Dizasta Vina a.k.a Maradona

Dizasta Vina a.k.a Maradona

ukiacha track ya SHAHIDI, Ngoma ya KANISA aliandika akiwa ametuliza Sana akili walau angekua kwenye hiyo class kwenye ngoma zingine Kama tano ningemshindanisha na Nikki mbishi lakini bado ajipange
Mwambieni dogo atupe taulo chini akaze gemu sio lelemama na kusifiwasifiwa Insta na Twitter kunamlemaza, ukifanya kweli mboni utasifiwa hata na asiekujua kwamba huyu mwamba ni kisanga kingine, Disasta najua upo humu kaza acha kulewalewa sifa tutakusahau toa mtiririko wa vyuma vikali, Niki Mbishi - Mama Luciya ndio naisikiliza hapa mda huu
 
Inategemeana u aposema Hip Hop ya siku hizi unakusudia wasanii gani

Kama ni hawa mainstream basi uko sahihi ila ukija underground hivyo vyote ulivyovitaja vipo

Kama umeisikiliza The Verteller ya Dizasta utaona lines fikirishi zimeanza kwenye ngoma ya kwanza ile intro mpaka unaifikia tatuu ya asili kote huko ame spit tungo tata

Achana na hizo

Kamsikilize Kinya Mistari, Nala Mzalendo, na dogo Boshoo japo siku hizi ameanza mitindo ya kina Lunya ila decent songs ziko vyema.
Kwanza hao kina boshoo ndo hamna kila kitu. Uwezo wao ni hamna ni dhaifu Ila hamna namna ndo maana Nikki mbishi kwenye ngoma ya maji Ni uhai Kuna mstari anasema "naaumia kujua chin bees ndo Yule King Kong" yaani kina chin bees wanaonekana ndio warithi wa kina chid Benz.. Sasa fikiria Leo hii kina boshoo ndo replacement ya Langa, Jay Moe, Solo thang, professor Jay... Si aibu mkuu tuwe seriously...
Walau Lunduno members/Tamaduni music ndo wasanii wangu wa mwisho kabisa baada ya hapo sitaki kabisa kusikiliza kizazi kilichofata....

Msikilize Bando mc anakwambia eti "demu wako akilala na Dera jua Kuna mtu anaenda kuchambwa ndotoni" Sasa kweli huu Ni mstari????

Kwenye ngoma ya TEMANOLEJI ya Fid Kuna mstari anasema "nikisikiliza hip-hop ya bongo si-gain na-lose vitu/ mamc wote waongo na wananiiuzi kilasiku... Mistari Yao Ni Kama mfano wa kile kisichofaa kuandikwa/ sauti zao si za michano walipaswa wajiunge misifa...."

Jamani jamani hip-hop bongo imekosa watu kabisa Kama young Lunya anaonekana n msanii bora wa hip-hop si Ni aibu kwa taifa
 
Beat nmesikiliza ambapo hata mimi naweza kutembea nayo bila kutokatoka nje ya beat ndio maana nikasema akipewa Azma anamtosha kumkalisha kutembea na hio beat bila kutoka nje ya beat namaanisha kunata na beat sio beat inaenda kushoto wewe unaenda kulia, hapo sijamtaja Moko wa Miujiza, PMawenge, Stereo, NikiMbishi, FidQ, Songa, Zaiid, CJaMoka, Conboi, Raptcha, Wakazi, Troubado Joji, Maalim Nash Mc

Mwambie atembee na beat km Bruno Mars mbon Msaga Sumu na Shoro Mwamba wananata na beat za Singeli, hio Hatia III angejua angefungia tu ndani kazidiwa hadi na Dulla Makabila, atembee na beat km anavyofanya Kontawa yaan anashindwa kujifunza kwa Mwana FA & AY, mwambie aende kwa Prof J ampe Darasa na Bill Nass

Yaan huyo rapper wenu hata Magazijuto hamfikii
Dizasta kulinganisha na Raptcha Ni utani Raptcha na genge lake la kina Lunya,bill nas, manengo na wengine wote waalitakiwa wafunguliwe kesi ya kujinufaisha kupitia hip-hop hao sio wasanii wa HIP-HOP Bali n kichekesho...
 
Sawa nazani kabla ya dizasta nliwasikiza sana akina
-fid q
-nikki mbishi
-one incredible
-stereo
-nash emcee
-p mawenge
-stamina

Lakini toka nmeanza kumsikiza dizasta pale tamaduni
Jamaa amekuja na kitu tofauti kuliko wote apo juu

Aina ya uandishi,story zake na flow!

Kwasasa watu ambao nawafatilia sana ni
1.Dizasta
2.young killer
3.G.H.A.F.L.A
4.Boshoo
5.Nacha
6.Toxic

Hawa marapper wengne akina Lunya,Rapcha ni vibes na flow tu hakuna.nachopata nkisiza ngoma zao
Sikupangii lakini ukimtoa Young killer na Dizasta hao wengine sijawai ona Kama Wana kitu Cha kunifanya niwafatilie nao nawaunganisha kwenye kundi la kina Lunya tu...
Toxic fuvu Ni mkali but Ni upande wa freestyle... Huko ndo nilimkubali Sana
 
Sikupangii lakini ukimtoa Young killer na Dizasta hao wengine sijawai ona Kama Wana kitu Cha kunifanya niwafatilie nao nawaunganisha kwenye kundi la kina Lunya tu...
Toxic fuvu Ni mkali but Ni upande wa freestyle... Huko ndo nilimkubali Sana

Take your time kamsikilize Ghafla
Anaandika councious sana thou kweli hajafika level za akina dizasta or young killer lkn kuna vitu utapata..!

Kama ulikubali ngoma ya kontawa-champion


Basi Ghafla alikuwa nazo hizo kitambo
 
sauti zao si za michano walipaswa wajiunge misifa / young Lunya anaonekana n msanii bora wa hip-hop si ni aibu kwa taifa..
Nimekuelewa nimekuelewa Ila wapo ambao hawajakuelewa utofauti wa vizazi nilimwambia Jana mwamba humu ampe Disasta title ya wimbo aiite VIZAZI HAVIFANANI kisha atengenezee story atembee ndani hio title mwanzo mwisho na ilete maana
 
Mwambieni dogo atupe taulo chini akaze gemu sio lelemama na kusifiwasifiwa Insta na Twitter kunamlemaza, ukifanya kweli mboni utasifiwa hata na asiekujua kwamba huyu mwamba ni kisanga kingine, Disasta najua upo humu kaza acha kulewalewa sifa tutakusahau toa mtiririko wa vyuma vikali, Niki Mbishi - Mama Luciya ndio naisikiliza hapa mda huu
Naam Kuna siku nilisema inabidi afanye ngoma ambazo zitapenya mainstream wakanidiss kua sijui kitu Mara kichwa panzi... Nikacheka sana. Kwani mbona kina solo thang, roho Saba, Rado, kalapina walikua wanafanya ngumu lakini zilikua zinaimbwa kina Kona

Kumbuka enzi zile kikosi Cha mizinga walikua wanatoa ngoma ngumu kinyama we kumbuka tu mstari wa mbele au moja Ni nguvu Ni ngoma ambazo zilitikisa kinyama na n ngumu zenye panchi kinyama au Nako 2 Nako walikua wanashusha Mapini magumu lakini yanahit Hadi kina dada wanakariri mistari nakumbuka enzi hizo tuko skuli unakuta demu anaweza kukuachania Hawatuwezi, niaje Ni vipi, au kimbia fasta ya babuu w akitaa Hadi unaona aibu... Sahivi sio rahisi mtu ambaye sio shabiki lialia wa hi-hop kuchana hata mistari mitatu tu ya Dizasta.

Fikiria wakati Stamina ametoa ngoma ya kabwela ilikimbiza kila Kona hadi wamama walikua waniimba je yenyewe sio ngumu? Kuna demu flani hivi aliwahi kuchana ngoma ya Nikki mbishi "kill your self" kwenye audition ya bongo star search Hadi majaji wakapagawa..

Hakuna aisiyemkubali Dizasta labda mwehu lakini ajifunze na akaze bado ana safari ndefu Sana.
 
Punchline Dizasta anazo chache sana huwezi kompare na hao niliowataja hata kidogo hawezi kabisa....

Ukipata muda chagua ngoma yake moja tu unayoikubali halafu compare na ngoma yoyote ya Fid kwenye albamu ya "VINA MWANZO KATI NA MWISHO" ilikua na haya Mapini....
1. August 13 ft. Juma nature
2. Kadi na Ua Rose ft. Jay see
3. Chagua moja ft. TID Langa & black rhino
4. Mwanangu ft Banana Zoro
5. Utaua bendi ft magazijuto
6. Vina mwanzo Kati na mwisho
7. Dunia nzima
8. Ni hayo tu ft. Langa & professor Jay
9. Unanijua unanisikia
10. Mwanza mwanza
11. Goodnite ft lady Jay dee

Kama ulikua tayari umeanza kusikiliza muziki hapo hamna ngoma hata moja ambayo haikuwa hit zote zilisumbua Sana top ten na pia ngoma ya "Ni hayo tu" pamoja na "mwanza mwanza" zilishinda Tuzo enzi zile kili music awards zikitamba.

Njoo album ya PROPAGANDA humo Kuna mawe si masikhara na zote zilitamba Sana kila pembe na Zina punchlines za kutisha..
Hebu pitia hii list iliyomo kwenye hiyo album ndo utaelewa nachomaanisha Nini maana ya mistari...
1.Propaganda
2.Wananiita king ft Nylon
3. Juhudi za wasio jiweza ft bi kidude
4. Utaua game ft juma nature
5. Kila siku ft Q Jay
6. Hey Lord ft Mzungu kichaa
7. Temanoleji ( Natamani kwanza wasanii wa hip-hop wangesikiliza hii ngoma kabla ya kwenda studio)
8. Mwanamalundi
9. Shimo limetema ft. AY & Ncha Kali
10. Mama ft Banana Zoro
11. Nyota ya mchezo ft Doreen
12. Usinikubali haraka ft matonya
13. Ripoti za mtaani ft Zahiri Zoro
14. Nilipotoka
15. Danger

Kiukweli Mimi Ni shabiki wa Dizasta Tena nina ngoma zake kwenye simu na hua namsikiliza Ila Kuna vitu vingi sana anamiss sahivi naona anadisiana na kina maarifa...
Kiukweli bado ana safari sana... ukiacha track ya SHAHIDI, Ngoma ya KANISA aliandika akiwa ametuliza Sana akili walau angekua kwenye hiyo class kwenye ngoma zingine Kama tano ningemshindanisha na Nikki mbishi lakini bado ajipange

Track11:nyota ya mchezo bonge la ngoma

Ofcoz naunguna na nyinyi kabisa
Hatuwezi kumfikisha dizasta level za akina fid hata nusu bado hajafika.fid ana kila kitu mpaka flow yake ni

Ongeza piaa last album yake ya “KITAALOJIA”

Ngoma zote ni hit huwa na skip “intro” tu

Halafu nkifika kene “ulimi mbili” naweka
 
Take your time kamsikilize Ghafla
Anaandika councious sana thou kweli hajafika level za akina dizasta or young killer lkn kuna vitu utapata..!

Kama ulikubali ngoma ya kontawa-champion


Basi Ghafla alikuwa nazo hizo kitambo
Hiyo ngoma ya kontawa sijawahi ikubali Ina mistari ya kijinga tu kwanza kontawa Ni komediani sizani Kama n msanii...
Ye si ndo alisema huko kwao hakuna aliyetoboa zaidi ya kutoboa sikio???
Kweli huyu naye tunapaswa kumjadili au kumuacha akafie mbele
 
Track11:nyota ya mchezo bonge la ngoma

Ofcoz naunguna na nyinyi kabisa
Hatuwezi kumfikisha dizasta level za akina fid hata nusu bado hajafika.fid ana kila kitu mpaka flow yake ni

Ongeza piaa last album yake ya “KITAALOJIA”

Ngoma zote ni hit huwa na skip “intro” tu

Halafu nkifika kene “ulimi mbili” naweka
Yap tukiacha ushabiki Fid Q atabaki kua Icon ya Hip-hop ya bongo....
We sikiliza ngoma Kama ielewe mitaa...
"Usiache ulichotaka maishani ghafla tu na kufata kile ulichotamani..!" Ni mstari wenye maono na maonyo mengi Sana...
Ifike mahali wasanii hao wanaotakiwa kua warithi wajifunze kwanza kwa ngosha ze swagger don
 
Fikiria wakati Stamina ametoa ngoma ya kabwela ilikimbiza kila Kona hadi wamama walikua waniimba je yenyewe sio ngumu? Kuna demu flani hivi aliwahi kuchana ngoma ya Nikki mbishi "kill your self" kwenye audition ya bongo star search Hadi majaji wakapagawa..
Ndio hivyo inabidi akaze msuli asilewe misifa

Fid kuna line alisema "japo miluzi ni mingi lakini Jibwa sipotei...."

Sasa Disasta atoe vitu vikali miluzi itampoteza, kuna ngoma moja ya XPlastaz inaitwa Ushanta (Masai Hip Hop) mule ndani kuna storylines anatiririka Father Neli mpaka basi, alafu kuna nyingine inaitwa Ahaa! Daah ngoja nitulie kwanza
 
Ndio hivyo inabidi akaze msuli asilewe misifa

Fid kuna line alisema "japo miluzi ni mingi lakini Jibwa sipotei...."

Sasa Disasta atoe vitu vikali miluzi itampoteza, kuna ngoma moja ya XPlastaz inaitwa Ushanta (Masai Hip Hop) mule ndani kuna storylines anatiririka Father Neli mpaka basi,
Mwanangu Kama unaijua ushanta we unajua ngoma hahahhahahahahahhahahahha umenifurahisha Sana hujui tu ungekua karibu ningekutunuku kreti tatu za bia na demu mmoja...
Kuna jamaa Alikua mwanaapolo akaanguka mgodoni anafungwa kudu kutolewa shimoni alivotoka wakati analilia Wana Waka mchana "Chali yangu unalala utafanywa kafala yerewiii"... Da you made my day
 
Naam Kuna siku nilisema inabidi afanye ngoma ambazo zitapenya mainstream wakanidiss kua sijui kitu Mara kichwa panzi... Nikacheka sana. Kwani mbona kina solo thang, roho Saba, Rado, kalapina walikua wanafanya ngumu lakini zilikua zinaimbwa kina Kona

Kumbuka enzi zile kikosi Cha mizinga walikua wanatoa ngoma ngumu kinyama we kumbuka tu mstari wa mbele au moja Ni nguvu Ni ngoma ambazo zilitikisa kinyama na n ngumu zenye panchi kinyama au Nako 2 Nako walikua wanashusha Mapini magumu lakini yanahit Hadi kina dada wanakariri mistari nakumbuka enzi hizo tuko skuli unakuta demu anaweza kukuachania Hawatuwezi, niaje Ni vipi, au kimbia fasta ya babuu w akitaa Hadi unaona aibu... Sahivi sio rahisi mtu ambaye sio shabiki lialia wa hi-hop kuchana hata mistari mitatu tu ya Dizasta.

Fikiria wakati Stamina ametoa ngoma ya kabwela ilikimbiza kila Kona hadi wamama walikua waniimba je yenyewe sio ngumu? Kuna demu flani hivi aliwahi kuchana ngoma ya Nikki mbishi "kill your self" kwenye audition ya bongo star search Hadi majaji wakapagawa..

Hakuna aisiyemkubali Dizasta labda mwehu lakini ajifunze na akaze bado ana safari ndefu Sana.

Mzee lakini unajua mziki umebadilika si sawa kulinganisha zama za akina Prof Jay ,Solo thang

Time flies and thing changes

Zamani bongofleva ilikuwa imebebwa na hiphop

Nowdays new generations media na mashabiki wanataka trap ngoma flani midundo wa kupigwa club

Na hapo ndo beef ya sugu na Ruge ilianzia
Kama ulifatilia Anti-Virus

Lakini turudi mpk tamaduni watu kama maalim Nash-kuwa na beef na media kubwa ambazo ndo zilikuwa zinaendsha biashara ya muziki

Hawa tamaduni wengi walishindwa kwenda na kasi na matakwa ya media enzi hizo that’s why wachache sana walifika mainstream

Kasikilize kivyovyote-one incredible

Amekupa summary nachokizungumza

So swala la young lunya kuwa mainstream na kutoa hit song ambazo zinaumbwa na kupigwa mtaani daily haimaanishi uwezo ni mkubwa kuliko walioko underground..!
 
Ndio hivyo inabidi akaze msuli asilewe misifa

Fid kuna line alisema "japo miluzi ni mingi lakini Jibwa sipotei...."

Sasa Disasta atoe vitu vikali miluzi itampoteza, kuna ngoma moja ya XPlastaz inaitwa Ushanta (Masai Hip Hop) mule ndani kuna storylines anatiririka Father Neli mpaka basi, alafu kuna nyingine inaitwa Ahaa! Daah ngoja nitulie kwanza
"japo miluzi Ni mingi lakini jibwa sipotei..." Hapo Ni hayo tu... Kuna mstari fid anasema "hii Ni high level sio eye level ndo maana hunioni" bonge moja la punchline
 
Mwanangu Kama unaijua ushanta we unajua ngoma hahahhahahahahahhahahahha umenifurahisha Sana hujui tu ungekua karibu ningekutunuku kreti tatu za bia na demu mmoja...
Kuna jamaa Alikua mwanaapolo akaanguka mgodoni anafungwa kudu kutolewa shimoni alivotoka wakati analilia Wana Waka mchana "Chali yangu unalala utafanywa kafala yerewiii"... Da you made my day
😂😂😂 Ushanta!
 
Ndio hivyo inabidi akaze msuli asilewe misifa

Fid kuna line alisema "japo miluzi ni mingi lakini Jibwa sipotei...."

Sasa Disasta atoe vitu vikali miluzi itampoteza, kuna ngoma moja ya XPlastaz inaitwa Ushanta (Masai Hip Hop) mule ndani kuna storylines anatiririka Father Neli mpaka basi, alafu kuna nyingine inaitwa Ahaa! Daah ngoja nitulie kwanza

Rest in Peace father Nelly
 
Mzee lakini unajua mziki umebadilika si sawa kulinganisha zama za akina Prof Jay ,Solo thang

Time flies and thing changes

Zamani bongofleva ilikuwa imebebwa na hiphop

Nowdays new generations media na mashabiki wanataka trap ngoma flani midundo wa kupigwa club

Na hapo ndo beef ya sugu na Ruge ilianzia
Kama ulifatilia Anti-Virus

Lakini turudi mpk tamaduni watu kama maalim Nash-kuwa na beef na media kubwa ambazo ndo zilikuwa zinaendsha biashara ya muziki

Hawa tamaduni wengi walishindwa kwenda na kasi na matakwa ya media enzi hizo that’s why wachache sana walifika mainstream

Kasikilize kivyovyote-one incredible

Amekupa summary nachokizungumza

So swala la young lunya kuwa mainstream na kutoa hit song ambazo zinaumbwa na kupigwa mtaani daily haimaanishi uwezo ni mkubwa kuliko walioko underground..!
We ndo hujanisoma Kama unakumbuka zamani hip-hop ndo ilikua haipewi kabisa kipaumbele na ulikua unaonekana mziki wa kihuni.... Hadi pale genius Professor Jay alipokuja kutoa ngoma ya CHEMSHA BONGO enzi zile anajiita nigger Jay akiwa na kundi la hard blaster crew HBC.. hii ngoma sio Siri iliyafanya mapinduzi makubwa Sana ndo watu wakaanza kuitazama hip-hop kwa jicho lingine.. enzi zile muziki uliokua unabamba bongo Ni dansi kina mumini mwijuma na takeu za kina mr. Nice ndipo kina fid wakaibuka.

Kubali kataa Ni utunzi tu mzee mtu akiandika ngoma inayoigusa jamii lazima atapata airtime kubwa.

Dizasta nilianza kumfatilia alipotoa ngoma ya KANISA. lakini hakua na consistency ya vitu Kama hivo....

Young Lunya Ni msanii wa mchongo tukianza kuzungumzia hip-hop labda kategori nyingine kuvuma n Jambo la kawaida hata mandonga n superstar au hamorapa.... Lakini huwezi sema ni wasanii

Swala Ni moja tu wanahiphop wenyewe ndo wamekubali kutumika vibaya...

Mtu Kama Nash unakuta anauza albamu insta na hataki kuziweka kwenye platform zingine we unazani mtu ambaye hamjui Nash atamjuaje!? Sawa Ni swala la mapato je kwanini baada ya muda asiziachie? Mfano albamu ya diwani ya maaalim Hadi leo sijui Kama Kuna ngoma iliwahi kupigwa redioni... Hii sio nzuri kabisa msanii lazima uwe na brand... Sizani kama Tupac angejulikana angetumia hii njia... Nash mcee n msanii mkali lakini kwa staili hiyo n ngumu kuacha alama
 
"japo miluzi Ni mingi lakini jibwa sipotei..." Hapo Ni hayo tu... Kuna mstari fid anasema "hii Ni high level sio eye level ndo maana hunioni" bonge moja la punchline
Hio ipo kwenye album ya Fid Q inaitwa VINA MWANZO KATI NA MWISHO niliweka nyimbo zake zote kichwani kila ngoma nilikua nachana hata ukiniwekea beat kavu na-flow na sitoki nje ya beat, enzi hizo album inatoka mahome tunatumia Radio Cassatte bro akanizawadia Tape kilichofuata ni hakuna kuruka nyimbo maana nyimbo zote kali
 
Mkuu katika maisha huwezi kupendwa na kila mtu hilo linajulikana vizuri kabisa kwahiyo hatuwezi kushangaa unavokuja na cheap reasons ili kushusha uwezo wa Dizasta vina

Katika sanaa yoyote ile kuna kitu kinaitwa ushabiki, mtu anaweza akawa na uwezo mkubwa sana ila tu wewe asikuvutie kuwa shabiki wake na wala sio dhambi ila at least heshimu uwezo wake

Zababu za kusema kuwa Dizasta vina anashindwa kunata na beat ni ujinga wa kiwango cha Lami, umeskliza nature ya hiyo beat? Umeskliza mtindo alioamua kuutumia katika hiyo beat? Au ilimradi tu nawewe umekuja kuandika ili tujue waga unaskilizaga hip-hop

Dizasta vina ndie msanii wa hip hop ambae anatumia beat ngumu kuliko msanii yoyote yule bongo, kaskilize beat zote za Hatia kuanzia 1-5 ndio utajua na hizo beat hakuna msanii wa ajabu ajabu anaweza kupita nazo lazima azitwist

Dizasta vina ndio msanii peke ambae yupo Underground stream mwenye nyimbo nyingi kuliko wasanii wote wa underground stream akiwemo Azma, Dizasta ndio msanii pekee ambae yupo Underground stream lakini ana nyimbo nyingi kuliko almost wasanii wote wa hip hop walio Mainstream

Na hiyo yote kwa sababu jamaa kuandika kwake halijawahi kuwa tatizo ata siku moja kama ilivo kwa MCs wengine wengi, kaskilize Album ya the verteller ndio utajua kwanini Dizasta vina anakuwa high rated kama msanii Bora

With all due respect to Azma, ila Dizasta ni maji marefu sana kwa mshkaji, labda tu nikuulize Umewahi kuona Uzi ambao unamuongelea Azma? Kama hapana unahisi ni kwa sababu gani? Na je umeona nyuzi ngapi humu zinaongelea uwezo wa Dizasta vina kama jibu ni ndio je unahisi kwanini?

Katafute msanii yoyote mkubwa wa hip-hop bongo muulize wasanii wake 5-10 Bora wa hip-hop Kwa sasa Bongo asipomtaja Dizasta vina njoo na uthibitisho nikupe 50k

Kwahiyo hawa wote hapa chini wao hawajui muziki ila wewe ndio fundi au sio?View attachment 2476038View attachment 2476040View attachment 2476041View attachment 2476042View attachment 2476043


Sent from my CPH1989 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom