Dk. Kitila Mkumbo ajitambulisha rasmi ACT

Dk. Kitila Mkumbo ajitambulisha rasmi ACT

Akili kubwa awe nayo Mwigamba? Huyu aliyemteua mjinga mwenzake Limbu kuwa Mwenyekiti? Kama Mwigamba mnamwona ana akili kubwa basi ACT itakuwa kama NRA

nitajie kiongozi wa chadema mwenye akili kubwa
 
Kwa lugha nyingine unaweza ukasema hivyo isipokuwa udhoofu huo haujatokana na dhamira ya CDM bali umetokana na mbinu iliyotumiwa na CCM ambayo kwa kiasi imefanikiwa kudhoofisha upinzani...

Ukiweza kuwagawanya, basi utaweza pia kuwatawala
Kwenye hili Chadema walikosea...sitaki kuamini kuwa watu walio tayari kuongoza nchi walishindwa kulimaliza hilo la Zitto humo ndani ya chama kimyakimya bila kuleta sintofahamu au udhaifu wao kwa wananchi huko nje.Hapa ndipo lilipokuwa kosa la Chadema,waliweka mbele jazba kuliko busara, hilo ni kosa bila kujali kama Zitto alikuwa na makosa au hakuwa nayo.
 
sifa zooote ulizoziandika ni za viongozi wa chadema wakiongozwa na mwenyekiti na katibu

Toka fununu zianze kuenea kuwa kuna ujio wa chama kipya.

Toka dr.kitila aandike makala zake kwenye gazeti la raia mwema, kuwa kuna haja ya kuanzisha chama kipya kitakachokua mbadala wa ccm na chadema'..... hii kitu imewauma wengi sana hasa chadema na sijui kwanini?

Watu mmewafukuza wenyewe, hata wanapotaka kuanzisha njia zao za kutimiza ndoto zao bado mnaonekana kuwapiga vita.

Mnataka wasifanye shughuli yoyote ya siasa na ndo roho zenu zitasuuzika?

Acheni ukafiki na wivu za kike na wala hazitowasaidia wala kuwazuia kitila,zito mwigamba na wengi wao waliopo kwenye foleni muda si mrefu ujao kuendelea na harakati zao za kimaisha na kisiasa.

KUMBUKENI MAISHA NI VITA.
NI WAJIBU WA KILA MTU KUIPIGANA VITA YA MAISHA NA KUISHINDA. MANENO YENU HAYATOSAIDIA KITU.
 
Kwenye hili Chadema walikosea...sitaki kuamini kuwa watu walio tayari kuongoza nchi walishindwa kulimaliza hilo la Zitto humo ndani ya chama kimyakimya bila kuleta sintofahamu au udhaifu wao kwa wananchi huko nje.Hapa ndipo lilipokuwa kosa la Chadema,waliweka mbele jazba kuliko busara, hilo ni kosa bila kujali kama Zitto alikuwa na makosa au hakuwa nayo.

Huwezi kuendesha mapambano ukiwa na wahuni, wanafiki, wasakatonge na wajinga kama Zitto, Kitila na Mwigamba. Wahuni hao kutimuliwa ni uamuzi wa busara kuliko uamuzi wowote uliowahi kufanywa na CDM
 
Back
Top Bottom