Diwani wa Lugata - Sengerema ajiunga Chadema

Diwani wa Lugata - Sengerema ajiunga Chadema

Crashwise

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
22,227
Reaction score
8,760
Diwani wa kata ya Lugata(Adrian Tizeba) Sengerema amejiunga rasmi na chadema na ameondoka na mh Lema kutoka sengerema kwenda Geita ambapo atakabidhiwa kadi nakatibu mkuu wa chadema Dr. Slaa na kesho madiwani wanne jimbo la sengerema na wenyeviti wa vitongoji 22 watajiunga na chadema...

Source: Godlbess Lema

================
huyo diwani amekabidihiwa kadi ya chadema na slaa muda huu huko geita
attachment.php

Kwenye picha hapo juu Diwani Tabasamu(aliyevaa kombati wanaokumbatiana) akipokelewa na makamanda...Kwa mjibu wa Ben
 
Breaking News:

Aliyekuwa Diwani wa Kata ya Lugata (CCM) Wilaya ya Sengerema Adrian Tizeba amekihama chama hicho na kuhamia CHADEMA,

Diwani huyo kwa sasa yuko na Mbunge wa Arusha Mjini Mh. Godbless Lema pamoja na Katibu wa Chadema Kinondoni wakielekea kwenye mkutano wa hadhara Mjini Geita ambapo atakabidhiwa kadi yake mpya ya CHADEMA na Katibu wa Mkuu wa chama hicho Mh. Wilbrod Slaa,


Kwa Mujibu wa Mh. Lema, kesho atawatangaza Madiwani wengine wanne wa Jimbo la Sengerema (CCM) wakiwa na wenyeviti 22 wa vitongoji pamoja na wanachama wao ambao kwa pamoja wamehamua kukihama Chama cha Mapinduzi na Kuhamia CHADEMA wakilalamika kufilisikia kimawazo na kimtazamo kwa kilichokuwa Chama chao.

Sikiliza Arusha Mambo FM, tembelea www.arushamambo.com click ''Sikiliza Arusha Mambo FM..." na tutajiunga na na wenzetu walioko eneo la tukio ili kuwaletea mahojiano ya moja kwa moja ya kuhama kwa diwani huyo.

Source Arusha Mambo.
 
Diwani wa kata ya Lugata Sengerema Bw. Adrian Chiziba amejiunga na CHADEMA rasmi. Hii ni katika mkutano wa hadhara unaofanyika Geita chana huu ukihutubiwa na Dr. Slaa na Godbless Lema.
 
Diwani wa kata ya Lugata(Adrian Tizeba) Sengerema amejiunga rasmi na chadema na ameondoka na mh Lema kutoka sengerema kwenda Geita ambapo atakabidhiwa kadi nakatibu mkuu wa chadema Dr. Slaa na kesho madiwani wanne jimbo la sengerema na wenyeviti wa vitongoji 22 watajiunga na chadema...

Source: Godlbess Lema

Kanyaga twende......Pipoooooooooooooooooooozzzzzzzzzzz!!!!!!!!!!!!!!
 
Kuna watu humu JF watafukuzwa kazi! Hakyanani nawaambia maana ninajua huwa wanafikisha taarifa za uongo kwa wakubwa zao! Nape, timua wote hao nawe ujivue gamba ujiendee zako CCJ.
 
Diwani wa kata ya Lugata(Adrian Tizeba) Sengerema amejiunga rasmi na chadema na ameondoka na mh Lema kutoka sengerema kwenda Geita ambapo atakabidhiwa kadi nakatibu mkuu wa chadema Dr. Slaa na kesho madiwani wanne jimbo la sengerema na wenyeviti wa vitongoji 22 watajiunga na chadema...

Source: Godlbess Lema
Ama kweli hakuna marefu yasiyo na mwisho, yaani CCM ndo inakufa kifo kibaya namna hii! Hii nafikiri ni dhambi ya kuiua Tanganyika kwa makusudi. Kaaaazi kwelikweli!
 
msharaha wa dhambi ni mauti,ohhhhhhhhh marehemu CCM dhambi ya dhuruma imekufikisha hapo!
 
Back
Top Bottom