Kusema pia uko katikati sikuelewi mkuu maana my question was so specific kuwa unakubaliana na kauli ya kuwa "acha ninyooshe nchi kwanza" ni sawa???
Irrespective ya mchakato ulikuaje au utakuaje je ni sawa rais kutoa kauli kauli kuwa katiba mpya sio muhim??? JIBU HILI
2.) Umesema wenzako walikusaliti am sure unawalenga kina marando and company ila nikuulize katiba ni ya wananchi au wanasiasa?? Kma ni ya wananchi kwanini mzigo uubebeshe vyama vya upinzani sio wananchi??
Pia una doubt vp elimu ya watanznaia na wakati literacy level ya mwaka 92 na sahivi imekuwa zaidi na elimu imeongezeka tofauti na miaka yenu je ni elimu gani unayotaka ambayo inatosha wananchi kudai katiba mpya?? Mbona walitoa maoni mazito yaliopelekea rasimu ya warioba kuwa ya kipekee sana je elimu gani unataka??
Pia kuhusu mchakato nani aliesema watu wanang'ang'ania mfumo wa bunge la katiba?? Na wakati juzi tu hapa lowasa katoa ushauri kuwa mchakato usihusishe wanasiasa rather uhusishe wataalam wasio na upande that means mawazo mapya yaliletwa je bado hutaki katiba mpya inhawa mawazo mapya kma haya yameletwa???
Hayo ya mchakato yanaweza badilishwa, coz sio constant au stagnant sasa nakuuliza je bado hakuna haja ya katiba mpya ???
Angalau umenisaidi kukionesha kile ambacho labd mimi ningekisema ningeonekana nina nongwa. Katiba ni ya wananchi si ya chama chochote cha siasa katika nchi yenye wanasiasa waungwana, wazalendo wanaoipenda nchi yao. Katika nchi ambayo wanasiasa wanajali matumbo yao, katiba ni ya kikundi ili waweze aidha kushiriki kula au iwawezeshe kuingia na kukaa madarakani.
Watanzania bado hawajaelimika na bado haijawa jamii yenye kuwajibika. Kuelimika ninakokuzungumzia mimi ni kuwa responsible, kufahamu kuwa mwananchi ndio mwenye nchi, mwenye haki ya kuhoji na kuuwajibisha uongozi. Jamii yenye kufahamu kuwa uchaguzi ni kasehemu kamoja tu ka demokrasia, afahamu kuwa demokrasia ina segmeny nyingine nyingi tu. Hatuna mtanzania anayesimamia uwazi, anayesimamia usikivu, uwajibikaji wa serikali na viongozi. Jamii ambayo haina check and balance institution katika kusimamia mambo muhimu ikidai katiba ni bure kwani bado haitaweza hata kuisimamia hiyo katiba yenyewe.
Jambo muhimu kwa sasa wacha ainyooshe nchi, wacha watu watie akili na adabu, wakitia akili na adabu watayatafuta hayo niliyoyasema hapo juu na hapo tutapata katiba ya maana.
Sipendi kujadili majina ya wanasiasa hasa hawa wanasiasa 'wachumia tumbo' wa nchi hii. Wakati katiba ikidaiwa miaka ya 1990 Lowasa alikuwepo. Lakini kwa vile kwake katiba sio ya wananchi ni ya kikundi akabaki na kikundi chake ili waendelee kutawala. Mchakato wa katiba ulipokuja alikuwepo lakini hakusema kama huo mchakato si sahihi. Kwa nini? Jibu ndio hilo hilo kwake katiba si ya wananchi bali ya kikundi cha watu. Akateuliwa kuwa mbunge katika Bunge la katiba, akakubali uteuzi na akaingia bungeni. Katika kupiga kura sina hakika kama alipiga au la lakini chama chake kilisimamia msimamo wake na kikashinda. Maisha yakaendelea, akaendelea na chama chake na akachukua fomu akiomba nafasi yakugomea urais kupitia chama chake na ofcouse baadae uenyekiti wa chama. Labda alikuwa na dhamira yakurudisha katiba ya wananchi si eti eeenh? Labda. Kilichotokea ni historia!
Swali kwa wanasiasa wengine wa upinzani! Je wao hawakujua kuwa ule mchakato si sahihi? Walilisema hilo kabla? Walipoitwa kuubariki ule mchakato wao walifanyaje? Walikimbilia zile posho au walikataa tangu mwanzo? Nani aitishe mchakato tofauti na huo? CCM? Ili iweje? Waondoke madarakani? Jamani tujitahidi kufikiri jamani!
Mimi nimekuwepo nao hao wapinzani na CCM inawajua uzuri ndio maana hawawasumbui, wanajua na kufahamu udhaifu wao, wanawapa chambo kinono, waroho wanakifuata baadae hao wanavuliwa. Mara nyingi hushtuka wakati wameshapotea na tabia hii haikuanza leo. Katika mazingira haya ya wananchi wanaofichwa ukweli na pande zote za watawala na wapinzani, katika mazingira haya ya kutotaka kuwajibika kwa mwanasiasa yeyote wa tawala wala wa upinzani, kwa kweli tumuache jamaa anyooshe nchi, watu waone umuhmu wa kuambiana ukweli pasipo kuoneana haya, umuhimu wa kuwajibika na tuache kuifanya nchi kijiwe cha Mafioso. Eti ubaya unajadiliana na wema? Wapiga dili duniani kote hawajawahi kuwa marafiki wa kweli wa wananchi, wanajipaka tu poda ya urafiki wa kinafiki. Ukiamua kufumbua macho na ukatazama kwa umakini utaona.