Dk. Joyce Ndalichako, usibabaishwe na mtu yeyote

Dk. Joyce Ndalichako, usibabaishwe na mtu yeyote

Kwanini akubali kubeba mzigo usio wake?
Kwani ule Msalaba wa Kufeli Islamic Knowldge Ulikuwa wake na Maafisa wa NECTA??????
Thats Politics, Nashangaa sana Kwanini Huyu Mama Hajajiuzulu Kwa kweli.
Wanasiasa ambao hata Elimu zao ni Za Kuunga unga zisizoeleweka Kama Lukuvi Wanaingilia Utendaji Uliotukuka wa Mama, Dr Ndalichako
 
Kuvuja mitihani
Kuchakachua matokeo
Upendeleo
Kubadilisha matokeo miongoni mwa watahiniwa
Matokeo yasio sahahihi kisingizio computer
Hizi ndoo zake


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
ojective ni nini hapa????
upo msalani nini???????
haya hebu tulia halafu andika ulichokuwa unataka kuandika.

Wote mliofaulu kwa ufaulu mwembamba lazima mtamuona huyu mama hafai, lakini kwa watu walio makini na wanaotaka elimu yenye tija wanamuona Ndalichako ni mtu makini.
Mbona hamjiulizi tokea waanze kumpigia kelele za kung'oka kwanini Rais asimsimamishe kazi, ni kwa sababu anajua kuwa anafaa, hayo mambo mengine ni chuki zenu tu.
 
Mtoa mada nakupa tano. Ni kweli siasa imeharibu elimu yetu na bado inaendelea kuharibu.

Ndalichako tunajua udini ndio unaokupiga vita, kaza uzi fanya kazi yako kwa weledi, hata kama watakuona hufai historia itakukumbuka.
Religion is what keeps the poor from murdering the rich. BY: Napoleon Bonaparte
 
Ndalichako alinifundisha UDSM course ya EP,ni mama mwelewa,smart na mwenye busara za kutosha!Hastahili kunyenyekea udhalimu wa serikali dhalimu yenye kutafuta sifa na kumharibia heshima yake kwa kuingilia maamuzi ya baraza!Haiwezekani serikali kuingilia maamuzi ya wizara yenye uweledi mbovu kwa taifa la baadaye!Ningelikuwa Ndalichako ningaliachia mgazi!
 
Kwa heshima yake, kwa utu wake , kwa utaifa wake na kwa uafrika wake , angejiuzulu ili kuwapisha wanaotaka kuliaminisha taifa kuwa yeye ndio tatizo la elimu nchini wakati hawana hata mtaala wa elimu.


Dr hawezi kujiuzulu ata kama mkiandamana kwa sababu hana kosa badala yake Shukuru na Mulugo wajiuzulu haraka.

"naapa kwamba sitoliamini jeshi la polisi milele ehe mwenyezi mungu nisaidie"
 
Ukweli mchungu.
Mama ndalichako you must go, Viva tume ya pinda kwa kuyalipua madudu haya ya Ndalichako, tuna uchungu sana tumezika watu kisa upumbavu wa wachache.
 
Tatizo ni kubwa kuliko mnavyofikiria. Tatizo si Ndalichako wala si baraza la mitihani.
 
kwanza pole kwa ndalichako kwa kuingiliwa na wapenda sifa

pili pole kwa lukuvi kwa kulazimishwa kusoma kitu asicho elewa madhara yake kwa taifa lake
 
kwanza pole kwa ndalichako kwa kuingiliwa na wapenda sifa

pili pole kwa lukuvi kwa kulazimishwa kusoma kitu asicho elewa madhara yake kwa taifa lake

Lukuvi anaingia kwenye historia ya kulipua bomu kwa mbwembwe ambalo nayeye linamwua kisa kutaka sifa
 
Ndalichako yuko makini lakini huu ni mpango wa waislamu kutaka kumngoa pale chini ya uongozi mdini no 1 ushauri wangu kwako Ndalichako kwa heshima yako jiuzulu uachie ccm na waislamu wateue mtu wao ili waizike kabisa elimu yetu na kuhani matanga.
 
Mkuu, tatizo liko hapa, Matokeo yamefutwa nadhani mpaka hapo tupo pamoja. Sababu kuu ya Tume ni kuwa ulitumika mfumo mpya bila wadau kushirikishwa. Na kutokana na mfumo huo wanafunzi wamefeli. Je ni nani aliruhusu huo mfumo? Na kama ufaulu wa wanafunzi ulikuwa chini kwa maana ya baraza lipo sahihi. Inakuwaje waruhusu matokeo yafutwe? Wakati wanajua kuwa wao wako sahihi na serikali haipo sahihi? HIVYO KAMA NDALICHAKO AMEKUBALIANA NA SERIKALI KUFUTA MATOKEO SAHIHI NA KUKUBALI WATUPATIE MATOKEO YASIYO SAHIHI KWA MAANA YA KUTUFURAHISHA hafai kukalia hicho kiti, vivyo hivyo KAMA ALITUMIA MFUMO MPYA BILA KUSHIRIKISHA WADAU hafai kukaa hapo. LA SIVYO AITE MEDIA NA ATUAMBIE UKWELI ULIVYO

Mkuu, Ndalichako aliteuliwa, hivyo aliyemteua ameamrisha afaulishe watoto. Ila kama angefikiria zaidi angeweza kulinda heshima yake ya udokta wa falsafa kwa kujiuzulu. Kuhusu mfumo mpya wa madaraja ya ufaulu, wizara itakuwa ilijua kuhusu mfumo huo. Matokeo walikaa nayo muda mrefu tu baada ya kukamilika na waziri Kawambwa aliyaona kabla ya kutangazwa, kwanini hakustukia anguko hilo lililotokana na huo mfumo kama alikuwa haufahamu? Matokeo yalitangazwa kwa idhini ya waziri, hivyo aliridhika na kilichofanyika na baraza la mitihani. Hivyo kufutwa matokeo haya, Kawambwa na Mmwenzake wanapaswa kujiuzulu, wamehusika na mchakato huu kwasababu baraza la mtihani ni idara tu ya wizara ya Elimu chini ya Kawambwa.
 
Kawambwa alisema matokea hayo ni kutokana na kudhibiti mainya ya wizi wa mitihani, sasa hii si ndio ilikuwa kauli ya serikali? na serikali hii hii inayafuta , kwakweli hizi hekaya za abunuasi
 
Ukweli mchungu.
Mama ndalichako you must go, Viva tume ya pinda kwa kuyalipua madudu haya ya Ndalichako, tuna uchungu sana tumezika watu kisa upumbavu wa wachache.

Bila shaka wewe ndiye ulichora zombie kwenye mtihani wako wa K4 mwaka jana. Na sasa unarukaruka kwa kuwa una uhakika na alama za bure. Poor you.

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Mkuu, Ndalichako aliteuliwa, hivyo aliyemteua ameamrisha afaulishe watoto. Ila kama angefikiria zaidi angeweza kulinda heshima yake ya udokta wa falsafa kwa kujiuzulu. Kuhusu mfumo mpya wa madaraja ya ufaulu, wizara itakuwa ilijua kuhusu mfumo huo. Matokeo walikaa nayo muda mrefu tu baada ya kukamilika na waziri Kawambwa aliyaona kabla ya kutangazwa, kwanini hakustukia anguko hilo lililotokana na huo mfumo kama alikuwa haufahamu? Matokeo yalitangazwa kwa idhini ya waziri, hivyo aliridhika na kilichofanyika na baraza la mitihani. Hivyo kufutwa matokeo haya, Kawambwa na Mmwenzake wanapaswa kujiuzulu, wamehusika na mchakato huu kwasababu baraza la mtihani ni idara tu ya wizara ya Elimu chini ya Kawambwa.

Huyu Kawambwa haonyeshi kama kweli ni msomi. Anavyoongea na kutoa hoja zake ni questionable. Mbona Lukuvi ni UPE lakini presention zake ni imara. Hawezi siasa ndiyo maana anajibu hata utumbo.
 
Dk. Ndalichako hongera sana kwa kazi nzito na nzuri unayoifanya. Mimi binafsi naridhika na kazi nzuri unayoifanya. Kushuka kwa kiwango cha elimu Tanzania ni sera mbovu ya serikali ya chama cha mapinduzi (CCM). Fanya kazi zako bila kuingiliwa na mtu yeyote. Watanzania wenye akili tuko pamoja nawe.

Nalisubiri gazeti la Anuur la ijumaa ijayo ndipo nicomment
 
ukweli mchungu.
Mama ndalichako you must go, viva tume ya pinda kwa kuyalipua madudu haya ya ndalichako, tuna uchungu sana tumezika watu kisa upumbavu wa wachache.

ni tanzania tu mtu anaweza kufaulu mtihani nje ya chumba cha mtihani, ushindi wa mezani.
 
ojective ni nini hapa????
upo msalani nini???????
haya hebu tulia halafu andika ulichokuwa unataka kuandika.

Objective ni kumwambia ndalichako asimamie msimamo wake asiyumbshwe na siasa majitaka za magamba ambao wanakwepa tatizo la msingi la vijana wetu kufeli.
 
Back
Top Bottom