Dk. Slaa awapagawisha wananchi

Dk. Slaa awapagawisha wananchi

sijui nini

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2010
Posts
2,553
Reaction score
1,292
SIKU moja baada ya mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, kunadi sera zake kwa njia ya mdahalo uliokuwa ukirushwa hewani moja kwa moja na kituo cha televisheni cha ITV, umeonekana kuwapagawisha watu wa rika mbalimbali mitaani.

Hatua ya Dk. Slaa kunadi sera hizo kwa ufasaha kumewafanya wananchi wa rika mbalimbali kukunwa nazo, ambapo jana walionekana kukaa vikundi vidogo vidogo kwa ajili ya mhadahalo huo na kueleza namna wanavyomkubali kiongozi huyo.

Alipotembelea katika maeneo mbalimbali ya Mivinjeni-Kurasini, mwandishi wa habari hizi alikuta wananchi wakiwa katika vikundi na kujadili yaliyokuwa yakizungumzwa naye.

"Si siri, Dk. Slaa ndiye anayefaa kuwa rais wa nchi, si ulimcheki namna alivyokuwa akizungumza kwa umakini bila kutetereka," alisema John Macha.

Naye Peter Stanley, alisema sera za mgombea huyo ni nzuri na ikiwa zitatekelezwa kwa vitendo ikiwa kiongozi huyo atafanikiwa kutawala nchi ataiweka mahali pazuri tofauti na ilivyo sasa.

"Mi namkubali sana huyu jamaa, kabla ya kufika hapa aliibua mambo mengi ambayo yalitusaidia kuyajua mambo mbalimbali yanayofanywa na wakubwa wetu, hivyo tafadhali jamani tusimfanyie mzaha," alisema Rajabu Jumanne.

Naye Fidelis Mtangi, alisema watu kama Dk. Slaa ndio wenye kuhitajika nchini kwani wataiwezesha Tanzania kufika mahali pazuri na kuondokana na hali ya kutokuwa na maendeleo iliyopo sasa.

"Dk. Slaa anazungumzia masuala yake kwa kutaja vitu vya msingi na vichache sana, bila kusoma mahali popote, si kama mpinzani wake mkubwa wa CCM,

…anaweza kuzungumzia juu ya uboreshaji wa huduma ya afya na elimu na akaeleza kwa kifupi sababu ya serikali kufanya hivyo, namna ya kutekeleza hilo na muda wa kutekeleza. Lakini mpinzani wake amefikia hatua akikuta hospitali ambayo ina hadhi ya hospitali ya wilaya anaahidi itakuwa ya mkoa au ya rufaa," alisema Mtangi.

Naye Daudi Mwakalinga kutoka mkoani Iringa, aliiambia Tanzania Daima kwa njia ya simu kuwa ni wazi Dk. Slaa ametambua uelewa wa wananchi wake wanahitaji nini na yeye kama mgombea amefafanua kwa ufasaha na kwa hoja inayokubalika.

"Watu hawahitaji mgombea kuzungumzia ujenzi wa barabara inayojengwa wakati watu wanaiona kwa macho, watu hawataki mgombea kuzungumzia vitu vinavyofanyika, ambavyo vimetengewa bajeti ya serikali, kwa kuwa bajeti hiyo inapitishwa mwaka hadi mwaka na wabunge wanahusika nayo, hivyo haina maana ya mgombea kuweka kwenye ahadi yake," alisema Mwakalinga.


CHADEMA::israel::israel:
CCM: 😛eep:😛eep:
 
"Watu hawahitaji mgombea kuzungumzia ujenzi wa barabara inayojengwa wakati watu wanaiona kwa macho, watu hawataki mgombea kuzungumzia vitu vinavyofanyika, ambavyo vimetengewa bajeti ya serikali, kwa kuwa bajeti hiyo inapitishwa mwaka hadi mwaka na wabunge wanahusika nayo, hivyo haina maana ya mgombea kuweka kwenye ahadi yake," alisema Mwakalinga.

Hapo ndipo Jk aliachia ngazi za kutawala.....................
 
kesho naanza safari ya kwenda Mwanza kwa lengo moja nalo ni kupiga kura ili kuuondoa utawala wa kiimla nchini kwangu

Hon.dk Slaa ndo Rais wangu. sina utani juu ya hili
 
kesho naanza safari ya kwenda Mwanza kwa lengo moja nalo ni kupiga kura ili kuuondoa utawala wa kiimla nchini kwangu

Hon.dk Slaa ndo Rais wangu. sina utani juu ya hili

Pepoziiiiiiiiiii...........................................
 
Mie hata kama nitakuwa na drip ya malaria nitaweka ki-memo ili docta aruhusu nikapige kura na drip yangu. Sitaki Dr. Slaa akose kura yangu.


 
Mie hata kama nitakuwa na drip ya malaria nitaweka ki-memo ili docta aruhusu nikapige kura na drip yangu. Sitaki Dr. Slaa akose kura yangu.


Jamani hakikisheni kuwa wazazi, watoto, wajomba na jamaa wote kuwa wanampigia kura Dr. Slaa tafadhali hiki ni kitu cha muhimu sana. Kura zetu zisigawanyike.
 
Wananchi sasa wameelewa nini wanataka!!!

God bless Tanzanians.

VOTE FOR CHADEMA
 
Nitasafiri ijumaa kwenda dar kwa ajili ya kujipanga kumpigia kura Slaa (PhD) na kuilinda kura yangu. Mimi na rafiki zangu tumeamua kufanya hivyo ili kuongeza kura zetu kwenye ushindi huu mkubwa wa watanzania wa kutafuta kuikomboa nchi yetu.

usisahau nina zaidi ya kura za CCM nilizozipeleka CHADEMA mwaka huu. Nikiwa kama mmoja wa wana-CCM waasi kwani hata kadi niliipoteza na wala sihitaji kuwa nayo tena, nimeamua kuondoka na watu wengi ili yale majigambo ya ccm ya kuwa na wanachama wengi yathibitike ni uongo. wanannihesabu mimi kuwa mmoja wao ilhali si mmoja wao kwa kuwa sikuwaaga na wala sijabisha hodi chadema, isipokuwa moyo wangu umeenda huko na matumaini mapya ya nchi ni Slaa (PhD) na si Kikwete (BA)
 
Kwa kweli hata Ma-waitress/Mawaiter waliokuwa wanashudia... Mwanzoni walidhani ni Mipira ya Ughaibuni... Lakini walikuja-ng'amua ni Mdahalo... Walikuwa wampigie kura Kikwete lakini wamekata shauri... HAWADANGANYIKI!!!
 
Mimi, Mke wangu, Wadogo zangu wanne na mama ni Dr Slaa. Bado namshawishi mzee naye sasa ameanza kumkubali ze Dr! So count 7 votes from my family...wewe watakoma this year!
 
SIKU moja baada ya mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, kunadi sera zake kwa njia ya mdahalo uliokuwa ukirushwa hewani moja kwa moja na kituo cha televisheni cha ITV, umeonekana kuwapagawisha watu wa rika mbalimbali mitaani.
Hatua ya Dk. Slaa kunadi sera hizo kwa ufasaha kumewafanya wananchi wa rika mbalimbali kukunwa nazo, ambapo jana walionekana kukaa vikundi vidogo vidogo kwa ajili ya mhadahalo huo na kueleza namna wanavyomkubali kiongozi huyo.
Alipotembelea katika maeneo mbalimbali ya Mivinjeni-Kurasini, mwandishi wa habari hizi alikuta wananchi wakiwa katika vikundi na kujadili yaliyokuwa yakizungumzwa naye.
"Si siri, Dk. Slaa ndiye anayefaa kuwa rais wa nchi, si ulimcheki namna alivyokuwa akizungumza kwa umakini bila kutetereka," alisema John Macha.
Naye Peter Stanley, alisema sera za mgombea huyo ni nzuri na ikiwa zitatekelezwa kwa vitendo ikiwa kiongozi huyo atafanikiwa kutawala nchi ataiweka mahali pazuri tofauti na ilivyo sasa.
"Mi namkubali sana huyu jamaa, kabla ya kufika hapa aliibua mambo mengi ambayo yalitusaidia kuyajua mambo mbalimbali yanayofanywa na wakubwa wetu, hivyo tafadhali jamani tusimfanyie mzaha," alisema Rajabu Jumanne.
Naye Fidelis Mtangi, alisema watu kama Dk. Slaa ndio wenye kuhitajika nchini kwani wataiwezesha Tanzania kufika mahali pazuri na kuondokana na hali ya kutokuwa na maendeleo iliyopo sasa.
"Dk. Slaa anazungumzia masuala yake kwa kutaja vitu vya msingi na vichache sana, bila kusoma mahali popote, si kama mpinzani wake mkubwa wa CCM,
…anaweza kuzungumzia juu ya uboreshaji wa huduma ya afya na elimu na akaeleza kwa kifupi sababu ya serikali kufanya hivyo, namna ya kutekeleza hilo na muda wa kutekeleza. Lakini mpinzani wake amefikia hatua akikuta hospitali ambayo ina hadhi ya hospitali ya wilaya anaahidi itakuwa ya mkoa au ya rufaa," alisema Mtangi.
Naye Daudi Mwakalinga kutoka mkoani Iringa, aliiambia Tanzania Daima kwa njia ya simu kuwa ni wazi Dk. Slaa ametambua uelewa wa wananchi wake wanahitaji nini na yeye kama mgombea amefafanua kwa ufasaha na kwa hoja inayokubalika.
"Watu hawahitaji mgombea kuzungumzia ujenzi wa barabara inayojengwa wakati watu wanaiona kwa macho, watu hawataki mgombea kuzungumzia vitu vinavyofanyika, ambavyo vimetengewa bajeti ya serikali, kwa kuwa bajeti hiyo inapitishwa mwaka hadi mwaka na wabunge wanahusika nayo, hivyo haina maana ya mgombea kuweka kwenye ahadi yake," alisema Mwakalinga.


CHADEMA::israel::israel: CCM: 😛eep:😛eep:

Hayo ndo tulikuwa tukitaka watu waelewe nani anaupendo wakweli na watanzania siyo upendo wamafisadi tuu!
 
Kutambua kuwa una tatizo kuna kupa uwezo wa kulichambua na kulitafutia dawa ama jawabu lake. Dr Slaa ametambua nini matatizo ya Tanzania, ameweza kuyachambua kwa kina na ameweza kupata majibu ya matatizo hayo. Hivyo itakuwa ni jambo la hekima sana kwa Watanzania kumpa Dr Slaa nafasi ya kuwa Kiongozi wetu wa juu ili aweze kutatua matatizo yetu. Ni jambo la aibu na kusikitisha sana kuona Jakaya hajui kwanini Tanzania ni masikini pamoja na kuwa amekuwa Raisi wetu kwa muda wa miaka mitano. Hii inanipa jawabu kwamba Jakaya hajui anafanya nini Ikulu. Watanzania hatuna sababu ya kumrudisha Jakaya Ikulu, aende Bagamoyo ama Msoga kulima mananasi.
 
Kutambua kuwa una tatizo kuna kupa uwezo wa kulichambua na kulitafutia dawa ama jawabu lake. Dr Slaa ametambua nini matatizo ya Tanzania, ameweza kuyachambua kwa kina na ameweza kupata majibu ya matatizo hayo. Hivyo itakuwa ni jambo la hekima sana kwa Watanzania kumpa Dr Slaa nafasi ya kuwa Kiongozi wetu wa juu ili aweze kutatua matatizo yetu. Ni jambo la aibu na kusikitisha sana kuona Jakaya hajui kwanini Tanzania ni masikini pamoja na kuwa amekuwa Raisi wetu kwa muda wa miaka mitano. Hii inanipa jawabu kwamba Jakaya hajui anafanya nini Ikulu. Watanzania hatuna sababu ya kumrudisha Jakaya Ikulu, aende Bagamoyo ama Msoga kulima mananasi.
Dr.anafaa,mimi na nyumba yangu tutamchagua.
 
ambaye atapigia kura ccm katika nyumba yangu nikigundua, atakula polisi!
 
nimeshau na kazini kwangu,wafanyakazi wa kampuni yangu wako kama 89 wote wanaenda kwao lengo ni kuhakikisha slaa anashinda, potelea mbali acha kampuni ipate hasara
 
frm nw na kuendelea,rais wa awam ya 5 wa tz ni Dr.wilbroad slaa,
kwa m2 muelewa huhitaji kuhoji,kikwete aende kufanya ufisad na akina rosti tamu ya ndizi (rostam aziz)
 
Back
Top Bottom