Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 734
Kama kiongozi sipendi kuwa mnafiki. Matatizo yangu sio matatizo ya watanzania wengi. Na matatizo ya watanzania wengi sio matatizo yangu. Sipandi daladala. Silali njaa. Watoto wangu hawaathiriki na migomo iwe ya mabasi, walimu au madaktari. Kufilisika kwa mifuko ya jamii hakunishtui.
Ujambazi haunisumbui sana kwa sababu ni silaha, nina walinzi, nina electric fence. Majirani zangu pia wanvyo vyote. Bei za sokoni hazinipi shida kwa sababu nanunua mahitaji yangu Supermarket. Barabara mbovu hazinikeri sana maana naendesha VX yenye air suspension! Foleni sio shida gari yangu in AC!
JE ni sababu gani kama kiongozi inayonifanya nitoke povu kujidai naumizwa na matatizo ya watanzania? Ni kwa nini watanzania hawaoni uongo na unafiki wa viongozi wao? Kwa nini wanakubali tunawadanganya mchana kweupe?
Msando Alberto - Diwani CDM kata ya Mabogini, Moshi Vijijini
Ujambazi haunisumbui sana kwa sababu ni silaha, nina walinzi, nina electric fence. Majirani zangu pia wanvyo vyote. Bei za sokoni hazinipi shida kwa sababu nanunua mahitaji yangu Supermarket. Barabara mbovu hazinikeri sana maana naendesha VX yenye air suspension! Foleni sio shida gari yangu in AC!
JE ni sababu gani kama kiongozi inayonifanya nitoke povu kujidai naumizwa na matatizo ya watanzania? Ni kwa nini watanzania hawaoni uongo na unafiki wa viongozi wao? Kwa nini wanakubali tunawadanganya mchana kweupe?
Msando Alberto - Diwani CDM kata ya Mabogini, Moshi Vijijini