Diwani CHADEMA arejea CCM

Diwani CHADEMA arejea CCM

To hell!a great idiot!!!he is none sense,rather than empty mind!!
 
WAKATI ikiwa katika mgogoro na madiwani wake wa Arusha, Chadema imepata pigo baada ya mmoja wa madiwani wake Singida kujiengua na kurudi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), akidai hataki kuwa sehemu ya machafuko nchini. <br />
<br />
Diwani huyo, Simon Tyosela wa kata ya Urughu, Iramba Magharibi, alisema hayo jana katika Ofisi ya Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, mbele ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia masuala ya Uchumi na Fedha, Mwigulu Mchemba. <br />
<br />
Tyosela aliyehamia upinzani wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 baada <br />
ya kuanguka katika kura za maoni ndani ya CCM, alisema hakushawishiwa kuihama Chadema na kurejea CCM, bali amenusa hatari kwa taifa katika siku za usoni. <br />
<br />
Alisema, maandamano yenye sura ya uchochezi kila kukicha, yamemkosesha amani na <br />
kujiona msaliti mbele ya Watanzania. <br />
<br />
“Haya ya kushinikiza wananchi kuiga maandamano katika nchi za wenzetu, tena yasiyo ya amani, binafsi yamenishinda. Chadema hakuna demokrasia ya kweli na nilitarajia ingekuwa mstari wa mbele kuhangaikia maendeleo ya wananchi. Nimejiondoa kwa sababu mimi ni mpenda amani kwa nchi yangu. <br />
<br />
“Kwa mtindo huu niliona kabisa hatuwezi kufikia malengo ya millennia, kwa sababu <br />
kila kukicha ni maandamano, hakuna la maana linalofanyika kwa ustawi wa nchi <br />
yetu,” alisema diwani huyo. <br />
<br />
Alisema, hana cha kujutia kwa sababu wananchi ndio waliokuwa wamemshawishi kuingia Chadema wakitaka atumie chama kingine chochote kuingia madarakani, baada ya kushindwa kura za maoni. <br />
<br />
Mchemba alimpongeza na kuitaka jamii kutokubali kuburuzwa na vyama vingine vya siasa kwa maslahi ya watu wachache wenye mwelekeo wa kulazimisha kushika madarakani kwa nguvu.
<br />
<br />

Kenge ni kenge tu hata arefuke vipi hawezi kuwa mamba. Kenge wengine waliojiingiza ktk kundi la mamba warudi kwa kenge wenzao. Tunahitaji ama ni bora tuwe na mamba wachanga kuliko kuwa na kenge wengi waliokomaa. Kuna msemo usemao kusikia kwa kenge ni kutoka damu masikioni.
 
Si mamluki wa kwanza kuondoka CDM, hiki ni chama cha makamanda wanaotenda kazi kwa maslahi ya umma, bora amejitoa mapema ameogopa kufukuzwa CDM hailei watu wa namna yake.
 
kuna wengine leo arusha sijui wataenda chama gani lakini hii ndiyo garama za kutafuta haki..

niliongea na diwani wa kata ya sekei nikamwuliza nini matarajio yake kuhusu matokeo ya cc, akaniambia atahamia nccr mageuzi, na vile vile ataweka court injection
 
Hata wakati wana wa israel wanatolewa utumwani misri kuna ambao walimlalamikia musa kuwa amewapeleka ili wakafie jangwani na walitamani kurudi misri kwa hiyo siyo ajabu kwa huyu diwani kurudi misri (ccm)
 
huyo diwani amefunguka macho cdm ni chama cha wavuta bangi
 
mbona mtu akitoka ccm akija cdm sisikii anguko la ccm ila hata m/kiti kutokea cdm utasikia anguko la cdm..

hapa jamvini watu wanapenda kusikia cdm imekufa leo au kesho..kitu kingine hizi ishu za cdm ni sawa na babu wa loliondo..

kila la kheli CDM ONE DAY YES!...
 
WAKATI ikiwa katika mgogoro na madiwani wake wa Arusha, Chadema imepata pigo baada ya mmoja wa madiwani wake Singida kujiengua na kurudi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), akidai hataki kuwa sehemu ya machafuko nchini.

Diwani huyo, Simon Tyosela wa kata ya Urughu, Iramba Magharibi, alisema hayo jana katika Ofisi ya Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, mbele ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia masuala ya Uchumi na Fedha, Mwigulu Mchemba.

Tyosela aliyehamia upinzani wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 baada
ya kuanguka katika kura za maoni ndani ya CCM, alisema hakushawishiwa kuihama Chadema na kurejea CCM, bali amenusa hatari kwa taifa katika siku za usoni.

Alisema, maandamano yenye sura ya uchochezi kila kukicha, yamemkosesha amani na
kujiona msaliti mbele ya Watanzania.

“Haya ya kushinikiza wananchi kuiga maandamano katika nchi za wenzetu, tena yasiyo ya amani, binafsi yamenishinda. Chadema hakuna demokrasia ya kweli na nilitarajia ingekuwa mstari wa mbele kuhangaikia maendeleo ya wananchi. Nimejiondoa kwa sababu mimi ni mpenda amani kwa nchi yangu.

“Kwa mtindo huu niliona kabisa hatuwezi kufikia malengo ya millennia, kwa sababu
kila kukicha ni maandamano, hakuna la maana linalofanyika kwa ustawi wa nchi
yetu,” alisema diwani huyo.

Alisema, hana cha kujutia kwa sababu wananchi ndio waliokuwa wamemshawishi kuingia Chadema wakitaka atumie chama kingine chochote kuingia madarakani, baada ya kushindwa kura za maoni.

Mchemba alimpongeza na kuitaka jamii kutokubali kuburuzwa na vyama vingine vya siasa kwa maslahi ya watu wachache wenye mwelekeo wa kulazimisha kushika madarakani kwa nguvu.

Ina maana huyu jamaa anamaanisha kuwa CHADEMA ni chama cha machafuko au? Huenda ana siri nzito kuhusu mpango wa machafuko kwa hiyo akamatwe ili aisaidie polisi kuzuia nchi isije ingia kwenye machafuko. Polisi fanyeni kazi yenu, makamateni mmuhoji ili awape clue ya anachosema kuwa hataki kuwa sehemu ya machafuko! Anasema hawezi kufikia malengo ya millenia; hivi anayajua kweli au ametoa tu tamko!
 
You have undeniably taken the right move.
 
kuna wengine leo arusha sijui wataenda chama gani lakini hii ndiyo garama za kutafuta haki..
nimeiona hii fb
Fadhila Lemba
TAHARIFA YA HARAKA RADO 1,VIONGOZ WA CHADEMA ARUSHA WAJIUZURU WASEMA'' tumechoshwa na chama kinachoendeshwa kama familia ya mboe na slaa,wakilala ksho wanahamka na hili mala lile bila kufata vkao vya chama,vita ya mboe anayompiga dk slaa ili asigombee urais 2015 na kumuachia nafas agombee yy wakat zito nae anataka yy agombee uenyekit wa chama mwakan na urais 2015 hivyo kila kiongoz anatafuta umaarufu si kwamaslahi ya nchi bali kujenga makundi yao kwa maslahi yao,tunaomba wana arusha watuelewe ili chama kitakapo vurugika mjue sababuni nini.tunawashukuru .
 
Na haya maandamano anayofanya Nape, Sitta, Mwakyembe, Lazaro Nyalando, Anne Kilango na wengine hayatishii amani? Diwani mzushi huyu!
 
Alivamia kichaka alifikiri cdm ni kama magambaz baada ya kujistukia kuwa yeye ni pumba kaamua kujiengua mwenyewe,hana upeo kaendekeza njaa wala c mzalendo mpenda nchi na ni bonge la mzushi
 
Hana jipya huyo..tumewazoea magamba..aliingia kwa nia ya kuvuruga, alipoona watu wapo stable kaamua kurudi kwa magamba wenzie!
 
Back
Top Bottom