Dk Kitima aitabiria mabaya CCM mbele ya Wassira

Kitima lazima atambuwemchango wa ccm kwa watanzania na cy kwa maslahi yake. Hakuna kama ccm labda kama ni ushabiki wa siasa sawa . Mfumo tuu wa ccm ni kielelezo tosha kuwa huwezi kilinganisha na cdm yake hy.
Cbezi upinzani lkn nauona kama bd haujakomaa zaidi ya kupiga kelele.
 
Kama ni kweli Dr. Kitima hakumkaribisha TL kwa sababu hajafanya lolote jimboni mwake, basi ni dhahili nchi yetu ina matatizo makubwa kuliko tuynavyodhani!

Mkuu nahisi kuna kitu nyuma ya pazia, ijapo kuwa sielewi ni kitu gani, but time will tell. Endapo wewe ni mfuatiliaji wa speech za Dr. Kitima, unaweza ng'amua ya kuwa huyu jamaa either ana chuki binafsi au Personal conflict na Kamanda Tundu Lissu.
 
Kitima lazima atambuwemchango wa ccm kwa watanzania na cy kwa maslahi yake. Hakuna kama ccm labda kama ni ushabiki wa siasa sawa . Mfumo tuu wa ccm ni kielelezo tosha kuwa huwezi kilinganisha na cdm yake hy.
Cbezi upinzani lkn nauona kama bd haujakomaa zaidi ya kupiga kelele.

Mfumo upi unao uongelea wewe? au ndo una kurupuka kutoka usingizini ?
 
Dk Kitima... Very wise man, Mwl wa Busara

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Bavicha ni janga la Taifa.

Hata mpangilio wa uandishi ni kizungumkuti achilia mbali kujenga hoja kimantiki.

Hiki ulichokiandika ndiyo nini?. Pay attention kwanza kwenye elimu ili uelimike.
UVCCM je? Kutongozana kwenda kula raha Zanzibar au kusema raisi hatakaa atoke kaskazini ndo akili?!!!
 
Nyambiri anaposema upinzani utaambukiza kulalamika kwa wananchi, yeye haoni umuhimu wa kuiambia CCM iache uonevu kwani itazaa taifa la waonevu?!!!
 
Ni kwamba watawla tulionao kweli ni janga la kitaifa na bahati nzuri nilikuwa kwenye ukumbi si Wassira wala Nyangine mwenye unafuu na hii ni kutokana na kulewa mdarakan wakidhani kwmba hawatatoka madarakani ni kukosa hekima.Kama historia ilivyo wahukumu wtawla wengine na wao wanakaribia mwisho,ila kiukweli inawauma kusikia ukeli huo kwamba wanaelekea mwisho na ukizingatia ni takribani mwaka mmoja umesalia.:yell:
 

MAKAMU Mkuu wa Chuo cha Mtakatifu Augustine (SAUT) kilichoko mkoani Mwanza, Dk. Charles Kitima, ameitaka serikali ya CCM ijiandae kuondoka madarakani kwa aibu hata ikiiba kura.Dk. Kitima alitoa kauli hiyo jana mkoani hapa mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Steven Masatu Wasira, ambapo alisema CCM imeonyesha idhaifu mkubwa katika kusimamia baadhi ya mambo. Wasira na Dk. Kitima walikuwa kwenye mjadala wa Dira ya Maendeleo ya Serikali, uliofanyika mbele ya wanafunzi wa chuo hicho cha SAUT Nyegezi, jijini Mwanza. Dk. Kitima alisema licha ya Wasira kutokuwa fisadi na ni mwanafunzi mzuri wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alimtaka awaambie wenzake wajiandae kuondoka kwa aibu.


“Mfano mzuri, Singapore wao walianza kusimamia utalii, lakini serikali yetu ilikosea sana kutokutekeleza mambo ya uzalishaji. Na msipotekeleza hili, CCM mtaondoka madarakani.“Ulaji mkubwa wa fedha umeingia sekta ya elimu, hamtekelezi kwa vitendo sera na dira za taifa. Nasema msipobadilika serikali ya CCM itaondoka na hata mkiiba kura, lazima mtaondoka tu, tunawaandalia wapinzani,” alisema Dk. Kitima kisha ukumbi mzima ukamshangilia kwa nguvu. Dk. Kitima ambaye kitaaluma ni mwanasheria, alisema Rais Jakaya Kikwete anao mawaziri watatu tu ambao wana mrengo chanya wa kuikomboa nchi. Alibainisha kuwa kitendo cha serikali kuruhusu wawekezaji kuingia nchini na kudharau wazawa na mali zao hilo litakiangusha chama tawala.

Alisema kwa sasa katika vikao vya Bunge, hoja za msingi zinapingwa huku mtoa hoja akizomewa, lakini mambo ya kipuuzi ndiyo yanayoshabikiwa na wabunge wengi. Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Steven Masatu Wasira, amewashukia watumishi wote wanaojihusisha na ubadhirifu wa mali za nchi na kusema lazima watu hao wahenyeshwe kwa kuchukuliwa hatua bila kuonewa aibu. Wasira ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi, alianza kwa kusema: “Mimi nachukizwa sana na wanaoiba mali za nchi. Sipendi wizi na siwezi kuiba wala simung’unyi maneno kusema hili.” Alisema wapo baadhi ya watumishi wanapoingia kwenye ajira kazi yao ni kuanza kuiba badala ya kujenga taifa, jambo ambalo ni hatari kwa maendeleo ya nchi, na kwamba fedha za EPA zilizorudishwa na wezi na zimetumika kuinua kilimo.

Waziri Wasira alisema kupungua kwa uadilifu hapa nchini ni tatizo kubwa, na linaweza kuleta mgogoro mkubwa na kudidimiza zaidi uchumi wa nchi, hivyo lazima kila Mtanzania awe muumini mzuri wa uzalendo. “Rasilimali zote za nchi lazima zitumike kuwanufaisha Watanzania wote. Na bila hivyo hakuna nchi. “Kupungua kwa uzalendo na uadilifu ni tatizo kubwa sana kwa nchi. Lazima tuenzi amani na upendo...ukishindwa kulinda na kuiheshimu Tanzania wakati na wewe ni Mtanzania hufai,” alisema Wasira. Alisema rasilimali zote yakiwemo madini, maziwa, utalii na nyinginezo nyingi ni vema zikageuzwa kuwa mali zinazonufaisha na kuleta maendeleo kwa wananchi na kwamba dira ya maendeleo ya taifa ni kuboresha fursa nyingi za kiuchumi.


Alisema ili kufikia malengo halisi, mpango wa serikali uliopo sasa ni kuboresha huduma za viwanda, reli, viwanja vya ndege, kilimo bora, bandari, maliasili, miundombinu na nishati.Kuhusu udini, Wasira alisema wamemeishi miaka 50 kwa amani, upendo na utulivu lakini sasa kuna chokochoko za baadhi ya watu ambao hawataki kuiona nchi ikitulia.Aliwataka wasomi, waandishi wa habari, wanasiasa, viongozi na waumini wa dini zote na makundi ya kijamii, kuhakikisha wanapigania kuendelea kumea zaidi uharibifu wa amani ya nchi, maana lazima kila Mtanzania aihurumie nchi.

Source: CHADEMA DIASPORA : CCM inakufa
 
hayo ni mawazo yake lakini jk aliwahi kuwaeleza watu kama hawa kuwa wanaosema ccm itakufa wataanza wao kufa.
 
jana niliiona hii taarifa huyu jamaa kitime ana guts kweli alimpasha wassira 1 on 1. wassira akavibrate uso kama simu ya mchina akaanza kujitetea eti yeye hajawai kuiba labda wenzake.
 
Dr. Kitima ni janga la taifa mfuatilieni hoja na mambo yake kwa makini utagundua madhaifu yake makubwa...
Kama ni kweli Dr. Kitima hakumkaribisha TL kwa sababu hajafanya lolote jimboni mwake, basi ni dhahili nchi yetu ina matatizo makubwa kuliko tuynavyodhani!
 
Nimegundua wanaJF wengi ni janga la taifa, hivi hamsomi hata alama za muda, Dr. Kitila alikuwa na maCCM, ili kubalance mambo ilibidi aume kidogo upande mmoja na baadae apigilie msumari upande wa pili.
 
Siamini kama Dr. Kitima aliyasema hayo kuhusu Tundu Lissu. kama kweli kasema hayo, nadhani amepotoka kwani atakuwa amezungumza kama mwanakijiji wa kawaida. Dr. Kitima asome katiba ya nchi ambayo imeainisha kazi za mbunge na kwa uchache ni kutunga sheria, kuisimamia serikali na kuiwajibisha. Sidhani katika hizo kazi za mbunge kama kuna eneo ambalo Tundu aliwahi kuwa mzembe hata mara moja.

Dr. Kitima aainishe ni aina gani ya maendeleo na kwamba Tundu Lissu angewaletea watu wa Singida kwa namna gani? Inawezekana kwa namna moja au nyingine anaweza akawa na kasoro lakini kwa vinawango vya kumrejea kama mbunge ambaye hafanyi chochote basi Dr. ktima analo lake jambo. Ufanisi wa mtu katika kutekeleza majukumu yake hupimwa kwa malengo yaliyowekwa kuendana na majukumu yake, hapo Dr. Kitiama alikuwa anarejea nini anaposema kuwa Mh. Tundu Lissu ameshindwa?

Dr. Kitima nakuambia kuwa ukigombea ubunge huko Singida huwezi kufikia hata 5% ya kazi alizofanya Tundu Lissu. Kama amemkosoa, tunakubali lakini sikubaliani na hoja za ukosoaji. Nakumbuka siku moja Tundu Lissu aliibana serikali bungeni siku moja, akiikosoa Halmashauri moja huko Singida kurejesha wizarani fedha za maendeleo ya elimu huku wananchi wakichangisha fedha kwa ajili ya maendeleo ya elimu. Nilivyoona Tundu Lissu alikuwa sahihi kwa sababu huwezi kufanya mchezo wa kitoto namna hiyo.

Acha uwongo we na uzandiki ni kweli Dr Kitima amenena sana kwani Tundu Lissu hakuna alichokifanya katika jimbo lake na hata mwenyewe anajua Hilo. Take my word katika wabunge wa upinzani atakae kuwa wa kwanza kuaga jimbo ni Lissu waulize wana Ikungi wote wanajua. Hajafanya lolote zaidi ya kuhamasisha wananchi wasichangie maendeleo ndio maana Ikungi ni ya mwisho kila kitu. Kati ya madiwani wote yy Ana mmoja tu na ni hovyo kweli kweli tena kichaa kabisa. Alidiriki kufyeka miguu ng'ombe wa wananchi hadi Lissu akamshangaa. Acheni ushabiki Lissu come 2015 hawezi kuwa tena mbunge. Kati ya madiwani 25 Chamdomo kina diwani mmoja tuu......Lissu Hana chake
 
Wamenena wengi kuwa mwisho wa ccm unakuja sasa nasibiri kuona vitendo na siyo maneno tu, nasubiri kuona kuzaliwa kwa Tz mpya, nasubiri kuona ukurasa mpya wa taifa hili tajiri wa rasilimali na masikini wa fedha na tegemezi wa mataifa mengine hata yale yasiyokuwa na rasilimali za kutosha kama sisi wananchi wake wakinufaika na rasilimali zake.
 
Aina ya uandishi wa namna hii ni matokeo ya uchakachuaji katika mfumo wa elimu yetu, haukuanza leo jamani ndio tuanze kuona madhara yake. Na hali ni mbaya kwa kweli ukikaa na mhitimu wa chuo kikuu wa miaka mitano hadi 7 iliyopita utashangaa na kujiuliza alikuwa anafundishwa nini, alikuwa akiandika nini katika mitihani, na mwalimu wake alikuwa akisahihisha nini hadi mtu huyu amehitimu degree ya daraja zuri tu!

Hali ni mbaya.
 
Mwanza
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino, Dk Charles Kitima amekitabiria kifo Chama Cha Mapinduzi kama kitaendelea na mtindo wa kuwanyima fursa wazawa katika maendeleo.

Akizungumza katika kongamano la kujadili amani na maendeleo na mpango wa miaka mitano wa kukuza uchumi na kuondoa umaskini nchini lililofanyika chuoni hapo jijini Mwanza, Dk Kitima alisema nchi haiwezi kufikia dira ya maendeleo ikiwa Serikali imeshindwa kutoa kipaumbele katika utawala mzuri wa rasilimali na wazawa:

"CCM isipojirekebisha itakufa mapema kama isipoipa kipaumbele sekta binafsi ya wazawa katika kusimamia rasilimali ya nchi.Tunataka rasilimali za nchi tusimamie wenyewe," alisema Charles Kitima.

Akizungumza mbele ya Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais, Uhusiano na Urtatibu, Steven Wassira aliyekuwa mgeni rasmi, aliongeza kuwa nchi itaendelea kwa kuwapa fursa wananchi wake.

Kwa upande wake Waziri Wassira alikiri kuwa umaskini wa Tanzania unasababishwa na kutokuwapo kwa uzalendo, kupungua kwa uadilifu na mfumo mbovu ya ufuatiliaji na utekelezaji wa mipango. "Uadilifu umekuwa mdogo sana kwa viongozi wetu wa leo. Mawazo yaliyotawala ni wizi tu na mimi sina mpango wa kuiba"alisema Wassira.

Hata hivyo Wassira alisema kutokuwa na uelewa tulikotoka nayo ni sababu kubwa kwa wananchi kutokujua maendeleo yaliyofikiwa kwa miaka 50 ya uhuru.

"Tanzania ni nchi tuliyoirithi ikiwa ni shamba tu hatukukuta kitu. Hapakuwa na barabara za kutosha, elimu haikupewa kipaumbele, kutoka wasomi wachache wa mwaka 1961 sasa kuna vyuo 44'' alisema.

Naye Mhadhiri wa Sheria chuoni hapo, Adelardius Kilange alisema tatizo la umaskini nchini linatokana na wananchi kukosa misingi imara ya itikadi ya siasa na uchumi wa jamii na kwamba ipo haja kwa Serikali kujipanga.

 
Kama Dk Kitima aliwahi kumzuia Lissu kufanya mhadhara hapo chuoni, hiyo inaweza kuwa sio kwa sababu ya kutokufanya chochote jimboni. Itakuwa dk Kitima ana malengo ya kisiasa baadaye, hawa jamaa wanatoka jimbo moja; dk Kitima asije akwa anataka kumdhoofisha Lissu ili apate upenyo.
Anyway, wote wawili ni wapiganaji na nawakubali haswa...na wahenga walisema mafahali wawili...
 
Back
Top Bottom