Dk. Slaa aibuka na Nyaraka za SIRI

Ritz, hapo kwenye rangi nyekundu ulitaka kusema nini? au ndio matatizo yako ya uelewa mdogo? Hata hivyo usipate shida sana kwani kama cheo tayari ninacho, kwa vile situmii jina langu halisi hutafahamu. Vumilia uchungu ndugu yangu, wenzio pamoja na kuwa na vyeo ndani ya serikali ya magamba hatupo tayari kabisa kuwaunga mkono mafisadi.

Hata mie hunijui usipate shida sana...kwa hiyo nyie ndio mnamuangusha JK mnauza wanyama wetu nje ya nchi.
 
watanzania tunasoma habari zako dr slaa kisha tunaenda kulala lakini iko siku tutaingia barabarani..
 
Hata mie hunijui usipate shida sana...kwa hiyo nyie ndio mnamuangusha JK mnauza wanyama wetu nje ya nchi.
Pole sana Ritz, wanaouza wanyama hufanya kazi ya ziada ya kujipendekeza kwa Jk kama unavyofanya wewe! sisi tupo hapa uwanjani kuwaumbua na sio kuwatetea kama unavyofanya wewe.
 
Wewe kweli osokoni Mbowe anavyompa JK mkono au siku ile Chadema walivyokwenda Ikulu wote walikuwa wanampa mkono JK walikuwa wanashukuru nini? Vipi zile kontena zipo wapi?[/QUOTE]

Si umesema vilikutwa vipodozi ndani ya zile kontena! sasa vipodozi hupelekwa wapi? Kamuulize Salma anajua!
 
Sasa hawa mafisadi wa tanzania wa ajabu sana...kila wakifanya ufisadi wanaandika na nyaraka za kuonyesha kila kitu walichofanya na mtandao wao.na wakilipana wanaandikiana na risiti ndo maana huyu jamaa anakamata nyaraka kiulaini sana.
SASA SI AZIWEKE HADHARANI TUWAONE HAO WEZI
 
Pole sana Ritz, wanaouza wanyama hufanya kazi ya ziada ya kujipendekeza kwa Jk kama unavyofanya wewe! sisi tupo hapa uwanjani kuwaumbua na sio kuwatetea kama unavyofanya wewe.

Wewe upo humu JF ni kujipendekeza tu na kumtetea Slaa na Chadema...
 
Dr. Kaamua kujiundia CIA na KGB binafsi ambayo inachunguza, inathibitisha, na kujiridhisha kiushahidi alafu ina report directly kwa wananchi! Ni nomaaaaaa! Ole wako uwe muovu alafu juzi hukuchangia kwenye harambee ya CDM jina lako la kwanza kutajwa. Bora Filikunjombe kajiwahi mapema!

Una maana gani hebu nieleweshe. Una maana CAHDEMA wanachukua fedha kutoka kwa mafisadi kupitia harambee ili kuficha maovu yao au?
 
Jumatano, Agosti 15, 2012 06:11 Na Mwandishi Wetu, Mikumi

dk.%20slaa.jpg
Dk. Wilbrod Slaa

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willbrod Slaa, ameibuka na kusema anazo nyaraka za siri, kuhusu mauaji ya faru yaliyofanyika hivi karibuni katika Hifadhi ya Serengeti, mkoani Mara.

Dk. Slaa, alisema nyaraka alizonazo zinaonyesha kuna mtandao mkubwa wa ujangili, unaohusisha vigogo wakubwa serikalini, watumishi wa vyombo vya dola, askari polisi na watumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo juzi, wakati akiwahutubia mamia ya wananchi wa vijiji vya Kata ya Malinyi, Mikumi na Ruaha.

Alisema nyaraka hizo, zinaelezea kiundani suala zima la mtandao wa ujangili.

Alisema mauaji ya wanyama adhimu faru, yaliyofanyika katika Mbuga ya Serengeti, ni dalili ya hujuma kubwa katika sekta ya maliasili ambazo zinafanywa na mtandao huo.

Alisema kumekuwapo na tabia ya kuwanyamazisha wabunge wanaotaka kupanua mjadala wa ufisadi mkubwa unaoendelea kuteketeza maliasili za nchi, wakiwamo twiga na faru.

“Naliomba Bunge kuacha kuminya mijadala, inayolenga kuibua matatizo ambayo tunaweza kuyatafutia tiba katika sekta mbalimbali za uchumi na maendeleo ya nchi… ninashangazwa kuona Serikali inaendelea kufumbia macho mtandao huo.

“Watanzania wenzagu wa Ulanga, hii ndiyo hali halisi namna ambavyo Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imetufikisha hapa tulipo leo, ufisadi umetamalaki kila mahali, leo hapa ninazo mkononi kwangu nyaraka za siri zinazoelezea namna ambavyo faru wetu, wale wanyama adimu walivyouawa hivi karibuni huko Serengeti.

“Kwa mwananchi wa kawaida, inaweza kuwa vigumu kuelewa haraka umuhimu wa faru katika masuala ya uchumi.

“Kwa wale wanaofuatilia Bunge, watakuwa wameona juzi Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema), alivyoambiwa bungeni baada ya kuibua suala hili la kuuawa kwa faru…mimi sitaki kuingia huko kwenye kamati yao na kile wanachofanya.

“Lakini nyaraka nilizonazo hapa zinaeleza bayana namna ambavyo faru hao waliuawa, huku wahusika, wakiwemo askari polisi majina wametajwa hapa, maliasili zetu wakiwemo wanyama, ziko hatarini kumalizwa kutokana na uzembe wa serikali kulea ufisadi.

“Kama Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki anaona kuna mahali angeweza kuchukua hatua, lakini anashindwa kwa sababu kuna watu wengine wanapaswa kuchukua hatua zaidi,” alisema.

Pamoja na mambo mengi, ameiomba Serikali kuwachukulia hatua kali wale wanaothibitika kufanya vitendo vya ubadhirifu wa mali za umma
MTU asiyeweza kutunza SIRI hafai kuwa Rais wa nchi maana aweza kuweka peupe SIRI za nchi.
 
Hana jipya, siasa majitaka zimepitwa na wakati. Sasa kuna siri ipi hapo na ujangili unajulikana kuwa upo toka wakati wa Nyerere na kila siku majangili wanashikwa, kama anawajuwa alete ushahidi wakamatwe, au yeye sio polisi jamii?

Mijitu mingine bwana, hata sijui inafikiri nini, inaona Watanzania wote wamelala? anataka kuhalalisha mkopo wa nyumba ya Josephine?
 
dr slaa ebu wataje hao vigogo tuwajue sio tu kusema unazo nyaraka za siri dr slaa, ulishawai kutuambia kuwa kuna umekamata kontena mbili umezikamata tunduma zimejaa karatasi za kupigia kura kutoka china zilipolikuja kufunguliwa na polisi mbele ya viongozi wa chadema wakakuta vipodozi dr slaa akawakimbia waandishi wa habari...tumeishakuzoea.

magamba presha inashuka na kupanda, kuhusu 2015 mapenzi ya mungu yatimizwe!
 
Dr Slaa ebu wataje hao vigogo tuwajue sio tu kusema unazo nyaraka za siri Dr Slaa, ulishawai kutuambia kuwa kuna umekamata kontena mbili umezikamata Tunduma zimejaa karatasi za kupigia kura kutoka China zilipolikuja kufunguliwa na polisi mbele ya viongozi wa Chadema wakakuta vipodozi Dr Slaa akawakimbia waandishi wa habari...tumeishakuzoea.
Aliwataja pale Mwembeyanga mbona wote walinywea? Mpaka leo hawajaenda mahakamani kama walivyokuwa wanatishia.
Alimtaja Ridhwani naye akajikurupusha kuwa atampeleka mahakamani mpaka leo nduhu! Awataje ili iweje?
 
Back
Top Bottom