Dk. Kilahama aibiwa, aomba msaada JF

Dk. Kilahama aibiwa, aomba msaada JF

Wadau, hapa chini nakuleteeni kilio cha Dk. Kilahama. Ameniomba niwasilishe ujumbe huu kwa wadau akiamini JF ipo kila mahali. Tafadhali usomeni na tuone namna ya kumsaidia.

Kupitia huduma ya mitandao ya kijamii, Dk. Felician B. Kilahama, anayo masikitiko makubwa sana kutokana na kitendo cha baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema walisababisha apoteze begi lake lililokuwa na vifaa vyake muhimu. Hali hii ilitokea tarehe 06 Julai 2014 akiwa njiani kutoka Iringa na ilikuwa kati ya Morogoro na Picha ya Ndege-Kibaha ilipodhihirika kuwa hilo begi ambalo lilikuwa na vifaa muhimu likawa halipo sehemu ambako alilihifadhi.

Vifaa hivyo ni pamoja na laptop, camera (canon ndogo), kisanduku cha miwani ya kusomea kikiwa na miwani pamoja na modems za internet mbili- Voda na Zantel; funguo za nyumbani, simu yenye njia mbili - Tigo na Zantel, flash discs kadhaa, nyaraka muhimu na dawa kadhaa za kisukari na BP. Hali ya kuibiwa kwa begi hiyo ilijulikana baada ya kufika Picha ya Ndege, Kibaha na kijana mmoja akawa anateremka hapo na akasema ameibiwa computer yake. Ndipo Dk. Kilahama aliposhtuka na akaangalia sehemu aliyokuwa amehifadhia begi lake ikawa halioni na kutafuta kila sehemu bila ya mafanikio. Hivyo kuashiria kuwa limeibwa.

Pia Msafiri mwingine naye akaona sehemu alipoweka computer yake haipo! Kikawa ni kilio. Inasemekana wanaume wawili waliteremkia sehemu ya Mlandizi na kwa kuwa ilikuwa saa tatu usiku na ilikuwa giza; lakini baadhi ya abiria waliowaona wakiteremka na mabegi yanayodhaniwa kuwa ni hayo yaliyotea.

Kwa hali hiyo wakazi wa Mlandizi wanaombwa kuwa wadadisi kwa watu watakaoonekana wakiuza vitu kama hivyo. Waliochukua vitu hivyo wanefanya kitendo cha kinyama na ni dhahiri kuwa hawatatumia vitu hivyo, bali wataviuza. Wakazi wa Mlandizi na maeneo mengineyo wanatahadharishwa kuwa waangalifu katika hili. Watakaoona dalili zozote za picha au nyaraka zinazomhusu Dk. Kilahama watoe taarifa katika Kituo cha Polisi au kwa viongozi wa eneo husika.

Pia ikitokea kuwa nyaraka au dawa zimetupwa mahali tafadhali peleka kwa viongozi au kituo cha polisi au piga simu 0783 007400 au 0756 007400. Tafadhali sana tushirikiane katika hili na tufichue wahalifu wa aina hii.

NB. Dk. Kilahama ni Mkurugenzi wa Misitu mstaafu katika Wizara ya Maliasili na Utalii



kuna walakini hapa huenda kuna nyaraka muhimu sana kwenye hizo vifaa vyake so wenye shida na hizo documents wame amua kuzichukua wakazifanyie kazi....nchi ngumu sna hii....
 
Wewe endelea kuchapa usingizi tu yaani mtu mkurugenzi mstaafu wa wizara ya misitu maliasili na utalii unamchukulia simple kama mama ntilie mstaafu.

we bwana we unakua kama hujui wastaafu wa nchi yetu wanavyoishi kwa shida? watu walikua mawaziri lakini hata pa kulala hawana wacha mchezo.
 
Wadau, hapa chini nakuleteeni kilio cha Dk. Kilahama. Ameniomba niwasilishe ujumbe huu kwa wadau akiamini JF ipo kila mahali. Tafadhali usomeni na tuone namna ya kumsaidia.

Kupitia huduma ya mitandao ya kijamii, Dk. Felician B. Kilahama, anayo masikitiko makubwa sana kutokana na kitendo cha baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema walisababisha apoteze begi lake lililokuwa na vifaa vyake muhimu. Hali hii ilitokea tarehe 06 Julai 2014 akiwa njiani kutoka Iringa na ilikuwa kati ya Morogoro na Picha ya Ndege-Kibaha ilipodhihirika kuwa hilo begi ambalo lilikuwa na vifaa muhimu likawa halipo sehemu ambako alilihifadhi.

Vifaa hivyo ni pamoja na laptop, camera (canon ndogo), kisanduku cha miwani ya kusomea kikiwa na miwani pamoja na modems za internet mbili- Voda na Zantel; funguo za nyumbani, simu yenye njia mbili - Tigo na Zantel, flash discs kadhaa, nyaraka muhimu na dawa kadhaa za kisukari na BP. Hali ya kuibiwa kwa begi hiyo ilijulikana baada ya kufika Picha ya Ndege, Kibaha na kijana mmoja akawa anateremka hapo na akasema ameibiwa computer yake. Ndipo Dk. Kilahama aliposhtuka na akaangalia sehemu aliyokuwa amehifadhia begi lake ikawa halioni na kutafuta kila sehemu bila ya mafanikio. Hivyo kuashiria kuwa limeibwa.

Pia Msafiri mwingine naye akaona sehemu alipoweka computer yake haipo! Kikawa ni kilio. Inasemekana wanaume wawili waliteremkia sehemu ya Mlandizi na kwa kuwa ilikuwa saa tatu usiku na ilikuwa giza; lakini baadhi ya abiria waliowaona wakiteremka na mabegi yanayodhaniwa kuwa ni hayo yaliyotea.

Kwa hali hiyo wakazi wa Mlandizi wanaombwa kuwa wadadisi kwa watu watakaoonekana wakiuza vitu kama hivyo. Waliochukua vitu hivyo wanefanya kitendo cha kinyama na ni dhahiri kuwa hawatatumia vitu hivyo, bali wataviuza. Wakazi wa Mlandizi na maeneo mengineyo wanatahadharishwa kuwa waangalifu katika hili. Watakaoona dalili zozote za picha au nyaraka zinazomhusu Dk. Kilahama watoe taarifa katika Kituo cha Polisi au kwa viongozi wa eneo husika.

Pia ikitokea kuwa nyaraka au dawa zimetupwa mahali tafadhali peleka kwa viongozi au kituo cha polisi au piga simu 0783 007400 au 0756 007400. Tafadhali sana tushirikiane katika hili na tufichue wahalifu wa aina hii.

NB. Dk. Kilahama ni Mkurugenzi wa Misitu mstaafu katika Wizara ya Maliasili na Utalii



Aliifanyia nn nchi hii kipindi cha uongozi wake? Isije kuwa wananchi wamerudisha mali alizowaibia
 
Mmm,
Pole zao;
Watakuwa hao vijana waliwasoma wakajua kuwa
mawazo yao yapo mbali na mabegi yao wakaamua
kujisevia;
 
daah!wezi sio kabisa yani acheni wauliwe wakikamatwa
 
Wadau, hapa chini nakuleteeni kilio cha Dk. Kilahama. Ameniomba niwasilishe ujumbe huu kwa wadau akiamini JF ipo kila mahali. Tafadhali usomeni na tuone namna ya kumsaidia.

Kupitia huduma ya mitandao ya kijamii, Dk. Felician B. Kilahama, anayo masikitiko makubwa sana kutokana na kitendo cha baadhi ya watu wasiokuwa na nia njema walisababisha apoteze begi lake lililokuwa na vifaa vyake muhimu. Hali hii ilitokea tarehe 06 Julai 2014 akiwa njiani kutoka Iringa na ilikuwa kati ya Morogoro na Picha ya Ndege-Kibaha ilipodhihirika kuwa hilo begi ambalo lilikuwa na vifaa muhimu likawa halipo sehemu ambako alilihifadhi.

Vifaa hivyo ni pamoja na laptop, camera (canon ndogo), kisanduku cha miwani ya kusomea kikiwa na miwani pamoja na modems za internet mbili- Voda na Zantel; funguo za nyumbani, simu yenye njia mbili - Tigo na Zantel, flash discs kadhaa, nyaraka muhimu na dawa kadhaa za kisukari na BP. Hali ya kuibiwa kwa begi hiyo ilijulikana baada ya kufika Picha ya Ndege, Kibaha na kijana mmoja akawa anateremka hapo na akasema ameibiwa computer yake. Ndipo Dk. Kilahama aliposhtuka na akaangalia sehemu aliyokuwa amehifadhia begi lake ikawa halioni na kutafuta kila sehemu bila ya mafanikio. Hivyo kuashiria kuwa limeibwa.

Pia Msafiri mwingine naye akaona sehemu alipoweka computer yake haipo! Kikawa ni kilio. Inasemekana wanaume wawili waliteremkia sehemu ya Mlandizi na kwa kuwa ilikuwa saa tatu usiku na ilikuwa giza; lakini baadhi ya abiria waliowaona wakiteremka na mabegi yanayodhaniwa kuwa ni hayo yaliyotea.

Kwa hali hiyo wakazi wa Mlandizi wanaombwa kuwa wadadisi kwa watu watakaoonekana wakiuza vitu kama hivyo. Waliochukua vitu hivyo wanefanya kitendo cha kinyama na ni dhahiri kuwa hawatatumia vitu hivyo, bali wataviuza. Wakazi wa Mlandizi na maeneo mengineyo wanatahadharishwa kuwa waangalifu katika hili. Watakaoona dalili zozote za picha au nyaraka zinazomhusu Dk. Kilahama watoe taarifa katika Kituo cha Polisi au kwa viongozi wa eneo husika.

Pia ikitokea kuwa nyaraka au dawa zimetupwa mahali tafadhali peleka kwa viongozi au kituo cha polisi au piga simu 0783 007400 au 0756 007400. Tafadhali sana tushirikiane katika hili na tufichue wahalifu wa aina hii.

NB. Dk. Kilahama ni Mkurugenzi wa Misitu mstaafu katika Wizara ya Maliasili na Utalii



Pole kwanza.Sasa wewe kwa akili yako mtu gani akuibie alafu aje kurudisha?
 
mlete doctor kwenye tv ya asili awaone wezi wake na watarudisha wenyewe.

au subili albadili ya mama wema sepetu ikianza kufanya wale masheikh wakabidhiwe jukumu la pili.

tatu si vibaya mdau mkitangaza hata reward kwa atakayefanisha kupatikana vitu hivyo.

simu zake kama ni za kisasa anzeni na kitengo cha it kwenye hiyo mitandao mzitrack.
 
na kama pale mlandizi watazipata tu, ni eneo dogo, labda wakauzie bagamoyo, na kama alikuwa kwenye basi uwa wanasema chunga laptop yako na mizigo yako ya ndani, na je wakati wanashuka taa hazikuwahswa kwenye gari?

pole kwa wote hao walioibiwa, hawa wezi wanarudisha watu nyuma sana, ndio maana jana vijana wawili wezi walipigwa sana 77 mule ndani, eti unategemea utakimbilia wapi, hawa wezi waliothibiitishwa ni wezi wapigwe tu.
 
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu,
mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?
tatizo nini hajapewa gari? hajapewa dereva?

unashangaa nin sasa kwani kupanda gari la abiria ni ajabu? kwani yeye siyo abiria .kwel ndio maana hii nchi hatuendelea na hatutaendelea kama tutakuwa na kizazi kama chenu.wakati nchi zilizoendelea watu kama professa wanapanda baskeli.
 
pole sana Dk Kilahama. Dk Kilahama ni mtu ambaye alikuwa muadilifu sana kwenye utumishi wa umma.
Mungu amjalie apate vitu vyake
 
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu,
mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?

Angepanda ndege mngelalamika pia.

Huna hata jema
 
Wewe endelea kuchapa usingizi tu yaani mtu mkurugenzi mstaafu wa wizara ya misitu maliasili na utalii unamchukulia simple kama mama ntilie mstaafu.

Ni bora ukae tu kimya jamaa wamekuzidi hoja. Claim yako haina mashiko, sanasana inakuexpose kama mtoto ambaye hajakuwa bado ufahamu wake wa maisha upo chini.
 
Naendelea Kushangaa na ninaomba mnisaidie kushangaa nyie wenzangu,
mtu mwenye hadhi ya ukurugenzi kisha doctor anapanda gari la abiria ya tsh 35,000?
tatizo nini hajapewa gari? hajapewa dereva?

why not using public transport? mimi acha waseme nikiwa bongo napanda zangu dala dala kama kawa haimaanishi kuwa sina gari au uwezo wa tax, bali maamuzi tu..ishi upendavyo usiishi watakavyo.
 
attachment.php
 
Back
Top Bottom