ni tanzania tu mtu anaweza kufaulu mtihani nje ya chumba cha mtihani, ushindi wa mezani.
Haya mambo mkuu mzizi wake uko mbali sana! Unapokua na mkuu omba omba! Tegemea wazazi omba omba! hivyo kutengeneza watoto omba omba!
Tatizo kubwa katika kuwa omba omba ni kuwa ni tabia ambayo ni self rewarding (positive reinforcing) na hivyo ni vigumu sana kuacha!! Hivyo tegemea kuomba kila upatapo nafasi hata kama kitu unakiweza. Na ni vigumu kujua kama unaweza au huwezi kwa kuwa unakua ushaomba!
Hii ina maana gani kwenye haya matokeo,
kwa sasa wazazi wamefurahi;
unajua kwa nini?! kwa wazazi wengi wao bora ufaulu, hayo ya kuelewa yatakuja baadae! Hii inamaanisha kuwa mzazi yuko tayari hata kumnunulia mwanae mtihani ili afaulu!
Unganisha dots uje kwenye suala la rushwa ilivyoshamiri katika nchi yetu na ufisadi uliotawala viongozi wetu, ni muendelezo wa fikra hizi! Cha kwanza ni bora kupata unachotaka, suala la umekipataje na wengine wanaumiaje, halina msingi.
Kuna makala moja ya Jenerali Ulimwengu, aliandika tunaishi kama vile hapa sio kwetu!! kama vile tunataka kufunga biashara hapa fasta ili twende kwetu sasa!
Mtu mwenye fikra sahihi ndio atagundua tatizo hapo, mazuzu wanafurahi serikali 'imesikia kilio chao' na hivyo watoto watafaulu kwa kipimo sio cha mtihani waliofanya bali eti kwa 'kuzingatia juhudi walizoweka na mazingira magumu ya Tanzania ya udahili mkubwa bila kujali ubora wa elimu hiyo' kulingana na kauli ya Lukuvi!
Watoto wao wako shule za international, kwa namna yeyote huwezi kuwalinganisha na hawa wa kupewa maksi za ugumu wa maisha! Interview zikija wao watapita!
Huu ulikua wakati wa wazazi kuhoji sasa, nini kilichotokea; kwa nini?! nini athari ya kutatua tatizo la kufeli kwa kushusha madaraja ya ufaulu?! maana maksi ziko pale pale! Na kufeli ni kufeli!
Hekaya za abunuasi,hadi 2015 tutasikia A inaanzia 50%!
Mwanasiasa anataka kura, mzazi anataka mtoto afaulu!
Na mtoto anataka kufaulu kwa kuwa hapendi kufeli sio kwa kuwa anapenda kufaulu!
Tunalishana ujinga! Kilichofanyika ni zaidi ya ugaidi! Kutengeneza taifa la wajinga kwa makusudi?!!
Nani atatutoa hapa tulipo?! Tunapika bomu! Mungu atuepushe!