Mkuu, tatizo liko hapa, Matokeo yamefutwa nadhani mpaka hapo tupo pamoja. Sababu kuu ya Tume ni kuwa ulitumika mfumo mpya bila wadau kushirikishwa. Na kutokana na mfumo huo wanafunzi wamefeli. Je ni nani aliruhusu huo mfumo? Na kama ufaulu wa wanafunzi ulikuwa chini kwa maana ya baraza lipo sahihi. Inakuwaje waruhusu matokeo yafutwe? Wakati wanajua kuwa wao wako sahihi na serikali haipo sahihi? HIVYO KAMA NDALICHAKO AMEKUBALIANA NA SERIKALI KUFUTA MATOKEO SAHIHI NA KUKUBALI WATUPATIE MATOKEO YASIYO SAHIHI KWA MAANA YA KUTUFURAHISHA hafai kukalia hicho kiti, vivyo hivyo KAMA ALITUMIA MFUMO MPYA BILA KUSHIRIKISHA WADAU hafai kukaa hapo. LA SIVYO AITE MEDIA NA ATUAMBIE UKWELI ULIVYO