioandamana Arusha hatuna akili na hatujielewi nadhani wewe bado uko kwenye enzi za ujima ambapo unafikiri sisi wana Arusha ni matahira na mazezeta kwamba tutaweza kuburutwa na wanasiasa kwa nini sasa CCM na pesa zenu zote za kuhonga na dola mkononi hamjaweza kabisa kutushawishi tukatulia,Kama unasema hatujiwezi sio CCM iliyotupeleka hapo ,wewe ni Mjinga sana Kanyafu,wakati watu wanazoa rasilimali za taifa kujineemesha ,watu wanapindisha sheria kubambika viongozi watakao linda maslahi yao hapo Arusha wewe unabariki,Nadhani mumechelewa sana Wananchi tumeamka hatuhitaji wana siasa kutuhamasisha tumehamasika wenyewe kudai haki zetu

Kuna watu bado hadi muda huu wanaburuzwa kwa kila jambo wanalotaka kufanya.

Wanajiita wako huru ilihai hawana jeuri ya kuamua juu ya mustakabali wa uogozi wa maeneo yao mtaa hadi taifa, kwao hao kila wanachofanya ccm na serilaki yake ndio sahihi lakini wakiona chama kingine kinajaribu kuwazindua watanzania ndio wanakuja hapa na maneno mbofu mbofu.
 
• LENGO NI KUJIBU ‘UCHAKACHUAJI’ WA POLISI

na Betty Kangonga




CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kinaandaa mikanda ya video itakayoonyesha matukio yote yaliyotokea wakati wa vurugu zilizozaa maafa wakati wa maandamano ya wanachama wa chama hicho katika Jiji la Arusha mwanzoni mwa mwezi huu.

Hatua hiyo ya Chadema kuandaa mikanda ya tukio hilo inakuja kama majibu ya kile kilichofanywa na Jeshi la Polisi ambalo kwa siku kadhaa wiki iliyopita lilisambaza katika vituo vya televisheni video za matukio ya Arusha ambazo zimezusha manung’uniko ya chini kwa chini kutoka kwa wananchi wa Arusha na ndani ya chama hicho cha upinzani.

Katika kujibu mapigo ya polisi, chama hicho kimesema hakina la kuficha kama walivyofanya viongozi wa jeshi hilo, badala yake wataonyesha tukio zima kabla, wakati na baada ya mkutano wao uliofanyika kwenye viwanja vya NMC Januari 5 mwaka huu.

Mgogoro kati ya polisi na Chadema ulitokana na maelekezo tofauti ya kutofanya maandamano kwa mujibu wa amri ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) iliyotolewa saa chache kabla ya kuanza kwa maandamano hayo yaliyosababisha jeshi kutumia risasi za moto na mabomu kuwatawanya waandamanaji hao.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Willibrod Slaa alisema kwa sasa wanakamilisha mkanda huo ambapo utatolewa kwa waandishi wa habari na umma wakati wowote kuanzia leo.........................Inaendelea

Source:Tanzanaia Daima
 
Sijui huo mkanda wa Chadema utaonyesha madudu yote waliofanya polisi? Maana jamaa walikuwa wanapiga utadhani wanapambana majambazi ingawa majambazi wenyewe wanawakimbiaga.
 
Back
Top Bottom